Stan Katabalo: Tunauhitaji mzimu wako wa habari za Uchunguzi!

Stan Katabalo: Tunauhitaji mzimu wako wa habari za Uchunguzi!

Tungepata mtu anaejua mjane aliko angekuwa anatunzwa jamani umenikumbusha mbali sana, alifia msumbiji kwenye ule mkutano sijui ulikuwa wa nini!!
Nawafahamu watoto wake watatu Charles , Kazaula na Rweyemamu kuna kaka yake na marehemu anaishi kibaha elimu sehemu moja inatwa Mwanalugali pia kuna mdogo wake na Marehemu Katabalo inatwa Mzee Slivesta Katabalo alikua mwalimu wa Shule ya Secondary Nyakato nje kidogo ya mji wa bukaba Mjini anaishi kijiji kimoja kinatwa Buhembe ukifika Nyakato ukaulizia familia ya Katabalo utapelekwa.
 
Kama ambavyo itatuchukua miaka 100 kumpata raisi kama mwalimu Nyerere ndivyo ambavyo itatuchukua miaka 100 kumpata Stan Kabalo mwingine katika uandishi wa habari. Stan Katabalo alikuwa ni zaidi ya mwandishi wa habari. Leo hii maripota wanajiita waandishi wa habari wakati hakuna cha maana wanachofanya zaidi ya kugombania posho/bahasha na kujisajili kwenye kambi (mitandao) zinazogombea uraisi 2015 wakati Watanzania hasa vijijini wanahitaji kuelimishwa mambo ya msingi na kalamu za waandishi wa habari.
Sasa tunaye Magufuli
 
Haya magazeti yapo kweli tena?...hivi magazeti yaliyo kwenye mrengo wa ukosoaji mfano Raia mwema (ambayo wewe ni mwandishi wa makala humo) hufanya pia habari za kiuchunguzi ?
Kwa sasa gazeti la Jamhuri la kina Manyerere Jackton ndio wamejipambanuwa kuandika habari za uchunguzi lakini tatizo kubwa naliona ni resources.

Huwezi kufanya investigation journalism huku una njaa na unatamani bahasha za kaki, hawa watu wanahitaji grants za kuwawezesha kufanya kazi bila kutegemea takrima kutoka kwa mtu.

Sasa hivi tuna waandishi wanazurula tu mitandaoni kuokoteza habari then wanaunganisha tayari news room.

Ndio maana ukimuuliza Mtanzania mgogoro wa Urusi na Ukraine atakueleza vizuri, lakini ukimuuliza tatizo la Ngorongoro na Loliondo ni nini hawezi kukupa majibu kwa sababu hajui lolote, ni kwa nini hajui lolote ni kwa sababu wenye jukumu hilo la kuupa umma ukweli wa mambo wamekimbia majukumu yao.

Sasa hivi kila siku kuna press za machawa tu, Haji Manara, Mwijaku na Baba Levo na waandishi wanafurika, hawa machawa ni kila siku wanaita press mahotelini.

Powered by bahasha ya kaki.
 

Attachments

  • Screenshot_20220513-055015_Facebook.jpg
    Screenshot_20220513-055015_Facebook.jpg
    28.1 KB · Views: 10
  • Screenshot_20220513-053848_Facebook.jpg
    Screenshot_20220513-053848_Facebook.jpg
    80.3 KB · Views: 11
Ndio maana ukimuuliza Mtanzania mgogoro wa Urusi na Ukraine atakueleza vizuri, lakini ukimuuliza tatizo la Ngorongoro na Loliondo ni nini hawezi kukupa majibu kwa sababu hajui lolote, ni kwa nini hajui lolote ni kwa sababu wenye jukumu hilo la kuupa umma ukweli wa mambo wamekimbia majukumu yao.

Powered by bahasha ya kaki.
Nimeguswa!.
RIP Stan Katabalo.
P
 
Kashfa ya Loliondo ilitufundisha mengi,tulijua kuwa wawekezaji uchwara walipokuja mara ya kwanza - Loliondo 1 hawakwenda Bungeni bali nyumba nyeupe; waliporudi tena kwenye Loliondo - 2 hawakwenda Bungeni bali nyumba nyeupe, na mwaka ule alipokuja tena mwana wa Zayed hakwenda Bungeni bali nyumba nyeupe! Nyumba nyeupe ndio mlango wao rahisi kabisa na ndio wamekuwa wakiutumia,kama nyumba nyeupe wakitaka kubadilisha sera wanaweza! RIP Stan Katabalo.
 
Raisi Mwinyi ndio aliamrisha kuuawa kwa Stan Katabalo ! Full stop ! Na sasa raisi mchongo Samia anaamrisha wamasai wa Ngorongoro wauwawe ! Period !!!
 
genekai,
Kabendela shinani hakuuwawa na yeyote bali ali commit suicide kwa kujitupa ziwani na watu waliona kile kitendo.

Alitoka nyumbani asubuhi akiwa ndani ya gari yake. akaegesha gari bandarini, kulikuwa na meli ya MV Victoria imetia nanga pale Bukoba, akaingia ndani ya meli na kujitupa majini kwenye maji ya kina kirefu.

Issue yake ni kwamba yeye ni mzaliwa wa Kagera ambaye aliamia Rwanda akaoa huko na kuchukua uraia na kuishi huko. Baada ya ile genocide ya Rwanda alikimbia kurudi huku kama mkimbizi. Lakini kwa kuwa alijua yeye ni mzaliwa wa hapa aliishi nje ya makambi ya wakimbizi na bahati mbaya sana alianza kujiingiza kwenye mambo ya siasa.

