Suala la mzee Mwinyi kuzikiwa Zanzibar wala lisifanywe la kisiasa, pitieni hapa msome muelewe sababu

Suala la mzee Mwinyi kuzikiwa Zanzibar wala lisifanywe la kisiasa, pitieni hapa msome muelewe sababu

Mwinyi ameishi maisha yake zaidi Bara kuliko huko visiwani. Ndiyo maana hata baada ya kufa ameendelea kuishi bara na si visiwani. Na nyumba yake ya kustaafu akajengewa na Magufuli Dar .... kwa nini hawakumjengea kwao Zanzibar ...... Hata Mwanaye pia maisha yake ameishi zaidi bara .... wanamzika kule kimkakati!!
"Ndiyo maana hata baada ya kufa ameendelea kuishi bara"!? Na wachawi wamo kwenye msafara.
 
Usihofu, mtoto wa mzee MWINYI akiitwa HASSAN nae amezikwa Zanzibar, kwa hiyo hatakua mpweke.
Na kama kuna ulazima wa kupeleka udongo Mkuranga utapelekwa.
Atleast wewe nimekuelewa, so hopefully na Mama Siti nae siku yake ikifika ataenda kupumzishwa Zanzibar, if this is the case, nafunga mjadala.

But then again, kama haya yalifahamika mapema, kwanini familia "ikakaa kikao" ili kuamua wapi imzike mpendwa wao?

- Huyo mtoto wake Hassan kama alikuwa na familia Zanzibar, kwa nafasi yake akaamua kuzikwa huko, maamuzi yake hayawezi kuingiliana/ kufanana kivyovyote na yale ya baba yake.

Baba yake tunaambiwa amekaliwa kikao, kukaa kikao sio maana yake hawakujua wapi wamzike? au palikuwepo na mawazo yanayopingana kuhusu wapi pa kumzika?

Mimi naona hiyo option ya pili ndio sababu, wakaamua iwe kumzika Zanzibar kwa manufaa ya kisiasa ya mwanae, nafungua tena mjadala ...

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Vipi wanaopinga Mwinyi kuzikwa Zanzibar huku wakidai kuwa mzee Mwinyi ali usia akifa azikwe Mkuranga. Wewe ushawahi kuuona au kuusikia huo usia wa Mkuranga kutoka katika kinywa cha Mwinyi mwenyewe?
Wanaosema hivyo watakua wamesikia kwa jamaa mmoja huko kwamtandao pendwa.
Tena walizushia mzee wawatu kifo kisha wakakanusha wenyewe.
 
Mwinyi hata nyumba Zanzibar Hana, Sasa alikuwa anaishi Kwa nani, AU kwenye Yale maflat ya pale unguja ?
 
Watanzania tupeane pole kwa msiba huu mzito katika taifa letu.

Kuna watu wanashangazwa na hili swala la kuamua kuhamisishia msiba wa mzee Mwinyi Zanzibar, wakidai kuwa mzee huyo alikuwa asha usia kuwa akifariki ...
Wewe ndo msemaji wa familia!? CHAWA mpenda Ubwabwa misibani
 
Hapa sio suala la maneno mengi yasiyo na msingi, ni suala la desturi zetu na kuzifuata. Kawaida desturi zetu inaonesha zinaenda kinyume na kile familia walichoamua.

Jiulize; vipi kama Dr. Mwinyi asingekuwa Rais wa Zanzibar leo, baba yake still angezikwa huko Zanzibar peke yake awaache ndugu zake wengine wazikwe Mkuranga? Jibu ni hapana.

Politics imeamua destiny ya Mzee Mwinyi kwa manufaa ya kisiasa ya mwanae.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Unarudi kulekule kwenye maneno ya kuungaunga nilikokukataa mimi.

Unasema desturi zetu hivi na vile, desturi za nani? Unajua unapotulundika wote katika "zetu" unakosea? Hapo kuna makabila tofauti, dini tofauti, misimamo ya kifalsafa tofauti, unaelewa neno "zetu" linaweza kukosa maana?

Mlikubaliana wapi hizo desturi? This is a logical fallacy, argument from tradition, problem of induction.

