Swali kwa Ayubu Rioba: Siku hizi sera ya Taifa inaruhusu taasisi za kidini kunufaika na fedha za walipa kodi kupitia TBC?

Diamond, Ali Kiba, Harmonize, Zuchu ni waislamu. Roma, Stamina, Professor Jay n.k ni Wakristo
 
Wewe ndio huelewei kanuni na taratibu za kuendesha taifa lisilo la kidini "secular state"
Mama Amon ameshindwa kuelewa katiba sijuwi labda anamatatizo ya lugha.

Kuendesha shughuli za dini ni tafauti na kuonesha au kureport
 
Analeta siasa za udini kwa kivuli cha katiba.
Vipindi vya miziki ya watu wananengua vikiwekwa pale TBC , wakristo na waislamu hawaoni kama Kodi zao zinatumika vibaya, kwani nao huvifurahia. Anayehama chanel kusubiri kipindi anachopenda sio kwa sababu kipindi hicho hakikubaliki kimaadili, bali ni tofauzi za hobby tu. Lakini ni jambo tofauti kama TBC wakiwema mkanda wa XXX. Huo ndio Utanzania. Ndio maana naamini wewe umetumwa kuvuruga mjadala. Mbele ya Mama Amon hautoboi.
 
Kuna tofauti ya kuweka habari inayohusu dini fulani na kuigeuza TV au redio kuwa jukwaa la mahubiri ya dini fulani.
Wanapoweka habari za waislam huwa wanaweka habari za wahindu na za wakatoliki.
 
Waache waislam wasikilize vipindi vyao nao ni walipa kodi kama wewe.

Jamii pana yenye makabila 120 haiwezi kuwa na hulka, Mila, dini na tabia zenye kufanana ni lazima tuvumiliane.
 
Kuna tofauti ya kuweka habari inayohusu dini fulani na kuigeuza TV au redio kuwa jukwaa la mahubiri ya dini fulani.
Hakuna kosa lolote, kama Haya kuhusu badili tu Chanel maana na hao wenye kujadiliana masuala ya dini yao unapofika muda wa dini yako kuwa na vipindi vya dini, wao pia hubadili Chanel.

Kuwa mpole tu.
 
Usiwe kama ngumbaru kuhamishia mjadala kwenye imani fulani ili ionekane uzi ni kwa ajili ya kupinga dini fulani. Suala ni vyombo vya habari vya taifa visiwe jukwaa la mahubiri kwa dini YOYOTE.
Waache waislam wasikilize vipindi vyao nao ni walipa kodi kama wewe.

Jamii pana yenye makabila 120 haiwezi kuwa na hulka, Mila, dini na tabia zenye kufanana ni lazima tuvumiliane.
 
Aliye kuambia mlokole anataka rhumba nani? Au mwislamu anataka rege nani kakuambia.Wacha watanzania tuishi kama tulivyo.Sisi tuna furahia vipindi vya TBC .
 
Soma bandiko vizuri.

Udadisi kuhusu utendaji wa TBC kupitia akaunti ya Mama Amon ulianza 15 Novemba 2020, wakati nchi hii inaongozwa na Rais Mkristo.

Wakati hio Makerubi alikuwa analijingisha Taifa kuwa Roho Mtakatifu amejenga ukuta kuzunguka Tanzania na hivyo kuikinga ndhidi ya korona.

Pia juzi niliwakumbusha watumishi wa umma, sekta ya maji, kutenganisha dini na kazi za serikali.

Asante kwa kuelewa.
 
Aliye kuambia mlokole anataka rhumba nani? Au mwislamu anataka rege nani kakuambia.Wacha watanzania tuishi kama tulivyo.Sisi tuna furahia vipindi vya TBC .
Hujasikia nyimbo za Injili zenye melody ya Ndombolo ya Solo?
Tafiti tena.
 
Unaongelea SECULER STATES gani ?

Nimetowa mfano wa secular countires kama BBC, FRANCH 24 , RT zote hizo ni mali ya nchi za secula. nabado wanareport vipindi vya Dini.

Mashindano ya quraan ambayo Wazir mkuu na Rais wanahudhuria itakuwa ni ujinga kukata ku report kwa madai ya Dini

Hembu acheni ujinga tuangalie mambo muhimu
 
Sijwahi kusikia waislamu au Wakristo wakilalamika nyimbo za bongo fleva kupigwa TBC. Waislamu na Wakristo wote wanzipenda sana na huzitumia hata katika harusi zao, maulid, kipaimara, arobaini n.k
Kwahiyo wanaimba mahubiri ya kiislamu na kikristo?
 
Kuna tofauti ya kuripoti matukio yanayohusisha dini na kuweka vipindi vya mahubiri, mawaidha, kwaya au kaswida.
 
Nikuelewe nini mbaguzi mshenzi tu kama wewe.
Hakuna haja ya kunielewa.
Na hata ukijaribu kunielewa, au kumwelewa mtu baki, hutafanikiwa.
Unaweza kuelewa kauli/hoja ya mtu, basi
So, unachopaswa kuelewa ni hoja yangu.
Basi.
 
Taarifa ya habari inayohusu tukio la kidini ni suala tofauti na tukio la kidini kuwe sehemu ya programu ya kituo cha luninga. Huko BBC, FRANCH 24 , na RT hawana kipindi cha kiongozi wa dini kuketi hapo na kuanza kuhubiri watu wasiojulikana ni kina nani na wako wapi. Hasa huu ndio ujinga unaopingwa hapa.
 
1. Nilichokisema mimi ni kwamba dini/imani ni sehemu ya utamaduni wa watu/walipakodi.
2. Kama kipindi kinachorushwa kinahusu dini/imani (sehemu ya utamaduni wa watu), kama kinavyoweza kuhusu uchumi, siasa na jamii, kwa kuzingatia taaluma ya uhandishi wa habari kwa namna ambayo haivunji maadili au sheria za nchi,
3. Na kwa vile baadhi ya walipakodi ni waumini pia katika hiyo dini/imani,
4(i) Basi, hakiwezi kukiuka utaratibu wa kawaida wa kurusha vipindi vya TV au radio na
(ii) hivyo (kwa maoni yangu) hakuna utata wowote katika hili.
5. Labada wewe mwenyewe uonyeshe urushaji wa hivyo vipindi vinavyosemwa ulikuwa na utata gani au ulikiuka utaratibu gani wa urushaji wa vipindi.
6. Kama urushaji wa hivyo vipindi una tatizo, basi tujadili hilo tatizo kuliko kujadili jambo la jumla hivyo.
 
1. Usiwachukie Wakristo, wasaidie waondokane na huo unafiki unaouona kwa Wakristo.
2. Ila siamini kuwa wanafiki ni Wakristo tu, bali kwamba mnafiki anaweza kuwa muumini wa dini yoyote.
3. Sidhani kama wanaonuna kwa sasa ni Wakristo (ingawa inawezekana kwa baadhi ya wanaonuna kuwa Wakristo) na ndio 'wanaolazimisha tusiyaone mema anayotutendea mama'.
4. Siku nyingine ukichangia hoja jaribu kupima hoja yako na uwasilishaji wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…