Swali gumu kidogo: Kwanini Urusi iliyosambaratika na dhaifu kuliko USSR inawasumbua sana NATO?

Mkuu asante sana kwa hiyi reply yako na huwa napenda sana kujadiliana na watu ambao kichwani wapo sawa,na wewe upo sawa haswa.Ukwe;i ni kwamba nchi za magharibi zinachagua nani wa kumuwekea vikwazo na nani wa kumuachia huru kulingana na matakwa yao wenyewe.Kwa mfano China hakuna demokrasia na ukiinua kichwa wanakutwanga(Tianmanen square masacre 1989,sijui wewe ulikuwa wapi). Na hawakuwekewa vikwazo ambavyo ni nail biting. Western countries ndo sababu kubwa sana ya china kuendelea. Ingawa China ipo number 2 lakini living standard average chinese ipo way below Japanese. Kwa kiasi fulani nakubaliana na wewe kuwa demokrasia(kama inavyokuwa defined na western countries) sio kichocheo cha maendeleo.Kuna mifano mingi ya nchi ambazo hazina demokrasia( As defined by western countries) lakini zimeendelea,kwa mfano China,Saudi Arabia,Qatar etc etc.Lakini ukichukua data na kuangalia nchi tajiri na wananchi wana maisha mazuri zaidi unaona nchi gani zinakuwa nyingi ? Zenye Democrasia au zisizo na Demokrasia ?Nawasilisha
 

Careful, kuhusu kuiona China imepiga hatua kubwa. Jua kuna idadi kubwa ya Wachina wanaishi kwa dhiki sana nchini mwao. Inategemeana unavyopima maendeleo. Matajiri wakubwa China wanasomesha watoto wao Marekani na Ulaya; wamewekeza utajiri mkubwa huko na wanamiliki makazi huko. Wana akaunti nzito za dollars, Euro, Pounds, n.k.

Tukija kwenye suala la India, ni open society kweli lakini isiyo na mifumo imara ya utawala. Hivyo, rushwa lazima iwe kubwa na "ionekane". Marekani na ulaya ni open lakini wana mifumo advanced ya kudhibiti graft. China ni "closed" na kama kawaida ya jamii "closed" rushwa yao ni ya kimfumo na inadhibitiwa kati ya wateule tu. Hao wanajichotea mabilioni na hayasikiki nje ya wigo wao. Ukisikia China watu wanahukumiwa kwa rushwa ni wale walio nje ya wigo wa ruling class na walioanguka toka kwenye ufalme (fall from grace) - kwa sababu za kisiasa zaidi. Tena kesi zao zina maajabu. Utakuta mtu aliyekuwa mzito anasimamishwa mahakamani anakiri "kuhujumu uchumi" na kuomba radhi kisha anapigwa risasi. I have no iota of admiration for such a state!

Hakuna namna tunaweza kupata na kujivunia maendeleo ya kweli nje ya mfumo wa demokrasia. Na hakuna kitu kinachoniudhi kama unafiki mkubwa wa wale wanaopendelewa na mifumo ya kidikteta kudai kwamba eti demokrasia haitufai kama tunataka maendeleo. Eti ni urithi mbaya toka kwa wakoloni! Tunaishi mara moja tu hapa duniani. Ili maendeleo yetu yawe na maana katika maisha yetu, tujitahidi kufikia hatua kama zilizofikiwa na Marekani na Ulaya (unaweza kuongeza japan, S. Korea, n.k). Japan walikuwa na maendeleo makubwa chini ya mfalme lakini walipaa zaidi kitaifa na kibinafsi baada ya kuachana na udikteta wa kifalme na kujiunga na ulimwengu wa demokrasia.
 
Bw. Lumumba, samahani, sijui namna ya kutumia "multiquotes" na muda wangu JF ni limited sana.
 
NATO kwa pamoja wana idadi ya watu milioni 603.73.
URUSI peka yake ana idadi ya watu milioni 144.3.
NB: NATO ina watu mara sita zaidi ya Urusi lakini kwanini iwasumbue ??
MALCOM LUMUMBA

NAONA NDUGU UNAYATUMIA VIBAYA MAJINA YA WANAZUONI WAKUBWA DUNIA HII

TAYARI HAPO AWALI UMESHATAJA NGUVU ALIZONAZO MRUSI,HALAFU BADO UNAJIULIZA KWA NN ANAMSUMBUA MMAREKANI

JE HUONI KUWA HIZO NGUVU MRUSI ALIZONAZO KUWA NDIZO ANAZOZITUMIA KUMCHACHAFYA MUAMERIKA?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzeee huyo sio dhaifu bado wapo vizur sana kijeshi na technology japo ni kweli uchumi waliyumba lakin bado wanamiliki eneo kubwa zaid kwenye nchi yao ile ya awali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe umetumwa nn?
Nikisikia Russia uwa nachukia Sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naondoa hoja baada ya kuufatilia uzi

