Spika Tulia: Bunge linataka mgao wa Umeme mpaka Juni uishe
Spika Tulia Akson aipa Wizara ya Nishati mpaka mwezi Juni 2024 kuhakikisha wanamaliza kabisa mgawo wa umeme.

Akiwa bungeni alipokuwa anaelezea jambo hilo Spika Tulia anasema

"Wacha tuipe serikali muda, kwa maana ipi wao walijipanga mwezi wa sita (shida ya umeme kuisha) wakarejesha nyuma mwezi wa pili, tunawapongeza sana na mmerejesha mpaka mwezi wa tatu kwa hizo mashine zote kukamilika, Bunge linawapa mpaka mwezi wa sita ili bunge linapokuwa hapa mgao uwe umeisha, tunawapongeza sana kwa kazi nzuri,"

Pia soma:
- Naibu Waziri wa Nishati: Mgawo wa umeme nchini utaisha mwezi wa tatu
Ukiona nchi ina ugaidi au uasi , usilamu magaidi au waasi , bali serikali ndo huandaa mazingira kwa ajili uasi au ugaidi kushamiri , yupo kijana kinyoz anajikuta mwez unaisha anamtafutia mwenye boma pia mabutcher pia wanaorusha muvi pia vitup vya afya vidogo private vya huko ndan ndan vinashindwa jiendesha sababu baadhi ya mashine za umeme hazifanyi kaz , hawa wote akisikia alshabib wanakulipa vzr haez endelea vumilia serikali ya kipuuz , SERIKALI ISILALE MUDA NI SASA , BAADAE ITAKUWA MAJOZI
 
Ukiwaona vile wamevaa suti zao aisee utasema tuna viongozi kweli.

Njoo kwenye kauli na vitendo aisee shetani ni bora.

Fikiria watu wangapi wanahitaji umeme kufanya shughuli zao na ukitazamia kuwa wengi wao hawamudu kununua majenereta.
 
Ipo siku waheshimiwa watapigwa makofi wanatuchukulia simple sana walipa kodi
Yale ya liberia mwaka 1980 yanaeza jirudia hapa bongo , serikali imelala sana na wanaolalamika hadi walio miongon mwao , MUDA NI MWL MZURI
 
Wako wapi wale maspika wanaojitambua?
Tulidhani jobo ndio worst spika kumbe .............
 

Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson, amesema kuwa Bunge limewapa Tanesco muda kufikia mwezi wa sita mgao wa umeme uwe umeisha.

"Wacha tuipe serikali muda, kwa maana ipi wao walijipanga mwezi wa sita (shida ya umeme kuisha) wakarejesha nyuma mwezi wa pili, tunawapongeza sana na mmerejesha mpaka mwezi wa tatu kwa hizo mashine zote kukamilika, Bunge linawapa mpaka mwezi wa sita ili bunge linapokuwa hapa mgao uwe umeisha, tunawapongeza sana kwa kazi nzuri," - Spika wa Bunge

Pia soma:
- Naibu Waziri wa Nishati: Mgawo wa umeme nchini utaisha mwezi wa tatu
Hatuna serikali makini
Hatuna mihimili makini
Hatuna viongozi makini
 
Baada ya Naibu waziri wa Nishati kusema mgao utapungua kwa mwezi huu wa pili kwa kiasi kikubwa na mwezi wa tatu mgao kuisha kabisa, Spika awaongezea muda mpaka mwezi wa sita ndio mgao uwe umeisha.

Spika amesema kwakuwa muda wa awali ulikuwa mwezi wa sita lakini wakapunguza na kusema mgao utaisha mwezi wa 3, basi Bunge limeiongezea muda serikali na hivyo mpaka mwezi wa sita wawe wamemaliza tatizo la mgao nchini.
Bunge wamechukua wap hayo maoni ya kuwaongezea muda wizara ya Nishati ? je walipiga kura bungeni ? viongoz washatudharau ila muda ukifika watalia na kusaga magego
 
Tulia ni spika mbovu kuwahi kutoa huyu kawa msemaji wa serikali.
 
Ukiwaona vile wamevaa suti zao aisee utasema tuna viongozi kweli.

Njoo kwenye kauli na vitendo aisee shetani ni bora.

Fikiria watu wangapi wanahitaji umeme kufanya shughuli zao na ukitazamia kuwa wengi wao hawamudu kununua majenereta.
Wabunge pamoja na supika hawajui kwamba umeme unachangia Sana kwenye Kodi ambayo ndio chanzo pekee Cha mapato Yao.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Bunge letu tukufu chini ya uongozi imara wa Nguli wa sheria kuwahi kutokea nyanda za juu kusini na Rais wa umoja wa mabunge Duniani, umeipa maagizo mazito serikali bya kuhakikisha kuwa ifikapo mwezi wa sita Mwaka huu basi tatizo na changamoto ya mgao wa umeme inafika tamati na kuwa mwisho na historia ya mgao wa umeme katika nchi hii ya asali na maziwa na ambayo Mungu ameijalia kila aina ya rasilimali na kila aina ya utajiri.

Bunge limetoa muda huo ambapo linaamini ni wakati huo ambapo mitambo yote katika bwawa la mwalimu Nyerere itakuwa imewashwa na kuanza kuzalisha umeme.

Nisiwe na maneno mengi na kuharibu habari hii njema kabisa kwa mamilioni ya watanzania wanyonge ambao wanaendelea kuwa watulivu na wenye subira kwa kila jambo linalokuja mbele yao.
Habari njema ipi we jamaa!mbona unakua kama mpumbavu!we unaona mwezi wa sita ni karibu??vijana wengi ajira zao zinaathirika kwa ajili ya umeme mf saloon, fundi wa kuchomelea nk!halafu we unasema umeme kupatikana mpaka mwezi wa sita ni habari njema!
 
Kuna mambo hayapaswi kuvumiliwa mojawapo ni hili la umeme.

Lakini kuwavumila wapumbavu kama huyu jamaa humu jukwaani ni uzembe sana. Lucas ni mtu wa hovyo sana, analitumia jukwaa kujifunza propaganda.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Bunge letu tukufu chini ya uongozi imara wa Nguli wa sheria kuwahi kutokea nyanda za juu kusini na Rais wa umoja wa mabunge Duniani, umeipa maagizo mazito serikali bya kuhakikisha kuwa ifikapo mwezi wa sita Mwaka huu basi tatizo na changamoto ya mgao wa umeme inafika tamati na kuwa mwisho na historia ya mgao wa umeme katika nchi hii ya asali na maziwa na ambayo Mungu ameijalia kila aina ya rasilimali na kila aina ya utajiri.

Bunge limetoa muda huo ambapo linaamini ni wakati huo ambapo mitambo yote katika bwawa la mwalimu Nyerere itakuwa imewashwa na kuanza kuzalisha umeme.

Nisiwe na maneno mengi na kuharibu habari hii njema kabisa kwa mamilioni ya watanzania wanyonge ambao wanaendelea kuwa watulivu na wenye subira kwa kila jambo linalokuja mbele yao.
Kaka eeh Kuna wakati Ni bora ukawa unanyamaza Tu
 
Habari njema ipi we jamaa!mbona unakua kama mpumbavu!we unaona mwezi wa sita ni karibu??vijana wengi ajira zao zinaathirika kwa ajili ya umeme mf saloon, fundi wa kuchomelea nk!halafu we unasema umeme kupatikana mpaka mwezi wa sita ni habari njema!
Hajawah kuwa na akil huyo
 
Back
Top Bottom