Subaru mnatufilisi, Gari zinakunywa mafuta kama zinameza!

Subaru mnatufilisi, Gari zinakunywa mafuta kama zinameza!

Mkuu, heshima mbele kwa gari yoyote ya mjerumani.
Gari za mjapani kwa kawaida gearbox iko syncronised kwa speed ya hadi 180km/hr kulingana na sheria zao.
Lakini mjerumani kwenye outobahn zao gari zao ziko sync hadi 240-280km/hr!!!
Hata hivyo hal hla , ni sehemu chache sana nchini za "kupaa" hata kwa hiyo 180km/hr!!!

Ni kweli mkuu natumia VW Polo nimeshawahi tembea 180Km/hr tokea Nyororo hadi Mafinga pale barabara ni nzuri ila sitakaa nirudie cause ni sawa na kuvaa bomu tu muda wowote linakulipukia
 
kaka kuna gari za watumiaji wa kipato kidogo na kipato kikubwa,ni kama kama huna biashara za safari ndefu za mara kwa mara unanunua prado v8 huku maisha yenyewe ni ya kuungaunga,utailaumu gari kumbe kosa ni lako kutokufanya uchunguzi mapema.Gari yako hiyo hiyo ipige long safari uone kama hujaifurahia kama wewe ni dereva lkn.
.
Duh Majangaa
 
Hahahaha....umenikumbusha mbali aisee...mimi nakumbuka nilinunua BMW kwenye mnada ilikua imekufa engine ila body ikawa iko powa, nililnunua kwa milioni mbili na nusu...nikaenda kariakoo nikanunua engine ya mark II laki sita unusu nikawa nimemaliza kazi...barabarani watu wananitolea mcho kumbe gari hata milioni 4 haijafika.... mjini bwana.

mkuu hivi hili swala linawezekana eeh?
 
Mkuu hiyo gari ina high perfomance engine 2000cc.
Watu wengi wana iconfuse na kufikiri ni sawa na Corolla!

Hii gari ni kiboko, ina perfomance bora kuliko Chaser au gari inayolingana na Chaser.

Ukitaka kuijua Subaru piga long trip kama Mbeya au Arusha ndo uyaiheshimu.
Its a leader in its class.

kama ni 2000cc bado ulaji ni wakawaida tu haina tofauti na Rv4
 
Vijana wengi wa Arusha wamenunua Subaru wakifurahia ule mlio wake lakini wamesahau ufahali nyumba ya umaskini hasa kama hela yenyewe ya kujichanga changa!

Subaru haifai kwa kiwese.

Km 350? litre 65 = Approx ya 1litre = km 5, Hiyo ni VX V8
 
Mimi nimetumia Subaru naenda mwaka wa tatu sasa.Katika magari mengi ambayo nimeshaendesha Subaru nalikubali hasa uwezo wa Engine yake na huwa aliharibiki mara kwa mara kama magari mengine ambayo nimewahi kuwa nayo.Spea ni gali ila once ukiweka inakaa mpaka unasahau kwani haichakachuliwi kama magari ya Toyota.Subaru kwa kijapani ni STAR.Mafuta inaenda one litre kwa mpaka 10 to 13 km na ni FWD.

Hiyo ni subaru ya aina gani mkuu?
 
Mm yangu baada ya kuona hivyo sikuongea na mtu...nikauza...nikarud kwenye vits sitak kufaidisha wafanya biashara ya mafuta
 
mimi nina Impreza WRX STI, kwa kweli ina undugu na petrol stations. lakini ni gari ya uhakikaaa ukiendesha una feel kweli unaendesha gari kitu manual 6 speed. top speed 260 :dance::dance::dance::dance::dance::dance::dance::dance::dance:
 
Nineweka full tank lita 65 ajabu nimetembea km 350 mafuta kwishney leo nimejaza tena

Brother ya kwako ni ipi mimi kwanza fultanj yake ni 50 ltrs, nimijaza full tank kwa mwendo wa kawaida natumia 1 ltr kwa 12 km na nikiendesha 160-180+ inaenda km9-8 ful burudani..
 
Abadili gari achukue BMW ulaji wake wa mafuta ni nzuri sana hasa ukipata diesel version

Brother ni kweli gari za diesel ni very economy hata hapa UK gari ndogo nyingi ni diesel, sasa kwa tanzania gari ya diesel mafundi wakiiona wanaogopa mimi binafsi nazipenda Ila ishu ni hiyo ya service spares na mafundi..
 
Brother ni kweli gari za diesel ni very economy hata hapa UK gari ndogo nyingi ni diesel, sasa kwa tanzania gari ya diesel mafundi wakiiona wanaogopa mimi binafsi nazipenda Ila ishu ni hiyo ya service spares na mafundi..
LACHERO ni woga wetu tuu siku hizi tuna mafundi japo si wengi mimi nina BMW mini niliweka liter 20 nikaenda chalinze na kufanya mizunguko ya yangu na kurudi Dar bila taa ya mafuta kuwaka ....imagine 20 litres km zaidi ya 230 I LOVE BMW
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom