Spika Tulia: Tusichanganye Maadili ya Mtanzania na Imani za kidini. Lipi kosa la walimu waliosimamishwa kazi Kwa kucheza muziki? Warudisheni kazini

Tangu amekuwa Rais wa IPU amekuwa na maamuzi ya Akili sana hata jana alimnyamazisha mwigulu akamwambia wabumhe wakillamika kuibiwa sio uongo hela kweli zimeibiwa...
Yaan kwa kweli, sijui awe ana maanisha, na vitendo afanye pia.
 
Walimu ni kundi la watumishi linaloonewa na kukandamizwa sana na wanasiasa maamuma.
 
Siyo kila nyimbo inapigwa kila mahali, watoto wanapaswa kufundishwa maadili mema, Maudhui ya ile nyimbo yanafaa watu walioko kwenye ma-bar na magenge mengine ya wahuni
Wimbo shule haupigwi ila nyumbani unapigwa na mauno yanakatwa.
 
Hata bila Spika kuhoji,yeye Kwa akili yake anaona ni sawa kuimba wimbo huo Shuleni?

Mdau kasema hapo tuwe na versio mbili za public na parental
Yeah mkuu kwa sababu BASATA Hawana mfumo huo hapo wa kwanza kiwajibika angekuwa BASATA na wizara ya Michezo kwa ujumla kwa sababu wameshindwa kufanya Censorship ya nyimbo ambazo hazina maasili kama sio kuzifungia kabisa au kuna double standard kwenye kufungia nyimbo zinaangaliwa zinazopinga serikali tu?
 
Ni kweli Kuna viongozi hawatofaitishi kati Imani au maadili ya kidini na maadili ya jumla ya Mtanzania
Na hapo ndio changamoto...
Linatakiwa Somo lianze kufundishwa kuhusu hasa ni IPI MILA/MAADILI YA MTANZANIA ili watu watofautishe na Tamaduni za kidini...
Kwa mfano kuwa na wake wengi hiyo ni mila ya mtanzania ila kidini hasa ukristo hairuhusu kwahyo mtu akioa watu watamwona kaenda kinyume na maadili..

Kwahyo inabidi uchorwe mstari kuhusu maadili ni yapi na Ipi ni tamaduni za kidini
 
Lilikuwa ni swali la Mbunge aliuliza kwahyo na yeye akaamua kuchagiza..angalia atached video utaelewa..hata ya CAG pia amegongelea msumali na kasema kuna pesa kweli zimeibiwa
 
Walimu ni kundi la watumishi linaloonewa na kukandamizwa sana na wanasiasa maamuma.
Huu ni ukweli sana unakuta eti mpaka mwenyekiti wa mtaa na kitongoji anawakoromea walimu na anajifanya boss wake tukiamua kuwatetea kuna watu wanakuja juu wanataka walimu waendelee kuonewa hii sio sawa...

Wanafnya kazi kwwny mazingira magumu hebu tuwape motisha sio kuwakandamiza..
Kitu hicho hicho akifanya mkuu wa mkoa,Mbunge ,mkurugenzi na watumishi wengine haikiitwi kuvunja maadili ila akifanya yeye anavunja maadili hebu tuae na huruma...
 
Nje ya mada kidogo


Hivi suala la Mdundo wa Taifa limefikia wapi pamoja na vazi la Taifa
 
Spika yupo sahihi wanaopasa kutimuliwa ni wale waliouruhusu huo wimbo uendelee kuwepo Nchini bila kuufungia !!
 
Spika yuko sahihi, kama wimbo huo hauna maadili kwanini BASATA wameupitisha upigwe kwenye jamii? Hao walimu walikuwa wameonewa , pia ikumbukwe hapo shuleni kulikwa na hafla ndo mziki huo ukapigwa je walimu wangezuia watoto wasicheze? Darasa la 7 Huwa wana graduation zao na huwa wanacheza miziki hiyo hiyo na wanafanyia shuleni.
 
Siyo kila nyimbo inapigwa kila mahali, watoto wanapaswa kufundishwa maadili mema, Maudhui ya ile nyimbo yanafaa watu walioko kwenye ma-bar na magenge mengine ya wahuni
Ndiyo maana kasema warudishwe kazini HALAFU NJIA SAHIHI ZIFUATWE..!! Wale walimu wakishitaki kuhusu utaratibu itakuwaje..!!?? Sababu kama hizi ndo zinatufanya hadi leo tunalimwa mafaini kisa kuna mtu mmoja hakufuata taratibu kwenye kuvunja mikataba iliyopo kisheria.
 
Mimi kama 'DJ' hapa nimekuelewa zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…