Nilichogundua hapo awali bwana Malcom ulikuwa unachokoza mada huku ukweli ukiufahamu

KWELI LEO KATIKA SIKU AMBAZO GREAT THINKERS IMETENDEWA HAKI BASI LEO NI SIKU YENYEWE

KEEP UP GUYS

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kila nchi ni mfungwa wa jiograph..NATO kwa wingi wao wanategema udhaifu wa masoko hafidhina kiitikadi..uimara wa soko hafidhina ni msiba kwa NATO..ili uwe imara sokoni lazima uwe na maliasili hasa gas,mafuta na chuma pia mlango bahari wa maji moto bila kusahau rasilimali watu[IQ kubwa]..jeuri ya russia ni maliasili,innovation na ufundi[IQ].....globalization iliasisiwa NATO waki assume hakuna ng'ombe kama China ataja ibuka...China na NATO wanakiu ya maliasili ambayo Russia anayo tele ila mbabe....kumwangusha China lazima uanze na russia ....kiitikadi ni walewale..kimsingi USSR haikufa ila imevaa ngozi ya kondoo..inasubiri mlango bahari wa arctic uwe moto ndiyo kitu pekee hawana....tukumbuke tu kwamba wapo syria kuweka bendera ya kiu ya energy duniani.
 
daaaahh ahasanteni wakuu" nimeelimika vyakutosha ".
 
Hoja nzuri sana hii,Mkuu ML
kwanza kabisa Urusi sio taifa dhaifu kabisa na wala halikuwahi kuwa dhaifu maishani,bali hizo ni propaganda za Mahasimu wake,bali Urusi iliwahi kupata ajali na kuugua,(ajali ni kuvunjika kwa umoja wa kisoviet,na kuugua ni madahra ya kupata ajali )yaani majeraha ya kuvunjiika Usovieti.
Ukuu wa Urusi ni uwezo wake wa kurudi haraka kutoka kwenye kuuguza majeraha(,kuvunjiaka usoviet).
Ni kweli haja ya Marekani ni kuitawala dunia bila upinzani wowote.
Sio tu furaha ya Marekani ilikua ni kuvunjika kwa Usoviet,bali kumaliza kabisa ushawishi, na allies wa Urusi,ndipo juhudi za kizigawa nchi zilizokua Warsaw pact ,na nchi za kisovieti zilipopamba moto.mfano mshirika mkubwa na ndugu wa damu wa Urusi nchi ya Yugoslavia ilipofanyiwa hujuma nzito na kubaki vipande vipande.
Urusi haikushindwa vita baridi kwa juhudi za west peke yake,bali kwa msaada wa taasisi nyingine kubwa duniani hasa kanisa KATOLIKI chini ya Baba Mt (PAPA) John Paul II,na hata Uislam.Hii haikua vita ndogo ya kuliangusha dubwana kuwa USSR.
UWEZO WA URUSI.
Elimu,maarifa,sayansi,teknolojia,mikakati na ulinzi na ufedhuri.
Marekani peke yake hamwezi Mrusi,hawezi kumdhibiti kwa sababu Urusi anavyo vitu vyote ambavyo marekani anavyo lakini wengine hawana navyo nimevitaja hapo juu,Urusi wana elimu,hapa ndio chimbuko la kila kitu duniani,ana maarifa kama vile marekani,ana sayansi na teknolojia kama vile marekani,ana mikakati thabiti ya kubaki kwenye game kama vile marekani ana uwezo wa ulinzi na usalama kama vile marekani,ili kumdhibiti labda uue wananchi wake wote ibaki ardhi tu.Ufedguri namaanisha ujasusi.
Ni kweli ML kuwa Urusi itawasumbua sana Marekani na washirika wake kwa sababu kiuchumi Urusi ana kila kitu ardhini hivyo hahitaji kununua kwa wengine, ambapo wangemfungia asinunue au asiuziwe.lakini kwa alivyonavyo watawazui wengine wasinunue kwake,hilo wanawewza.
kijeshi kumdhibiti Urusi ni kukusudia kuiangamiza dunia,kama sio kujaribu kujipiga risasi mwenyewe.vita ya Urusi na wao haitakua vita ya Kalashinikov na bunduki nyingine bali ita kua ni vita ya ICBM's
sasa fikiria marekani akirusha na urusi akirusha kuna kitu kitabaki?
 
