TANZIA SSGT Reginald Ruta wa JWTZ amejiua kwenye Kaburi la marehemu Mkewe

TANZIA SSGT Reginald Ruta wa JWTZ amejiua kwenye Kaburi la marehemu Mkewe

Daa Mungu atusaidie, wengine tukiwa na nyumba ya kuishi na ka usafir naona dunia yangu wengin wananyumba za ziada bado usafiri wa ziada upo na anaona dunia imemdhulumu. Hakika tumwombe alietuumba atupe tu utulivu wa nafsi. Kwa sababi bila hili hakika ndio mtu anaishia kufanya maamuzi kama haya
 
Sababu ya huyu Mgambo kujiua ni Majuto. Namuita mgambo sababu mwanajeshi kamili hawezi kujiua kizembe namna hii. Kiufupi jamaa alikuwa mbali na mke wake kimahusiano. Kifo cha mke wake asilimia kubwa kimesababishwa na tabia na matendo yake yasiyokuwa mazuri. So alijiona kakosea na hakuna tena nafasi ya kumuomba msamaha mkewe. To me haya ni maamuzi yenye ubinafsi. Nafikiri kifo cha mkewe kingekuwa turning point ya yeye kuwa mtu bora zaidi kwa familia na jamii kwa ujumla kuliko kujiua. Hili tukio limetokea mtaani kwangu so hiki nilichoandika siyo story ya kutunga.
Basi ni laana maana kuna wanawake wakifa kwenye mateso ya ndoa yanayotokana na mume basi husema kabisa nikifa huyu mtu hachukui round atanifuata na inakuwa kweli.
Ndo hicho kilichotokea.
Babangu alikuwa mjeda so I know, hawa watu kuua au kujiua ni mara moja tu
 
Duh! Huyu alikuwa anampenda sana Mkewe. Hakustahili kuachwa peke yake hata kwa dakika chache. Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi 🙏🏾🙏🏾🙏🏾
Kwa ambaye anamfahamu SSGT Ruta alikuwa Msata amejiua kwenye kaburi la mke wake ambaye alifariki siku ya Jumamosi huko kilakala kaacha ujumbe kuwa alikuwa anampenda mke wake.

========

Dar es Salaam. Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Reginald Ruta amekutwa amekufa huku mwili wake ukiwa juu ya kaburi la mkewe, Godebertha aliyezikwa katika makaburi ya Mekyuri Kipawa jeshini mkoani Dar es Salaam.

Juni 7, mwaka huu mwili wa askari huyo aliyezikwa katika makaburi hayo jana, ulikutwa katika kaburi la mkewe aliyefariki dunia Alhamisi iliyopita baada ya kuugua ghafla.

Kifo cha askari huyo wa kambi ya Msata mkoani Pwani kimeacha simanzi kwa ndugu, jamaa na marafiki, kwa kuwa kilitokea siku tatu tangu mkewe afariki.

Akisoma risala kwenye ibada ya kuaga mwili wa askari huyo, iliyofanyika nyumbani kwake mtaa wa Karakata Kipawa, diwani wa Karakata, Idary Karugendo alisema marehemu ameacha watoto wanne na wajukuu watano waliokuwa wanamtegemea.

“Mzee Ruta alikuwa tegemeo kwenye familia yake kama baba, hasa baada ya kifo cha mke wake kutokea siku chache zilizopita,” alisema Karugendo.

Akizungumza katika ibada hiyo, Katekista wa Kanisa Katoliki la Bikira Maria Kipawa, Silivester Sadick alisema kifo hicho ni funzo kubwa kwa watu wote na kinaonyesha wazi hakuna binadamu mkubwa mbele ya Mungu.

“Juzi tulikuwa hapa hapa, tena nawaongoza kwenye ibada ya kumuaga mke wake, hakuna aliyekuwa anajua nani anafuata lakini leo mzee Ruta anafuata, ni funzo kubwa ndio maana nawakumbusha kuzidi kumuomba Mungu wakati wote,” alisema.

Alisema kifo kinaharibu mipango yote ambayo binadamu anakuwa amejipangia kuitekeleza na ndiyo maana watu husema kifo hakina huruma, lakini ukishakufa unakwenda kwa Mwenyezi Mungu.

“Maisha ya hapa duniani yanapita, juzi tulizungumza hatujui nani anafuata, lakini mume ameenda, kama maisha yetu yako namna hii binadamu ni nani mbele ya Mungu.

Familia ipo kwenye wakati mgumu, kama ingekuwa ni mimi leo ingekuwaje, kikubwa tujitengenezee njia ya kufika mbinguni mapema na naiomba familia kuzidi kufanya maombi na kusimama katika imani kwa Mungu kwani hawezi kuwaacha,” alisema.

Kifo kilivyotokea

Kwa mujibu wa jirani mmoja ambaye hakutaka kutaja jina lake, alidai kuwa walikuwa wote na Ruta siku ya Jumamosi ambayo yalifanyika mazishi ya mkewe aliyefariki ghafla wakati akijiandaa kwenda kazini.