Wakati huo huo akiwa Rwanda alikuwa mtangazaji wa redio pale Rwanda, na mwakilishi wa BBC pia pale Rwanda. Lakini pia inaaminika alikuwa rafiki sana wa marehemu rais Habyalimana. Baada ya kifo cha Habyalimana kulitokea machafuko yaliyosababishwa na umwagaji damu sana. Na yeye alikuwa mmoja kati ya watu waliochochea sana through propaganda (kumbuka anayofanya yule Kibonde wa clouds?) mauaji katika radio na baadhi ya wenziwe walikuwa wameshakamatwa na kupelekwa Rwanda na wengine walikuwa Arusha.

Kwa kujihusisha kwake na siasa hapa kulimzalishia maadui na wakafichua siri kuwa pamoja na kwamba yeye alikuwa mzaliwa wa Tanzania lakini alishakana tayari uraia wa Tanzania na kupewa uraia wa Rwanda na kwamba alishawahi kumiliki passport ya Rwanda. Hilo lilifanya watu wa uhamiaji waanze kumuhoji na kumfuatilia sana na kutaka kujua kwa nini hakuwa anaishi katika makambi ya wakimbizi na kwa nini aliwahi kuomba passport ya Tanzania kwenda nje bila kusema ukweli kuwa yeye si raia wa nchi hii? Jambo hili lilimtia hofu sana.

Kwa hofu kwamba wangeweza kumrudisha makambini au kumrudisha Rwanda au kumkabidhi kwa makachero wa Rwanda waliokuwa wanamtafuta at that time, aliona bora ajiue na hivyo akafanya kama alivyofanya. Ilikuwa ni kuogopa mkono wa serikali ya Rwanda.
No body killed him but he killed himself. Familia yake wengine walirudi Rwanda wengine bado wako hapa Tanzania.
Kuna ukweli kadhaa katika maandishi yako ingawa pia Kuna uongo mwingi Sana.Ni kweli kwamba Kabendera alijitosa ziwa Victoria na kufariki Dunia.Kabendera alizaliwa na kukulia Kagera,alihamia Rwanda baada ya RPF ya akina Kagame kuchukua madaraka.Akiwa huko ndo alitofautiana na Kagame na ikabidi arudi Kagera .Alikamatwa anajiandikisha kama mpiga kura.Akafunguliwa kesi kwakuwa alishaukana uraia wa Tanzania.Kwa kipindi kirefu Kabendera alikuwa mwandishi wa BBC bila shida.Kabendera asingeweza kukaa makambini ilihali asili yake ni Katoro hapo Kagera ,alichoharibu ni kuchukua paspot ya Rwanda.Ni kosa kubwa kumhusisha Kabendera na mauaji ya kimbari ya Rwanda na pia kumhusisha na Habyarimana ni kumkosea Kabendera.
 
Kuna ukweli kadhaa katika maandishi yako ingawa pia Kuna uongo mwingi Sana.Ni kweli kwamba Kabendera al8jitosa ziwa Victoria na kufariki Dunia.Kabendera alizaliwa na kukulia Kagera,aligamia Rwanda baada ya RPF ya akina Kagame kuchukua madaraka.Akiwa huko ndo alitofautiana na Kagame na ikabidi arudi Kagera .Alikamatwa anajuandisha kama mpiga kura.Akafunguliwa kesi kwakuwa alishaukana uraia wa Tanzania.Kwa kipindi kirefu Kabendera alikuwa mwandishi wa BBC bila shida.Kabendera asingeweza kukaa makambini ilihali asili yake ni Katoro hapo Kagera ,alichoharibu ni kuchukua paspot ya Rwanda.Nu kosa kubwa kumhusisha Kabendera na mauaji ya kimbari ya Rwanda na pia kumhusisha na Habyarimana ni kumkosea Kabendera.
Mkuu balibabambonahi , asante sana for this, marehemu watendewe haki. Hivyo huku ni kumtendea haki Kabendera Shinani.
P
 
Siamini sana uchawi lakini kifo chake kinasemekana kulikuwa na mkono wa mtu.

Aliwasumbua sana jamaa na kashfa ya Loliondo na mpaka walitishia kumuua lakini hakuacha kuandika. Tulikuja kushtukia amekufa tayari lakini alikuwa ni mwandishi mahari ambaye akianza kuriporti tukio ni mwanzo mpaka mwisho. Lakini Ndolanga (mkurugenzi wa wanyama pori wakati ule na Rais Mstaafu Mwinyi) wanaweza kueleza kilichomkuta!!! Inawezekana alilishwa sumu bila kujua.

RIP Stan Katabaro. Hivi alikufa na gazeti lake la mfanyakazi? Mbona silioni wala kulisikia siku hizi?

Tiba
hivi ni mfanyakazi au motomoto hebu tuwekane sawa sababu ni kitambo.
 
Nafikiri watu wengi mnakumbuka yule mwandishi wa habari miaka ya themanini na tisini marehemu stan Katabaro,alikuwa ni mwandishi mahiri kwa miaka ya leo hana tofauti na Saed Kubenea,Johnson Mbwambo,nauliza kifo chake kilisababishwa na nini hasa?wanaokumbuka watujuze
CCM watakuwa walipita naye kama kawa
 
Back
Top Bottom