Starehe za Mlimani City na bei za ajabu ajabu

Starehe za Mlimani City na bei za ajabu ajabu

M/city haina uzuri wowote, samaki samaki pia ni yakawaida sana. Nimekula chips samaki pale mara kadhaa na juice, bei zao ni za wastani kwangu mimi, sio ghali na wala sio rahisi kivile. Mara ya mwisho kuwa pale tulikuwa na kampani ya Lugumi na alitoa ofa kwa wadada waliokuwa pale mida ya saa kumi na moja hivi jioni. Ingawa Lugumi hakuwa na kawaida ya kunywa whisky ama beer kutoka bar, mabaunsa wake walikuwa wanashuka na vinywaji kutoka kwenye msafara wake ndio alikuwa anakunywa hivyo. Wakuu muwe mnatembea na kuingia sehemu expensive walau mara tano kwa mwaka. Sasa mkuu ukienda Moyo Kitchen ama Coral Ridge Spur si ndo utazimia kabisa wewe, Maisha mafupi wakuu tembeeni musipige mahesabu sana.

so hiyo moyo kitchen nayo ni mall?
 
Hayo maeneo huwa sisogelei nikiwa vibaya mfukoni, mara nyingi naendaga nikiwa na wajomba zangu tu maana kuna vimichezo wanavyopenda ila wakileta tamaa tamaa inakuwa ticket ya kuwarudisha home.[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Ice cream tu na pipi za buku 5 zinawatosha.

Nakumbuka ilikuwa ni sehemu ya mabishoo kwenda kuwinda vyupi, sijui hilo jambo linaendelea hadi leo.
Hii ilikua mda sio sasa mlimani city enz hizo miaka ya 2007 mbona vitu vilikua rahisi yaani kila weekend nilikua naenda kwasababu nilikua nakaa mwenge alafu mule ndani kuna hadi mahabusu ndogo ujue
 
Hivi wakuu nyie mnawezaje kumudu bei za pale kuanzia vyakula mpaka vinywaji?
Kuna siku nimeuziwa glass ya juice ya pineapple 5000, mpka nikajicheka, nikauliza popcorn za chumvi eti 4000..wale watu sidhani kama wapo serious..
Imefika muda nikienda yale maeneo nakuwa mziko kutumia visenti vyangu, hivi nyie mnaokula pizza, bugger na kulewa pale samaki samaki mnaweza vipi? Au mnajitoa akili tu?

Tafuta hela tu boss...ukiwa nazo hizi ni bei ndogo sana wala hutagundua

Ukitaka juice ya nanasi zilizooza basi swekeni zimejaa tele
 
Chai laki 6?huwez kuwa seriuz.kuwa makini na 0 na alama za uandishi mkato nk.
Siku ya kwanza kwenda mlimani city, mara paa nakutana na mshikaji, ilikua kama sa 4 alafu hata sikua nimekunywa chai, tukakaa kwenye mgahawa, tukaagiza vitu vya kawaida kabisa. Bili kuja 60,000.00, na mfukoni nilikua na hiyo hivyo 60 ikabidi niende ATM pale niongezee kidogo ila nilichoka. Ilikua early 2010s.
 
Kitu kinachotupa bei, katika uchumi, ni makutano ya curves za demand na supply, ceteris paribus (all factors being equal).

Katika curves za supply/ demand zinazotupa price kwenye uchumi, kuna abnormal curves.

Kawaida, katika free market, kwa ceteris paribus, price ikiwa chini watu wengi wanakuwa na uwezo wa kununua kitu, demand inakuwa kubwa kuliko supply, bei inapanda mpaka demand, supply na price vinapo stabilize.

Kwa mfano wa Mlimani City, bei za chini zinaweza kujaza watu hapo mpaka ikawa vurugu, pakawa hapakaliki. Na wenye biashara wakiona kwamba kuna wateja wapo hata tukipandisha bei, watapandisha, mpaka pale watakapoona hapa sasa tukipandisha zaidi tutakosa wateja.

Kawaida kitu kinavyozidi kuongezeka price, demand inazidi kupungua.

Lakini, kuna abnormal curves zipo katika vitu kama "luxury goods", kuna vitu vingine vikiwa na bei ya juu ndipo watu wanavitaka, vikiwa na bei ya chini inaonekana kama feki.

Yani inawezekana kitu kisiwe na chochote cha ajabu, ila ile branding tu inafanya bei iwe juu, na watu wanaotaka kujionesha wana hela za kununua vitu vya bei ya juu watanunua.

Ndiyo maana unasikia Kanye West katoa raba inauzwa kwa dola za Marekani 350! Na watu wanaunua, wanataka waonekane wamevaa kitu cha bei mbaya.

Kwenye sehemu za starehe, kuna watu wamejijengea mawazo kwamba sehemu zenye vitu vya bei rahisi zitajaa watu wasio na hela wenye matatizo mengi na wasio na ustaarabu, na kwamba ukienda sehemu za vitu vya bei mbaya utaepuka kukutana na matatizo ya ku socialize na watu wa ngazi za chini za jamii.

Inawezekana hapo Mlimani City/Samaki Samaki panafuata abnormal curve ya "luxury goods/services".

Ila Mlimani City kwa mfano Samaki Samaki kusema unatanua kiota cha maraha naona bado sana.

Nilipelekwa na wadogo zangu nilivyorudi likizo, kufika tu, mwenyewe najua hapa hakuna mtu anayenijua, mchizi mmoja akaanza kupiga kelele kama kaona jini ananiita jina langu, anawaambia watu "mnamjua huyu nani? Mnamjua huyu nani?" kama vile Prince Akim kwenye "Coming To America", nikamwambia cool down, you are putting me on the spot.Jamaa hakutegemea kabisa kuniona pale kwa sababu nilikuwa nimejichimbia nje miaka 10 kabla ya hapo.

Kwa hiyo labda kama sehemu inayoweza kuwakutanisha watu waliotengana siku nyingi, watu wakajua kwamba pale ndipo wanyamwezi wote tunaoshuka Dar tutafika, panaweza kuwa na maana.

Na tukirudi na hivyo vidala vyetu, hizo juisi za sh 5,000 hata USD 2 hazijafika bado, kwa hiyo hatuoni cha ajabu kulipa kama hilo litamaanisha tunakutana na long lost friends.

But the place could be better.
 
Hii ilikua mda sio sasa mlimani city enz hizo miaka ya 2007 mbona vitu vilikua rahisi yaani kila weekend nilikua naenda kwasababu nilikua nakaa mwenge alafu mule ndani kuna hadi gereza dogo ujue
ilo gereza unahukimiwa ukifanya kosa mda gani na kusomewa mashtaka mda gani na kuhukumiwa?
 
Hayo maeneo huwa sisogelei nikiwa vibaya mfukoni, mara nyingi naendaga nikiwa na wajomba zangu tu maana kuna vimichezo wanavyopenda ila wakileta tamaa tamaa inakuwa ticket ya kuwarudisha home.🤣🤣🤣🤣🤣

Ice cream tu na pipi za buku 5 zinawatosha.

Nakumbuka ilikuwa ni sehemu ya mabishoo kwenda kuwinda vyupi, sijui hilo jambo linaendelea hadi leo.

🤣🤣🤣 hata wewe jamani. Mbona wanaume jamii ni stingy hivi. Mlimani city pale vitu bei poa sana tu.
 
Back
Top Bottom