TANZIA SSGT Reginald Ruta wa JWTZ amejiua kwenye Kaburi la marehemu Mkewe

TANZIA SSGT Reginald Ruta wa JWTZ amejiua kwenye Kaburi la marehemu Mkewe

Hakuna cha Uchawi wala shangazi yake ulozi,
Kwenye familia nyingi ikitokea Mama katangulia basi Baba huwa hachukui round, hapa nazungumzia watu wanaopendana kwa dhati.

Wababa wana roho ndogo sana wanapofiwa na wake zao tofauti na wamama ambao wakiangalia watoto basi wanajikaza na maisha yanasonga.
 
Unakuta kuna muda mtu unawaza, bora uanze wewe kufa, uwaache vipenzi wako. Lakini analopanga Mola halina makosa.

Sisi huwa tunaomba mwisho mwema, sababu kujiua ni kuidhulumu nafsi yako na ni kosa kubwa pia.
 
Alikuwa hana sifa ya uanajeshi. Mwanajeshi anapohesabika amekufa kishujaa ni anapokuwa vitani anapoona ametekwa au kuliko kutoa siri kwa maadui ni aheri ajitoe uhai huyu ndio mwanajeshi.

Ila mwanajeshi anayejiua sababu za hovyo hovyo za kis?$*&%$##nge za kidunia mfano mapenzi huyo alikuwa mwanajeshi feki hata vitani angeweza kusaliti wenzake.

Kwa kawaida mwanajeshi wa aina hii huwa akifa hazikwi kwa heshima za kijeshi
 
Kwa ambaye anamfahamu SSGT Ruta alikuwa Msata amejiua kwenye kaburi la mke wake ambaye alifariki siku ya Jumamosi huko kilakala kaacha ujumbe kuwa alikuwa anampenda mke wake.

========

Dar es Salaam. Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Reginald Ruta amekutwa amekufa huku mwili wake ukiwa juu ya kaburi la mkewe, Godebertha aliyezikwa katika makaburi ya Mekyuri Kipawa jeshini mkoani Dar es Salaam.

Juni 7, mwaka huu mwili wa askari huyo aliyezikwa katika makaburi hayo jana, ulikutwa katika kaburi la mkewe aliyefariki dunia Alhamisi iliyopita baada ya kuugua ghafla.

Kifo cha askari huyo wa kambi ya Msata mkoani Pwani kimeacha simanzi kwa ndugu, jamaa na marafiki, kwa kuwa kilitokea siku tatu tangu mkewe afariki.

Akisoma risala kwenye ibada ya kuaga mwili wa askari huyo, iliyofanyika nyumbani kwake mtaa wa Karakata Kipawa, diwani wa Karakata, Idary Karugendo alisema marehemu ameacha watoto wanne na wajukuu watano waliokuwa wanamtegemea.

“Mzee Ruta alikuwa tegemeo kwenye familia yake kama baba, hasa baada ya kifo cha mke wake kutokea siku chache zilizopita,” alisema Karugendo.

Akizungumza katika ibada hiyo, Katekista wa Kanisa Katoliki la Bikira Maria Kipawa, Silivester Sadick alisema kifo hicho ni funzo kubwa kwa watu wote na kinaonyesha wazi hakuna binadamu mkubwa mbele ya Mungu.

“Juzi tulikuwa hapa hapa, tena nawaongoza kwenye ibada ya kumuaga mke wake, hakuna aliyekuwa anajua nani anafuata lakini leo mzee Ruta anafuata, ni funzo kubwa ndio maana nawakumbusha kuzidi kumuomba Mungu wakati wote,” alisema.

Alisema kifo kinaharibu mipango yote ambayo binadamu anakuwa amejipangia kuitekeleza na ndiyo maana watu husema kifo hakina huruma, lakini ukishakufa unakwenda kwa Mwenyezi Mungu.

“Maisha ya hapa duniani yanapita, juzi tulizungumza hatujui nani anafuata, lakini mume ameenda, kama maisha yetu yako namna hii binadamu ni nani mbele ya Mungu.

Familia ipo kwenye wakati mgumu, kama ingekuwa ni mimi leo ingekuwaje, kikubwa tujitengenezee njia ya kufika mbinguni mapema na naiomba familia kuzidi kufanya maombi na kusimama katika imani kwa Mungu kwani hawezi kuwaacha,” alisema.

Kifo kilivyotokea

Kwa mujibu wa jirani mmoja ambaye hakutaka kutaja jina lake, alidai kuwa walikuwa wote na Ruta siku ya Jumamosi ambayo yalifanyika mazishi ya mkewe aliyefariki ghafla wakati akijiandaa kwenda kazini.

