Ina maana umeropokwa tu ? Kama hivyo ndivyo wewe ni muongo au una matatizo ya akili,inakuwaje anaweka mambo usiyo yajua ?
Sijaelewa swali lako.Wewe unaweza kunipa ushahidi Abunuwasi hayupo au hajawahi kuwepo?
Au unaweza kunipa ushahidi wale Sungura wanaozungumza kwenye hadithi za watoto hawajawahi kuwepo?
Hiyo ni ya KweliStory ya Ester, bahati bukuku alitusimulia kupitia wimbo wake wa waraka,
Yaani kuanzia Wimbo unaanza unaweza kwenda sokoni kununua dagaa, unarudi unapika, unamalizia kusonga ugali ndio utasikia wimbo umefikia "ooh Ester aah kwa mahombi huku akisindikizwa na mioyo ya wayaudi" .
Du hapo tulipigwa.
🤪🤣🤣Ni kweli hiyo.Kama Mungu aliumba Adam na Hawa na wakazaa watoto wawili tu ina maana duniani palikuwa na watu wanne tu. Je hao watu aliokuwa akiwaogopa Kaini ni akina nani? Je huyo mwanamke alielala na Kaini na kuzaa nae mtoto alitoka wapi?
Wataalamu hebu naomba mtusaidie hapa
Sijaelewa swali lako.
Unamuongelea Muandishi au ? Lakini mfano wako ni tofauti na habari za Dini. Naomba ulinganishe habari za dini na habari za visa vya Abuu Nuwas ? Huyu alikuwa mshairi mwenye kujulikana,baba yake alikuwa Muarabu na mama yake alikuwa na asili Irani,aliitwa Abū Nuwās al-Ḥasan ibn Hānī al-Ḥakamī.
Ninachokuomba mimi utoe ulingano kati ya habari za Abuu Nuwas na habari za dini,kwa uchambuzi wa kielimu. Ukishindwa nitakusaidia kisha uje ukiri ya kuwa wewe ni mjinga katika hili.
Nimekuuliza wewe swali hilo,unaniuliza mimi tena ?Habari za dini yako zina tofauti gani na visa vya Abu Nuwas?
Naomba nikujibu swali lako kama ifuatavyo.Kwamba Mungu aliumba dunia na kila kilichomo (sawa) kisha akaumba mwanaume na kuumba mwanamke kwa kumtoa ubavu mmoja mwanaume (sawa).
Kisha hao wawili (Adam na Eva/Hawa) wakazaa watoto wawili (Kaini na Abeli) - (sawa).
Kisha Abeli akawa mfugaji na Kaini akawa mkulima (sawa). Lakini Mungu alipendezwa zaidi na sadaka za Abeli kuliko za Kaini (sawa). Kaini akamuua kaka yake kwa wivu (sawa).
Mungu akampa adhabu Kaini kwa kumfukuza bustanini awe anatanga tanga huku na huko duniani (sawa).
Kaini akamwambia Mungu kuwa akitangatanga watu atakaokutana nao watamuua (shida inaanza kuja hapa). Mungu akamwekea alama usoni ili walimwengu wasimuue (shida inaendelea). Kaini akaenda huko nchi ya Nodi mashariki mwa Eden.
Kisha kaini akalala na mkewe akamzaa mtoto aitwae Henoki. (Sio sawa).
Reference: Soma kitabu cha Mwanzo 4:1-17.
Hii story haija balance kabisa hasa hapo mwishoni. Kama Mungu aliumba Adam na Hawa na wakazaa watoto wawili tu ina maana duniani palikuwa na watu wanne tu. Je hao watu aliokuwa akiwaogopa Kaini ni akina nani? Je huyo mwanamke alielala na Kaini na kuzaa nae mtoto alitoka wapi?
Wataalamu hebu naomba mtusaidie hapa.
Naomba nipe reference katika biblia nasoma wapi hiyo hadithi. Na pia naomba kukuuliza je hao malaika waasi ni watu?Naomba nikujibu swali lako kama ifuatavyo.
1, kabla ya kuwepo au kuumbwa kwa adamu mbinguni kulitokea vurugu ambayo majeshi ya malaika yalijigawa, robo tatu ya malaika yakawa upande wa shetani ambaye alitaka kuweka mapinduzi mbinguni na robo iliyo bakia ikabaki upande wa Mungu na mda ambao mapinduzi ya shetani kutaka kuchukua kiti cha Mungu ndo mda ambao Mungu alikuwa yupo duniani kuumba yaani kuyagawanya maji, n.k
Hivyo lile kundi lililo mfuata shetani lilishushwa duniani ila Adamu na eva walifichwa katika bustani ya edeni, na baada ya kutenda dhambi alitoka nje ya bustani na kujitengenezea majani ya miti kama kujistili kutokana na walijiona wapo uji, na kama wewe ni msomaji mzuri wa bible kuna pahara Mungu anauliza Adamu upo wapi, maana kwenye bustani hakuwepo.
Kwa hiyo Kaini alienda kuoa majitu yale ambayo ni malaika waasi kutoka mbinguni na majitu hayo nadhani ndio wa Nefili ambao Mungu aliwaonya kuwa wanadamu wasichangamane na hao majitu wa kuoa / kuolewa.
kama kuna swali nakaribisha
Wacha upuuzi wako, nani aliyekuambia Qur'an ni ujumbe wa ulimwengu wote.....usipende kujipa ujinga, una akili za kuzaliwa zitumie.Hujathibitisha nililo kuuliza.
Nalusaidia kwa swali lako rahisi sana. Naizungumzia Qur'aan.
Mtume alikuwa ni katika Waarabu,na ndiyo maana Qur'aan imetermshwa kwa lugha ya Kiarabu.
Kisha ikawafikia wasio kuwa Waarabu sababu ni ujumbe kwa walimwengu wote.
Mola akajaalia ukijifunza jambo unalijua hata kama si la lugha yako. Watu wakafundishwa lugha ya Kiarabu na wakaelewa. Leo hii ukienda bara la arabu au ukisoma historia ya wajuzi wa kiarabu kiasili si Waarabu.
Sasa usiwe mjinga kukataa jambo usilo kuwa na elimu nalo.
Hakuna aliye zaliwa anajua,hata wewe bila kufindishwa leo hii usingejua kusoma wala kuandika,yaani ungebweteka.
Sasa nataka uthibitishe ya kuwa Qur'aan imeandikwa yaani imetungwa ba Mwanadamu.
Pinga kwa hoja usilete utoto katika mambo ya kielimu.Wacha upuuzi wako, nani aliyekuambia Qur'an ni ujumbe wa ulimwengu wote.....usipende kujipa ujinga, una akili za kuzaliwa zitumie.
Mkuu tutajie huyo aina ya samaki aliyemeza Yunus....??? Tukianzia hapo itakuwa sawaSasa chai hapo iko wapi ? Kwani kitu hakiwezi kuwa hai ndani ya kitu kingine ?
Lakini habari ya kumezwa na Samaki Chewa ni habari ya haki na huu ni katika muujiza.
Allah mtukufu anasema :
139. Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
140. Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
141. Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
142. Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
143. Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
144. Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
145. Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
146. Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
147. Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
148. Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda. (as-Saffat : 139 - 148)
Sijui ni Samaki gani. Jenga hoja yako sasa.Mkuu tutajie huyo aina ya samaki aliyemeza Yunus....??? Tukianzia hapo itakuwa sawa