Supu ya pweza inanimalizia hela nashindwa kuiacha

Supu ya pweza inanimalizia hela nashindwa kuiacha

Za jioni wakuu, supu ya pweza ni maarufu sana Dar es salaam mida ya jioni ambapo tunaona watu wanauza supu kwenye vimeza vyao.

Sasa kitu kinachofanya nije leo ni ulevi wa supu ya pweza aisee nimejitahidi kuacha nimeshindwa yaani kila nikitoka kazini njia ya kwenda nyumbani kuna kibanda cha pweza kama wana dawa vile hawa watu unasema ninywe supu ya mia tatu ,mara unapiga kachori, paap kata mkia wa elfu mbili, weka na prawn puuh elfu tano imeenda.

Nikaamua nipige hesabu kila nikila pweza niandike kwenye google notes aiseee nimekuja kupiga hesabu mwezi december 2023 nimetumia elfu 65600 ukichezesha mwaka mzima kama laki 7 hv jamani si Tv mpya hiii.
Nifanyeje niache huu ulevi wa supu ya mdudu pweza.

Tushee experience walevi wenzangu
Ungekuwa unakunywa pombe ungesemaje?
 
Hizo lumbulumbu ni ugonjwa kwa kweli, kimasihara tu unajikuta elfu 5 imekatika,
Mie siachi, sina fikra hizo.
 
Pweza wanauzwa kwa kilo. Huyo pweza wa 10K unampata wapi mwenzetu?
Najua pweza wanauzwa kwa kilo, ni mpaka afike ndani sokoni au eneo la mnada ndio anapimwa. Ukimfata nahodha au baharia kwenye chombo anakuuzia kulingana na ukubwa
 
Za jioni wakuu, supu ya pweza ni maarufu sana Dar es salaam mida ya jioni ambapo tunaona watu wanauza supu kwenye vimeza vyao.

Sasa kitu kinachofanya nije leo ni ulevi wa supu ya pweza aisee nimejitahidi kuacha nimeshindwa yaani kila nikitoka kazini njia ya kwenda nyumbani kuna kibanda cha pweza kama wana dawa vile hawa watu unasema ninywe supu ya mia tatu ,mara unapiga kachori, paap kata mkia wa elfu mbili, weka na prawn puuh elfu tano imeenda.

Nikaamua nipige hesabu kila nikila pweza niandike kwenye google notes aiseee nimekuja kupiga hesabu mwezi december 2023 nimetumia elfu 65600 ukichezesha mwaka mzima kama laki 7 hv jamani si Tv mpya hiii.
Nifanyeje niache huu ulevi wa supu ya mdudu pweza.

Tushee experience walevi wenzangu
Maisha hayapimwi kwa bajeti dhaifu za namna hiyo!

Unatupa au unakula mwenyewe?

Ungelikuwa unatupa ama kuhonga tungelikushauri vinginevyo.

Lakini mtu unakula kwa afya, halafu tena unaanza kujushitukia!

Unaweza kuchepusha matumizi ya supu, 'seva' ikajaa lakini ukaishia kuhonga,Tv usinunue na wala hapa usitokeze kutuomba ushauri, ikawa ni siri yako.

Wewe bwana kula, Tv ina bajeti yake na mwili una bajeti yake.
 
Back
Top Bottom