Jana asubuhi nilimtuma mtoto na shillingi 8,400 kununua sukari kilo tatu nikifahamu mteja wangu huwa ananiuzia sukari Tshs. 2,800 kwa kilo.
Mtoto alirudi mikono mitupu akanieleza kuwa sukari imepanda bei na sasa kilo moja ni Tsh. 3,500. Nilishtuka sana na mpaka sasa sijaamini.
Nina maswali yafuatayo kwa Serikali:
1. Ongezeko hili limesababishwa na nini?
2. Je, kama Serikali mlitoa taarifa kwa wananchi kuhusu ongezeko hili?
3. Je, mnajua wananchi wengi hawataimudu bei hii?
4. Je, Serikali haijui kuwa Wananchi tunakosa imani na Serikali yetu?
Ninaomba majibu ya maswali yangu.