Alisema baada ya mazishi Jumatatu iliyopita, vijana waliokuwa wanachunga mbuzi waliukuta mwili wake juu ya kaburi hilo.

Chanzo hicho kilieleza kwamba watoto hao baada ya kuona mwili huo wakaenda kutoa taarifa jeshini kwa sababu eneo hilo linamilikiwa na Jeshi na walipofika pale wakampekua hawakuona chochote zaidi ya kitambulisho chake.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa baada ya mazishi ya mkewe, Jumapili iliyopita Ruta alifanya vikao vya mara kwa mara na watoto wake wanne na kuwaeleza mali alizonazo na sehemu zilipo.

“Baada ya kufanya vikao virefu na watoto wake huku akiwachekesha muda wote, aliwaambia kuwa atakwenda kununua marumaru kwa ajili ya kujengea kaburi la mkewe na aliwaeleza kuwa akishafanya manunuzi atawaeleza,” zinaeleza taarifa hizo.

Habari zaidi zinaeleza kuwa alimuomba mwanaye mmoja ampe Sh50,000 kwa ajili ya kununua marumaru hizo na alipopewa fedha hizo aliondoka nyumbani hakurejea tena.

Polisi wanena

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Ilala, Janeth Magomi alikiri kupokea taarifa ya kifo na kudai ililetwa na wanajeshi wenzake kutoka kituo cha Polisi Stakishari.

“Kwamba kuna mwenzao wamemkuta amefariki juu ya kaburi la mkewe, wakati wanatoa taarifa hiyo tayari mwili ulishachukuliwa na kupelekwa hospitali ya Lugalo,” alisema Janeth.

View attachment 1815077
View attachment 1815080
 
Kipo alichokikosa kwa mkewe huku akiamini hawezi kuishi bila yeye, na mbaya zaidi akakosa hata faraja ya walimwengu
Afande huenda alikuwa maryo! Hivihivi haiingii akilini kwa mtu wa umri wake kujipiga risasi as simple as that. Angekuwa kijana mdogo sawa, mzee tena mwenye wajukuu?! No.
 
Kabisa Mkuu ndiyo sababu vifo vya Mzazi, Mke/Mume na mtoto huitwa misiba mikubwa kwani wahusika 9/10 times huumia zaidi wanapofikwa na misiba ya hawa watu.
Maumivu ya moyo wewe acha tu
 
Kama Mkewe alifariki kisha na yeye ndio hivyo basi hajawatendea haki watoto wake.
Labda inawezekana Katoka kujipima VVU bila kupata ushauri nasaha.

Mzazi unapofanya maamuzi kama haya ni rahisi sana tukio kama hili la kujiua kuja kujirudia tena kwenye familia. Anawafanya watoto wake wakiwa kwenye Sonona nao waone njia rahisi ni kujiua.

Hakuna mtu anajiua kwasababu ya kukutwa na VVU siku hizi!!! Ukimwi sio passport ya kifo tena; kuna dawa watu wanakunywa na wala huwezi jua kuwa wameathirika.
 
Afande huenda alikuwa maryo! Hivihivi haiingii akilini kwa mtu wa umri wake kujipiga risasi as simple as that. Angekuwa kijana mdogo sawa, mzee tena mwenye wajukuu?! No.

Inawezekana kilichommaliza ni kwamba yeye kazi yake ilikua kutafuta pesa na wife alikua mhasibu mkuu na bibimanunuzi mkuu wa familia..... Na inawezekana hapo alipojiua alikua hajui hata zinakokaa socks na boxer zake..... inawezekana hajuagi hata bei ya vest wala chupi, yeye anachojua ni kutafuta pesa tuuu

Wewe unaweza kuviona vidogo ila kwake ni mzigo mkubwa sana tena usiobebeka
 
Inawezekana kilichommaliza ni kwamba yeye kazi yake ilikua kutafuta pesa na wife alikua mhasibu mkuu na bibimanunuzi mkuu wa familia..... Na inawezekana hapo alipojiua alikua hajui hata zinakokaa socks na boxer zake..... inawezekana hajuagi hata bei ya vest wala chupi, yeye anachojua ni kutafuta pesa tuuu

Wewe unaweza kuviona vidogo ila kwake ni mzigo mkubwa sana tena usiobebeka
Hakuna kitu kama hicho ni Obsession tu, TZ yote hii akosekane mwanamke mwingine wa kupanga bajeti!!
 
Dah, poti kazingua sana. Ila poa tu .
Hivi Mshana Jr hujawahi kuwa pale milambo barracks na jamaa mmoja alikuwa anaitwa zero zero? Alikuwa MP then akajoin kufanya mortuary
 
Hii ni depression lakini kibongobongo tunaichukulia poa kisa mjeshi lazima awe na roho ya chuma.
Comments za baadhi ya watu humu zimenifanya niache kusoma huu uzi..watu wanahukumu ile mbay hadi moyo unaniuma

Watu hawaoni jinsi huyu mtu alivyopata sonona kwa kufiwa
Huwezi jua waliishi vipi na mkewe

msione watu wanatembea jmn
Watu sio wazima.,kila mtu anajua msalaba wake
 
Back
Top Bottom