NATO kwa pamoja wana idadi ya watu milioni 603.73.
URUSI peka yake ana idadi ya watu milioni 144.3.
NB: NATO ina watu mara sita zaidi ya Urusi lakini kwanini iwasumbue ??
USA,ndio nchi inayopokea misaada ya kijeshi kiulinzi na kijasusi Duniani kuliko nchi yeyote ili kuikabili Russiah Federation (RF)
.Baada ya vita kuu ya pili ya dunia,kukatokea vita nyingine mbili lakini sio za moto
1.vita baridi
2.mashindano ya kutengeneza silaha kali duniani.
Vita baridi USSR ilishindwa na USA
Vita ya kutengeneza silaha bado inaendelea, kama vile ilivyokua mwanzo kati ya USSR na USA.lakini USA bado anaendelea kusaidiwa na washirika wake ,wakati RF( Urusi) akiwa peke yake.
Hata baada ya kuvunjika umoja wa Kisovieti,bado USA anasaidiwa kutengeneza silaha na masuala ya Intelijensia ili kikabili Russian Federation( RF) yaani Urusi ya Vladimir Putin.
ONA.
Baada ya WWII, kukaibuka vita baridi kati ya USSR akieneza ukomunist na USA ikieneza ukapitalist.
USSR akaunda Warswa Pact kujihami,USA akaunda NATO kujihami.
USSR ikavunjika na Warsawa Pact ikavunjika ikabaki Russian Federation ( RF)peke yake,Wakati USA ikabaki na NATO ikabaki,lakini Bado hawajaweza kumcontain RF,Urusi.
Baadhi ya nchi zilizokua USSR,zikajiunga na NATO,bado Russia iko peke yake,lkn hawajamweka mkononi RF.
Baadhi ya nchi zilizokua Warswa Pact zikajiunga na NATO,bado Russia iko peke yake lakini hawajaweza kumdhibiti,RF.
Kwa kupitia NATO,USA anapata misaada mikubwa sana ya kiteknolojia,kijeshi na kiintelijensia ili kuikabili Urusi. Nchi kama UK,France,German,etc zimeisaidia sana USA kijeshi kudili na Russia.
MISAADA YA KIJESHI KWA MAREKANI NJE YA NATO
Israel,huisaidia sana USA kijasusi na tech dhidi ya Urusi,
Pakistan iliwahi kuisaidia USA kudili na USSR huko Afghanistan,
Ugiriki,hawa walinunua S300 toka Russia,wakawaalika Waisrael,wakaenda kuichunguza na kuifanyia mazoezi jinsi ya kuishinda,
Uingereza kama nchi pekee nje ya NATO ina bifu la asili na Urusi hapa mashirika ya kijasusi kama MI6,MI5 na CIA huishughulikia kwa pamoja Urusi,anaefaidika sana ni USA,
USA wameshiriki mara nyingi kuiba silaha za URUSI na kwenda kuzisoma na kisha kujua siri zilizowanufaisaha .Rubani mmoja wa jeshi la Iraki aliwahi kuiba MIG ya kirusi kwa faida ya Israel na aliyefaidika ni USA.
Hiyo mifano michache,na mara zote Urusi huwa haiteteleki wala kulalamika.
Ukraine,Georgia,Poland,Chek ni mfano wan chi zinazoinufaisha USA.
Hivyo mbinu zote za kijeshi,kijasusi na baadhi ya vifaa vilivyokua vya baadhi ya wanachama wa Warsaw Pact na nchi zilizokua za Kisoviet zilizohamia upande wa NATO na USA, ZIMEIFAIDISHA sana USA lakini bado wameshindwa kuimudu Russia Peke yake na kuitiisha.
VIKWAZO VYA KIUCHUMI.
Kwa kuwatumia EU na yeye mwenyewe USA,dhidi ya Russia ,bado wameshindwa kumtiisha na kumpinda.RUSSIA limebaki kuwa ni taifa imara.
Saud Arabia
Hawa hutumika kushusha mafuta ili bei ya mafuta ishuke ili kudhoofisha uchumi wa Russia,hii nayo ilifeli.
Haya ni machache tunayoyajua ,ni mangapi tusiyoyajua ,Je mpaka hapa USA haisaidiwi kuliangusha Dubu LILILOKATAA KUFA?
Haya ni maoni yangu tu,na hii ni makala ya kujifurahisha tu ili kuchangamsha ubongo,je si kweli kuwa USA inapewaga MISAADA kidili na URUSI?
Mjadala uko wazi.
 
Ahsante sana mkuu,
Sasa kama Urusi alikuwa na nguvu nyingi zaidi ya hizi za leo kwanini alishindwa Vita Baridi ??
Katika mantiki hii unataka kuniambia kwamba Urusi ya zamani ilikuwa na nguvu kuliko Marekani ??
UNAJUA MAANA YA VITA BARIDI???
 
Kumbe majibu unayo alafu unauliza maswali jamani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante sana mkuu,
Sasa kama Urusi alikuwa na nguvu nyingi zaidi ya hizi za leo kwanini alishindwa Vita Baridi ??
Katika mantiki hii unataka kuniambia kwamba Urusi ya zamani ilikuwa na nguvu kuliko Marekani ??
Eneo ambalo urusi litamsumbua sana kuweza kumfikia Marekani ni Propaganda, Intelligency na Millitari/War strategies.
Maeneo yote hayo matatu ndiyo yanampa nguvu sana Marekani na yamekua nguzo sababu ya financial Power aliyonayo.
Russia inabidi afanye ku customise hayo maeneo ili yaweze kumsaidia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…