Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Waliokuwa wanajiandaa kumwongezea Muda ndio waliosababisha kukatishwa Maisha aisee.Yani mpaka wanatia Huruma hawa UVCCM.
Majuva alikua karani wa Baraza la mawaziri Das musoma hapo anafanya nini?Alikuwa Das Musoma huko, amefariki wiki iliyopita.
Walikua kimya kumshauri mambo ya msingi pamoja na kuzingatia afya ya Rais leo anakuja na hoja ya miradi yaani anaona ni kitu cha muhimu mno bila kuzingatia usalama wa afya zao na wananchi kwa ujumla hata watu sijui tatizo lao nini...Who is she by the way?
Si wamjua marehemu na vimbwanga vyake?Majuva alikua karani wa Baraza la mawaziri Das musoma hapo anafanya nini?
Mwacheni ajichanganye, ngao yake imeondoshwaMuulizeni Ndugai vipi hata zile ndege alizonunua fedha zake zilipitishwa na bunge lini, aache unafiki sasa hivi hana mwega hawezi kurudi.
Bajeti kupitishwa na bunge ni kitu tofauti na upatikanaji wa pesa na utashi wa kisiasa kuendelea miradi yote hiyo kwa wakati mmoja, ndugai asipotoshe ummaLeo Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai wakati akitoa salamu za pole kufutia kifo cha Rais Magufuli, amewataka watanzania kuwa watulivu na kusema ilani ya CCM ya 2020 - 2025 na miradi yote ya maendeleo aliyoacha Rais Magufuli itatekelezwa kwani fedha zote za miradi hiyo zilikuwa zinapitishwa na Bunge.
Amewataka wabunge ambao kupitia kamati mbalimbali sasa hivi wako wanatembelea miradi hiyo kuwa watulivu.
=======
SPIKA NDUGAI: Ikumbukwe kwamba mheshimiwa Rais kwa nafasi yake ni sehemu ya pili ya Mhimili wa Bunge kwahiyo ni mdau wetu muhimu sana katika uendeshaji wa Bunge na shughuli za Bunge kwa ujumla wake kwahiyo tumepata pigo kubwa sana.
Natoa pole nyingi kwa mheshimiwa makamu wa Rais, mama Samia Suluhu, viongozi wa serikali, kipekee tunatoa pole nyingi sana kwa mama Janeth Magufuli, familia ya mheshimiwa Rais wetu lakini kikubwa zaidi kwa watanzania wote popote pale walipo.
Kama mnavyofahamu ndugu waandishi, waheshimiwa wabunge walikuwa katika ziara za kukagua miradi ya maendeleo kutokana na utekelezaji wa bajeti inayoendelea ambayo inaishia tarehe 30 June mwaka huu.
Imebidi tutoe wito na maelekezo kwamba, sasa wabunge wote waliokuwa katika waliokuwa katika ziara hizo za ukaguzi wa maendeleo warudi Dodoma haraka sana.
Kwahiyo wabunge wako njiani kutoka sehemu mbalimbali za nchi kurudi hapa Dodoma.
Kama tunavyojua, mheshimiwa Magugufuli ana mambo ambayo alijipambanua mapema, ni mengi sana lakini kwa kifupi alikuwa ndio Rais mjenga nchi hasa katika eneo la miundombinu. Miundombinu ya barabara, reli, bandari, shirika letu la ndege, ujenzi wa viwanja vya ndege, miradi mikubwa mikubwa ya maji, miundombinu ya elimu, eneo la afya. Sijui ni eneo gani utaweza kusema kwamba mheshimiwa Rais ameweka kumbukumbu ya aina yake.
Kwahiyo tunayo kazi kuwa sana sisi Watanzania ya kuhakikisha kwamba tunaendeleza nngwe ambayo amekwisha kuiweka ili kuhakikisha kwamba kazi zote alizokuwa akizisimamia ikiwemo ya utekelezaji wa ilani ya chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020-25 na kwa mambo mbalimbali ambayo aliyaainisha kupitia hotuba ambazo alizitoa hapa bungeni yeye mwenyewe tunaendelea kuzisimamia kwa faida kubwa zaidi ya Mtanzania.
Mama Samia ili afanikiwe afuate ya Tshikedi Kongo na ubia wa KabilaHili bunge la kuteuliwa livunjwe tu tuanze upya
Mungu amelipigania taifa, na kuonesha kila mtu anaweza kutuvusha. Na Taifa Lina hazina ya viongozi kibao, tuachane na wachumia tumbo ambao walitaka aongezewe mda kwa sababu ya kujijengea vitambi. Tuendelee kuomba ili wachumia tumbo waendelee kupigwa mapigo Kama ya faraoMbona tuliambiwa tumuongezee na muda kwamba bila yeye hakuna wa kutuvusha ?
Aione:-Mbona tuliambiwa tumuongezee na muda kwamba bila yeye hakuna wa kutuvusha ?