Ali Hassan Mwinyi ndiye mtu wa kwanza kuzaliwa bara, kwenda kuwa rais wa Zanzibar, na kuwa rais wa Tanzania. Hakuna precedent ya mtu mwingine yeyote mwenye historia hiyo, sasa utatumia vipi desturi kumzika mtu ambaye maisha yake hayako defined na desturi, mpaka leo watu wanabishana kama Mwinyi ni Mzanzibari au mtu wa bara?

Unatumia vipi desturi kumzika mtu ambaye maisha yake hayako easily defined ki desturi?

Habari yoyote ya "ingekuwa mtoto wake si rais wa Zanzibar asingezikwa huko" ndiyo hizo ninazosema habari za kuunga unga. Hujui Mwinyi alifikiri nini, aliienzi Zanzibar vipi, una speculate tu.

Mimi si rais wala nini, nimeishi tu Marekani, nimepapenda, nimesema nikifa nisirudishwe Tanzania. Mazishi yangu yafanyike Marekani. Sasa ikiwa mtu kama mimi nimeamua hivyo, kwa nini iwe ajabu Mwinyi kuzikwa Zanzibar sehemu ambayo bado ni ndani ya Tanzania na huhitaji hata passport kwenda?

Huna ushahidi kwamba politics ndiyo imeamua wapi Mwinyi azikwe, hizo ni simple stories za kijiweni tu.

Manapenda sana conspiracy theories.
 
Hebu tutazame hili jambo kwa upana wake, issue hapa sio passport, hao watu wanaozikwa huko nje mostly hushindwa kurejeshwa nyumbani kuzikwa kwasababu za ukosefu wa kifedha, nyie diaspora huwa mnajichangisha mwisho wa siku mambo huwa magumu.

Lakini kwa Mzee Mwinyi, hakuna chochote walichokosa kushindwa kumzika Mzee Mkuranga walipozikwa ndugu zake wengine, kwenda kumzika Zanzibar ninaona kabisa hajatendewa haki, na sitaki kuamini kama yale yalikuwa maamuzi yake.

Jiulize, kwanini baada ya Mzee kufariki familia ikakaa kuamua wapi azikwe? kwani kwa kawaida hawajui mtu akifariki anatakiwa kuzikwa kwao? hizi ni siasa ndio zimeamua hatma ya Mzee Mwinyi (RIP) wala sio maamuzi binafsi ya marehemu.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Kwanza si kweli kwamba watu wanaozikwa nje wanashindwa kurejeshwa nyumbani kuzikwa kwa sababu za ukosefu wa fedha.

Hapo ndipo mna[poshindwa wabongo wengi, mnaishi kw akukariri kariri mambo.

Kuna watu tupo nje hatutaki kuja kuzikwa Tanzania, tumeamua kuondoka Tanzania kimoja, kuja kuishi nje, na kuanzisha maisha nje, na tukifa tuzikwe huku.

Na hatuna tatizo la fedha, tunalipia ada watoto wasio na uwezo huko Tanzania kila mwaka, watu wanaofulia kulipa kodi za nyumba wanatufuata kila mwaka tunawalipia.

Na mara nyingine tunakaa miaka mingi nje bila kurudi Tanzania kwa kufuata kazi zetu tu, kw akuamua.

Sasa kwa hesabu zako za kukariri, utaona watu wanaoamua kuzikwa nje hawana fedha.


Last time I came to Tanzania I spent about $20,000, kwenye likizo ya wiki tatu.

Na nimeamua nikifa nisizikwe Tanzania.

Sasa hapo utasema nimeamua nisizikwe Tanzania kwa sababu ya gharama za kusafirisha mwili?
 
Wekeni clip akiongea azikwe Mkuranga
Waswahili mna mambo
Hapo Mzee kwao ni Znz period
 
Kwanza si kweli kwamba watu wanaozikwa nje wanashindwa kurejeshwa nyumbani kuzikwa kwa sababu za ukosefu wa fedha.

Hapo ndipo mna[poshindwa wabongo wengi, mnaishi kw akukariri kariri mambo.

Kuna watu tupo nje hatutaki kuja kuzikwa Tanzania, tumeamua kuondoka Tanzania kimoja, kuja kuishi nje, na kuanzisha maisha nje, na tukifa tuzikwe huku.