Alisema baada ya mazishi Jumatatu iliyopita, vijana waliokuwa wanachunga mbuzi waliukuta mwili wake juu ya kaburi hilo.

Chanzo hicho kilieleza kwamba watoto hao baada ya kuona mwili huo wakaenda kutoa taarifa jeshini kwa sababu eneo hilo linamilikiwa na Jeshi na walipofika pale wakampekua hawakuona chochote zaidi ya kitambulisho chake.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa baada ya mazishi ya mkewe, Jumapili iliyopita Ruta alifanya vikao vya mara kwa mara na watoto wake wanne na kuwaeleza mali alizonazo na sehemu zilipo.

“Baada ya kufanya vikao virefu na watoto wake huku akiwachekesha muda wote, aliwaambia kuwa atakwenda kununua marumaru kwa ajili ya kujengea kaburi la mkewe na aliwaeleza kuwa akishafanya manunuzi atawaeleza,” zinaeleza taarifa hizo.

Habari zaidi zinaeleza kuwa alimuomba mwanaye mmoja ampe Sh50,000 kwa ajili ya kununua marumaru hizo na alipopewa fedha hizo aliondoka nyumbani hakurejea tena.

Polisi wanena

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Ilala, Janeth Magomi alikiri kupokea taarifa ya kifo na kudai ililetwa na wanajeshi wenzake kutoka kituo cha Polisi Stakishari.

“Kwamba kuna mwenzao wamemkuta amefariki juu ya kaburi la mkewe, wakati wanatoa taarifa hiyo tayari mwili ulishachukuliwa na kupelekwa hospitali ya Lugalo,” alisema Janeth.

View attachment 1815077
View attachment 1815080
Mkiambiwa muwe na michepuko hamsikii, ona sasa. Anakosaje mke mdogo wa pembeni? Hili ni tatizo
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Inawezekana kilichommaliza ni kwamba yeye kazi yake ilikua kutafuta pesa na wife alikua mhasibu mkuu na bibimanunuzi mkuu wa familia..... Na inawezekana hapo alipojiua alikua hajui hata zinakokaa socks na boxer zake..... inawezekana hajuagi hata bei ya vest wala chupi, yeye anachojua ni kutafuta pesa tuuu

Wewe unaweza kuviona vidogo ila kwake ni mzigo mkubwa sana tena usiobebeka
Upo sahihi kabisa. Nilisema vile kwa sababu niliamini ktk umri wake ule ameshashudia mambo mazito ikiwemo hata vifo vya ndg zake wa karibu kiasi kwamba moyo na ubongo vimeshakuwa na uwezo kuhimili mambo mazito!
 
Pole sana kwa watoto na familia, siku zote kauli yangu ni kutokushindwa, nipitie misuko suko na mateso ya nafsi na mwili kama Mwenyezi Mungu hajaamua kunichukua, hakika siwezi idhulumu nafsi yangu na niwaachao.

R.I.P Ruta.
 
Hujapenda wewe...hata mimi naweza jitoa uhai kwaajili ya mapenzi...wee acha kbs!ndo maana kasema wanaye wamsamehe

Nilikuwa na mawazo kama ya kwako, na nilikuwa pia na hisia kama za kwako, ila kwa sasa nishakuwa sugu[emoji81][emoji23], yaani ni kama ambulance vile unalia huku safari inaendelea.
 
Asilaumiwe huzuni ilinishinda nguvu. Au anajisikia vibaya labda ni yeye alisababisha mke kutangulia. Hizi Mali unaweza kufanya utaniutani ukaingia kwenye maagano yakakucost.
 
Nilikuwa na mawazo kama ya kwako, na nilikuwa pia na hisia kama za kwako, ila kwa sasa nishakuwa sugu[emoji81][emoji23], yaani ni kama ambulance vile unalia huku safari inaendelea.
Mimi hata kwenye usugu nimepita.. sijui niko stage gani nw🤣🤣
 
Yaani amekutwa tuu amekufa juu ya kaburi kwa kuugua ghafla?

Njia pekee ninayoiona ni yeye kunywa sumu na kulala/kwenda hapo kusubiri kifo, japo kutetea hoja hii inahitaji nguvu...
Halafu wamelizika na kuamua kumzika fasta tuuh??

Anyway R.I.P.

Kuna vitu kidogo hata mimi naona vipo tofauti ilitakiwa ichunguzwe vizuri
 
Back
Top Bottom