Spika Ndugai aumizwa na chama cha siasa kutoleta Wabunge wa Viti Maalum, adai zingekuwa nafasi za wanaume wangelishafika

Mbona hajasema namna walivyowaibia kura hao hao kina mama wakipogombea majimboni?

Huyo Ndugai asilete propaganda katika jambo "very sensitive" kama hilo.

Nadhani akili zinaanza kuwarudia baada ya kuona kuwa wamefanya wizi Wa kitoto, kwa kuwa Kamati za Bunge zinapaswa kuongozwa na wabunge Wa upinzani, kama sharti kuu la wahisani wa maendelei wanaotuletea mapesa ya maendeleo

Kwa hiyo ndiko huko kuhaha na kuwabembeleza Chadema, eti wapeleke wabunge wa viti maalum!

Chadema kazeni hivyo hivyo msiwapeleke hao wabunge wa viti maalum, ili muonyeshe kwa vitendo namna mlivyochukizwa na wizi wao wa kura wa kitoto kabisa!
 
Viti maalum kupitia vyama vya saisa, viko vyama bado havijatuletea wabunge wao, tunachoona kwenye mitandao na mahali pengine eti wanalumbana eti wasiwalete sijui wawalete, yaani ni ajabu, aibu kubwa sana kwa vya vya namna hii
KUMBE wapeni TLP na UDP wagawane hizo nafasi huku pia wanawake wapo,wao wameshasema hawakubaliani na kilichofanyika sasa wapeni wengine au ni lazima wao bac sawa
 
sasa anaumia nn huyu ndu.guy wakati hicho ndicho bosi wake (Jiwe) anachokitaka?! kwamba wawepo ccm peke yao mjengoni kwakuwa wapinzani wanazuia maendeleo!

namshauri wabadili kanuni bungeni nafasi zote wajaze ccm kusudi nchi tupate maendeleo
Mbunge wa Nkasi ana akili sana.
 
Kwa sababu Watanzania wana kiu ya maendeleo ni vema Kama CCM wangechukuwa hizo nafasi ili kusiwe na watu wa kupinga hoja zao mjengoni. Maendeleo huletwa na chama kimoja sio vyama vingi.
 
Wajiongeze wao wenyewe, mbona wanajitekenya wenyewe kisha kujichekesha!!
 
Utawasubiri sana, endelea kupambana na ilani ya chama chako 2020-2025. Pia pambana na bajeti ya serikali.
 
Kama mna kila kitu na quoram inatosha kinachowawasha ni nini sio wewe uliyesema bunge hili hutaki kuona mpinzani hata mmoja.
 
Ili kukwepa hayo yote angewateua yeye mwenyewe toka kwenye chama chake CCM. Shida iko wapi??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…