Na hatuna tatizo la fedha, tunalipia ada watoto wasio na uwezo huko Tanzania kila mwaka, watu wanaofulia kulipa kodi za nyumba wanatufuata kila mwaka tunawalipia.

Na mara nyingine tunakaa miaka mingi nje bila kurudi Tanzania kwa kufuata kazi zetu tu, kw akuamua.

Sasa kwa hesabu zako za kukariri, utaona watu wanaoamua kuzikwa nje hawana fedha.


Last time I came to Tanzania I spent about $20,000, kwenye likizo ya wiki tatu.

Na nimeamua nikifa nisizikwe Tanzania.

Sasa hapo utasema nimeamua nisizikwe Tanzania kwa sababu ya gharama za kusafirisha mwili?
Kukaa kwako nje Bado haukuondolei kuwa mjinga.
 
“Na ile mifupa ya Yusufu ambayo wana wa Israel waliileta kutoka Misri, wakaizika katika nchi ya Shekemu. Katika shamba alilonunua Yakobo”.
 
Kukaa kwako nje Bado haukuondolei kuwa mjinga.
Hapana.

Ujinga ni kumuona mtu mjinga kwenye maamuzi aliyoyachukua kwenye maisha yake ambayo huyajui, kwa sababu zake ambazo huzijui.

Watanzania wengi mna kasumba ya kutoheshimu maamuzi ya binafsi ya watu wengine.

Mnaishi kwa sheria za kukaririshana ambazo hazina kichwa wala mguu.

Mimi nikizikwa nje ya Tanzania, wewe inakupunguzia nini?

Na wewe hujatoka katika lindi la upumbavu huu.

Mimi nimeamua kutozikwa Tanzania.

Wewe kulazimisha hilo kuwa ujinga bila hata kuwa na udadisi wa kujua sababu zangu ndiyo ujinga wenyewe.

Watanzania wengi kama wewe hamuwezi kusema "hiki ni jambo binafsi la ntu, tumuachie aamue mwenyewe".

Mmezoea kuishi kwa kupangiana maisha mpaka sehemu ya kuzikwa mnataka kupangiana. Mnajipa umuhimu mkubwa kwenye maisha ya watu ambao hamuwajui na wao hawawajui.

Kama hapa ushajipa umuhimu kwenye maisha yangu, unataka kunipangia mazishi yangu yawe wapi, nikiamua yawe nje mimi mjinga.

Upumbavu mtupu.
 
Unarudi kulekule kwenye maneno ya kuungaunga nilikokukataa mimi.

Unasema desturi zetu hivi na vile, desturi za nani? Unajua unapotulundika wote katika "zetu" unakosea? Hapo kunamakabila tofauti, dini tofauti, misimamo ya kifalsafa tofauti, na neno "zetu" linaweza kukosa maana?

Mlikubaliana wapi hizo desturi? This is a logical fallacy, argument from tradition, problem of induction.

Ali Hassan Mwinyi ndiye mtu wa kwanza kuzaliwa bara, kwenda kuwa rais wa Zanzibar, na kuwa rais wa Tanzania. Hakuna precedent ya mtu mwingine yeyote mwenye historia hiyo, sasa utatumia vipi desturi kumzika mtu ambaye maisha yake hayako defined na desturi, mpaka leo watu wanabishana kama Mwinyi ni Mzanzibari au mttu wa bara.

Unatumia vipi desturi kumzika mtu ambaye maisha yake hayako easily defined ki desturi?

Habari yoyote ya "ingekuwa mtoto wake si rais wa Zanzibar asingezikwa huko" ndiyo hizo ninazosema habari za kuunga unga. Hujui Mwinyi alifikiri nini, aliienzi Zanzibar vipi, una speculate tu.

Mimi si rais wala nini, nimeishi tu Marekani, nimepapenda, nimesema nikifa nisirudishwe Tanzania. Mazishi yangu yafanyike Marekani. Sasa ikiwa mtu kama mimi nimeamua hivyo, kwa nini iwe ajabu Mwinyi kuzikwa Zanzibar sehemu ambayo bado ni ndani ya Tanzania na huhitaji hata passport kwenda?

Huna ushahidi kwamba politics ndiyo imeamua wapi Mwinyi azikwe, hizo ni simple stories za kijiweni tu.

