Swali kwa wapinzani: Je, Samia agombee 2025 au ampe kijiti chuma kingine kama Magufuli?

Swali kwa wapinzani: Je, Samia agombee 2025 au ampe kijiti chuma kingine kama Magufuli?

Kwani kila mpinzani ni mwanachama wa CDM, au hujui upinzani ni nini boss?
Huyo ni pimbi hajui kuwa asilimia kubwa ya wanaompinga mma Abdul ni maccm na hata yeye mwenyewe aliwahi kusema kuwa wapinzani wake ni wenye kuvaa mashati ya kijani.
 
Upinzani sasa hivi wanasema Samia ameshindwa uongozi na ni kiongozi mbaya kuwahi kutokea.

Yaani ni mbaya kuliko hata Magufuli waliyekuwa wanadai ni kiongozi mbaya zaidi.

Tundu Lissu mara kadhaa amesikika akimsifu Magufuli kwa uzalendo wake na kusema ataenda Chato kumwambia jinsi CCM na serikali aliyoiacha walivyomsaliti na kuharibu nchi.

So Samia akiwasikiliza na kuamua kumpisha mzalendo na chuma kingine chenye msimamo kama Magufuli wapinzani si mtafurahi ili hata CCM ikishinda nchi iwe salama zaidi?

Au mtaogopa na kukimbia tena?

View attachment 2739496
Samia mpaka 2030 kisha January. Hatutaki TEC wachukue nchi tena.
 
Pamoja na utopolo wa ccm ila wapinzani wana tatizo la kutokuwa na sera inayowatambulisha.

Ni kama wanasubiri ccm ndo iwape sera ya kuipigania kupitia aina ya kiongozi na mfumo wa siasa wa ccm uliopo kwa wakati huo.

Lowasa hafai-Lowasa anafaa
JK dhaifu tunataka raisi asiyecheka na mali za uma-JPM dikteta uchwara
Samia mgeni rasmi maridhiano nchi sasa imekombolewa kutoka kifungoni - Nitaenda kwenye kaburi la JPM kulia sijui kufanyaje.
Hii ni hoja yakitoto umeandika.nchi ni zaidi ya hichi ilichokiandika.Tofautisha sera na mazungumzo yakisiasa ya wanasiasa.
 
Na katiba mpya isipopatikana kabla ya 2025 agombee au atuletee JPM mwingine?
Anatakiwa kiongozi mwenue sifa zakuongoza wananchi sio kiongozi mwenye sifa za rais mwingine.Kuchagua rais kwasababu anafanana na rais fulani huo ni ujinga.Nchi inatakiwa itoke kwenye ujinga wakutegemea kiongozi mmoja kwenye kila kitu.
 
Hafai, yaani Rais pekee ambae hajambanishwa huko CCM, tangia mfumo wa vyama vingi.
 
Hii ni hoja yakitoto umeandika.nchi ni zaidi ya hichi ilichokiandika.Tofautisha sera na mazungumzo yakisiasa ya wanasiasa.
Ww sema ni hoja ya kitoto ukidhani kuna wananchi wanafuatilia sera za chama chako kupitia nyaraka zenu hapo ofisini. Watanganyika wapiga kura wanasikiliza wanachosema wanasiasa.
 
ishu ni katiba wala sio rais. weka katiba ya warioba na tume huru kisha acha rais samia aendelee tena na wabunge/ mawaziri wake afu tuone.
 
Mbona mama yuko fresh hiv mnataka malaika ndio awaongeze au.yule mlisema dictator huyu kaja kaeka mambo yote mliokua mnalalamika bdo mnaleta chuki
 
Ishu sio kusifiwa, wanasema Magufuli ana afadhali ya Samia, je Samia ampe Magufuli mwingine kijiti 2025?
hata wengine wanasema Samia ni bora kuliko Magufuli, inategemea umeelemea kundi gani, na wala hakutakuwa na Magufuli mwingine mpaka mwisho wa dunia. Atakuja dikteta mwingine mwenye masharti ambayo wapambe wake watayashangiria na wengine watabaki kulalamika.
 
Labda Makonda na ndo wapinzani wanamuogopa maana jamaa anajiamini na kutumia madaraka vyema.
 
Kitendo cha Samia kuwapa Polisi mabilioni ili kununua vifaa vikimemo maji ya pilipili ni kwamba anajiandaa kupora uchaguzi.

Hajui kuwa tumeshakuwa sugu😁 mimi nimejiandaa na virungu na mabomu ya machozi ila safari hii tunajizatiti.
Polisi nao watakuwa waajabu kwani watakuwa migambo wa mapolisi wa Dubai
Kwani Waarabu wakisha tawala wao watakuwa mawakala tu
 
Rais ajaye ni Wakili Msomi Mwabukusi chuma toka Busokelo. Ni suala la muda tu.
 
hata wengine wanasema Samia ni bora kuliko Magufuli, inategemea umeelemea kundi gani, na wala hakutakuwa na Magufuli mwingine mpaka mwisho wa dunia. Atakuja dikteta mwingine mwenye masharti ambayo wapambe wake watayashangiria na wengine watabaki kulalamika.
Nazungumzia Chadema, nafahamu kuna watu waliokuwa wakimsifu Magufuli kabla hajafa na wanamuona ni bora kuliko Samia, ila Chadema ambao walikuwa wakimponda na sasa wanasema afadhali yake, mfano mtu kama Lissu...
 
Back
Top Bottom