Manapenda sana conspiracy theories.
Mkuu uko smart sana, Great.
 
Unarudi kulekule kwenye maneno ya kuungaunga nilikokukataa mimi.

Unasema desturi zetu hivi na vile, desturi za nani? Unajua unapotulundika wote katika "zetu" unakosea? Hapo kunamakabila tofauti, dini tofauti, misimamo ya kifalsafa tofauti, na neno "zetu" linaweza kukosa maana?

Mlikubaliana wapi hizo desturi? This is a logical fallacy, argument from tradition, problem of induction.

Ali Hassan Mwinyi ndiye mtu wa kwanza kuzaliwa bara, kwenda kuwa rais wa Zanzibar, na kuwa rais wa Tanzania. Hakuna precedent ya mtu mwingine yeyote mwenye historia hiyo, sasa utatumia vipi desturi kumzika mtu ambaye maisha yake hayako defined na desturi, mpaka leo watu wanabishana kama Mwinyi ni Mzanzibari au mttu wa bara.

Unatumia vipi desturi kumzika mtu ambaye maisha yake hayako easily defined ki desturi?

Habari yoyote ya "ingekuwa mtoto wake si rais wa Zanzibar asingezikwa huko" ndiyo hizo ninazosema habari za kuunga unga. Hujui Mwinyi alifikiri nini, aliienzi Zanzibar vipi, una speculate tu.

Mimi si rais wala nini, nimeishi tu Marekani, nimepapenda, nimesema nikifa nisirudishwe Tanzania. Mazishi yangu yafanyike Marekani. Sasa ikiwa mtu kama mimi nimeamua hivyo, kwa nini iwe ajabu Mwinyi kuzikwa Zanzibar sehemu ambayo bado ni ndani ya Tanzania na huhitaji hata passport kwenda?

Huna ushahidi kwamba politics ndiyo imeamua wapi Mwinyi azikwe, hizo ni simple stories za kijiweni tu.

Manapenda sana conspiracy theories.
Naona hautaki kulundikwa kwenye desturi zetu, mindset ya kimarekani imekuingia unaanza kuzikataa mila na desturi zako, hata kama huzitaki, wazazi wako na ndugu zako wengine wanazifuata, hiyo ndio sababu iliyonifanya nikachagua kutumia neno "zetu" nikimaanisha waswahili, sio wakina wewe "swahili-zungu".

Hapa pia kuna angle ya pili niiite social status.

Mzee Mwinyi alikuwa mtu mzito hapa Tanzania -Rais Mstaafu, hivyo kwangu sioni ubaya yeye kujadiliwa, hata nawe huwa unakuwa kwenye upande wa kuunga mkono mtu mwenye nafasi kwenye jamii kuzungumziwa, nikikumbuka umekuwa ukilaumu taarifa za viongozi wagonjwa kwenda nje kutibiwa kufanywa siri na serikali.

Sasa sijui kwanini hapa kwa marehemu Mzee Mwinyi umeamua kugeuka kuwa mtu wa kutaka "ushahidi wa vikao vya kifamilia", kwanini wakati ule wa ugonjwa wa viongozi huwa huulizii ushahidi wa ugonjwa wa kiongozi toka kwa familia yake kwanza, badala yake huishia tu kuitaka serikali isitufiche habari zao kwenda kutibiwa nje?



Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Kwanza si kweli kwamba watu wanaozikwa nje wanashindwa kurejeshwa nyumbani kuzikwa kwa sababu za ukosefu wa fedha.

Hapo ndipo mna[poshindwa wabongo wengi, mnaishi kw akukariri kariri mambo.

Kuna watu tupo nje hatutaki kuja kuzikwa Tanzania, tumeamua kuondoka Tanzania kimoja, kuja kuishi nje, na kuanzisha maisha nje, na tukifa tuzikwe huku.

Na hatuna tatizo la fedha, tunalipia ada watoto wasio na uwezo huko Tanzania kila mwaka, watu wanaofulia kulipa kodi za nyumba wanatufuata kila mwaka tunawalipia.

Na mara nyingine tunakaa miaka mingi nje bila kurudi Tanzania kwa kufuata kazi zetu tu, kw akuamua.

Sasa kwa hesabu zako za kukariri, utaona watu wanaoamua kuzikwa nje hawana fedha.


Last time I came to Tanzania I spent about $20,000, kwenye likizo ya wiki tatu.

Na nimeamua nikifa nisizikwe Tanzania.

Sasa hapo utasema nimeamua nisizikwe Tanzania kwa sababu ya gharama za kusafirisha mwili?
Hapa naona umeamua kujizungumzia wewe kibinafsi zaidi, hasa your finacial status zaidi ya kuwazungumzia na wengine pia, au huko America hali zenu wote zinafanana?



Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Naona hautaki kulundikwa kwenye desturi zetu, mindset ya kimarekani imekuingia unaanza kuzikataa mila na desturi zako, hata kama huzitaki, wazazi wako wanazifuata, hiyo ndio sababu iliyonifanya nikachagua kutumia neno "zetu" nikimaanisha waswahili, sio wakina wewe "swahili-zungu".

Hapa pia kuna angle ya pili niiite social status.

Mzee Mwinyi alikuwa mtu mzito hapa Tanzania -Rais Mstaafu, hivyo kwangu sioni ubaya yeye kujadiliwa, hata nawe huwa unakuwa kwenye upande wa kuunga mkono mtu mwenye nafasi kwenye jamii kuzungumziwa, nikikumbuka umekuwa ukilaumu taarifa za viongozi wagonjwa kwenda nje kutibiwa kufanywa siri na serikali.

Sasa sijui kwanini hapa kwa marehemu Mzee Mwinyi umeamua kugeuka kuwa mtu wa kutaka "ushahidi wa vikao vya kifamilia", kwanini wakati ule wa ugonjwa wa viongozi huwa huulizii ushahidi wa ugonjwa wa kiongozi toka kwa familia yake kwanza, badala yake huishia tu kuitaka serikali isitufiche habari zao?



Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Kuhusudu sana mila na desturi ni ujinga.

Mwinyi angehusudu sana mila na desturi, angebaki kijijini kwao, asingeenda hata Zanzibar, na tusingempata huyu Ali Hassan Mwinyi wa leo.

Wapo wenzake wengi sana walioheshimu mila na desturi hata shule za elimu dunia wamekataa kwenda. Wameishia kufulia.

Wakati wakoloni wanaanzisha mifumo ya elimu, walipita kuchukua watoto wa machifu wakasome. Chifu Mazengo wa Ugogo alikataa watoto wake kuchukuliwa wakasome. Jirani yake Chief Mazengo alikuwa baba yao kina John Malecela na Job Lusinde, yeye alikuwa na muamko kidogo wa kutaka elimu, akakubali watoto wake kina John Malecela na Job Lusinde waende kusoma.

Matokeo yake, mtu aliyeheshimu mila na desturi Chief Mazengo, kawakosesha fursa ya kuwa viongozi watoto wake, kwa sababu hawakupata elimu, mtu ambaye alisema hizi mila na desturi zipo lakini inabidi tujiongeze, Mzee Malecela, watoto wake kina John Malecela na Job Lusinde wameenda kuongoza nchi.

So kuangalia mila na desturi bila ku focus kwenye kuangalia mbele na ku shape mila na desturi mpya zinazofaa zaidi kwa dunia ya kesho ni ulofa, ni ujinga tu kama alioufanya Chief Mazengo wa kukataa shule.

Kuhusu kujadiliwa.

Kwani wapi nimekataa Mzee Mwinyi kijadiliwa?

Unajua kuna tofauti kati ya kukataa Mwinyi kujadiliwa na kukataa Mwinyi kujadiliwa kwa hadithi za uzushi zisizo na chembe ya ushahidi?
 
Hapa sio suala la maneno mengi yasiyo na msingi, ni suala la desturi zetu na kuzifuata. Kawaida desturi zetu inaonesha zinaenda kinyume na kile familia walichoamua.

Jiulize; vipi kama Dr. Mwinyi asingekuwa Rais wa Zanzibar leo, baba yake still angezikwa huko Zanzibar peke yake awaache ndugu zake wengine wazikwe Mkuranga? Jibu ni hapana.

Politics imeamua destiny ya Mzee Mwinyi kwa manufaa ya kisiasa ya mwanae.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Naungana na wewe ktk hili.
 
Back
Top Bottom