Nani aliyesema wanaoondoka ni wanyarwanda peke yao?
Soma magazeti ya leo. Wanyarwanda 520 wameshaondoka kurudi kwao. Soma Mwananchi. Usibishe hata kwa mambo yaliyo wazi kabisa.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nani aliyesema wanaoondoka ni wanyarwanda peke yao?
Mwanakijiji is an IDIOT asiyejua kinachoendelea Tanzania. Anaendeshwa na chuki iliyomjaa juu ya Rais wetu.
Hao wahamiaji haramu wana silaha za kivita na wanaua polisi na watanzania wengine wanaoishi maeneo hayo. Mtu mwenye silaha ya kivita unamuondoa kwa kutumia nini zaidi ya jeshi?
jibu maswali unayoulizwa!alichokifanya JK ndio utaratibu?hapo ndipo linapokuja swali la mleta hoja ....ni utaratibu upi alioutumia Mwalimu kukabiliana na jambo hili?kuna post yako moja umekiri kuwa wote hawa wanaongozwa au wanatakiwa kuongozwa na sera zilezile za chama chako sasa iweje wachukue 'utaratibu' tofauti katika kudeal na jambo lile lile?shame!Kila kitu kina utaratibu wake wa kukishighulikia.
jokaKuu,
Mimi nimemwelewa Mwanakijiji. Of course Nyerere hajawahi kufukuza mkimbizi yeyote iwe ametoka Kenya, Uganda hata Malawi. Ndio point ya Mwanakijiji hiyo. Waganda waliosaidiwa ni wale waliokimbia kutoka utawala wa Idd Amin. Hivi huoni kuwa ni ajabu kwa rais Kikwete kutaka wakimbizi wasio halali warudi kwao wakati huu wa ugomvi wake na Kagame? Je, atafanya msako pale Kariakoo kuwaondoa Wachina, wahindi na wapakistan walioko Tanzania kinyume na sheria. Kwa nini wanaoondoka ni Wanyarwanda peke yao?
............Vilevile hawa mashabiki wa Kagame wanashindwa kuelewa kuwa unapokuwa na wahamiajo haramu, adui yako anaweza kuleta wanajeshi wake nchini kwako washambulie huku wakijifanya kuwa wao ni wahamiaji haramu. Hili analifanya Kagame huko Congo kwa kupeleka wanajeshi wake na kuwavisha uniform za waasi.......
adolay,
..naomba kutofautiana kidogo na wewe.
..Kagera kuna tatizo la ujambazi. Raisi ametoa wiki 2 kwa MAJAMBAZI kusalimisha silaha zao.
..Kagera kuna tatizo la walioingiza mifugo ktk maeneo yasiyostahili kama hifadhi za taifa. Hao pia wamepewa wiki 2 watoe mifugo yao.
..Kagera kuna tatizo la wahamiaji toka nchi jirani. Raisi kawapa wiki 2 waweke mambo yao sawa, au warudi nchi walikotoka.
..hivi Raisi anayebembeleza mpaka majambazi anapaswa kuitwa dikteta kweli? kuwapa muda watu waliovunja sheria waziwazi ni udikteta?
..Raisi amechukua maamuzi hayo baada ya kusikia malalamiko toka kwa wananchi wa Kagera. Nakushauri usome au usikilize hotuba ya Raisi.
..In 2010, Kikwete akiwa ndiyo Raisi wetu, Tanzania iliwapa uraia wakimbizi 160,000 toka Burundi. Sasa madai kwamba Kikwete ni mkatili na dikteta yanatoka wapi?
..Mwisho, natofautiana na Raisi Kikwete ktk masuala chungu nzima, lakini katika hili nakubaliana na hatua alizochukua.
cc Sikonge, Ogah
Mkuu asante sana kwenye hiyo quote hapo juu.........unajua watu wanazungumzia unafiki nafikiri hawajui maana ya unafiki......mtu huwezi kujinafiki.......bali unanafikiwa....hawajui unafiki wa baadhi ya majirani zetu (na hasa Rwanda).............all these shenanigans....it was just a matter of time........now time is telling.....watu wanapiga mayowe hapa.......kweli inashangaza sana........
Inashangaza kwa kuwa.......baadhi ya watu hapa wanataka kutuambia........eti kwa kuwa tuna matatizo 1,2,3,4.....then tusithubutu kukabiliana na tatizo 5, 6,and 7........hii akili sijui ni ya wapi.......kwenye muktadha huu sijui wanatumia sayansi gani kwamba usipotatua hili tatizo usitatue lile......otherwise eti ni unafiki!!........wanatumia neno unafiki pasipo.......
Wakuu Kobello , JokaKuu and masopakyindi heko kwa michango murua so far kwenye hii issue......

Mkuu asante sana kwenye hiyo quote hapo juu.........unajua watu wanazungumzia unafiki nafikiri hawajui maana ya unafiki......mtu huwezi kujinafiki.......bali unanafikiwa....hawajui unafiki wa baadhi ya majirani zetu (na hasa Rwanda).............all these shenanigans....it was just a matter of time........now time is telling.....watu wanapiga mayowe hapa.......kweli inashangaza sana........
Inashangaza kwa kuwa.......baadhi ya watu hapa wanataka kutuambia........eti kwa kuwa tuna matatizo 1,2,3,4.....then tusithubutu kukabiliana na tatizo 5, 6,and 7........hii akili sijui ni ya wapi.......kwenye muktadha huu sijui wanatumia sayansi gani kwamba usipotatua hili tatizo usitatue lile......otherwise eti ni unafiki!!........wanatumia neno unafiki pasipo.......
Wakuu Kobello , JokaKuu and masopakyindi heko kwa michango murua so far kwenye hii issue......
Huo ni mtazamo wako na nimawazo mgando!Enyi watanzania mliojaa unafiki miyoni mwenu na kujiita watu wa amani mbona matendo na maneno yenu yanawasuta.
1.Rais kikwete aliwahi kusema anawajua wauza unga kwa majina lakini hakuwataja wala kuwachukulia hatua.matokeo yake tumeona vijana kama kina Langa,Ngwea na Ray C wakiangamia kwa sembe
2.Rais kikwete aliwajua mafisadi walionyakua vitita vya mabilioni ya shilingi lakini aliwasamehe na kuwaomba warejeshe.
3.Serikali ya rais kikwete imeshuhudia matukio ya kikatili kama kuteswa kwa Dr Ulimboka,Kibanda.kupigwa mabomu kwenye mikutano ya kidini na mauaji kadhaa bila kuchukua hatua stahiki za udhibiti.
4.Serikali hiyo hiyo ya JK imeshindwa kutimiza ahadi ilizoahidi kwa wananchi na badala yake kuyafanya maisha kuwa magumu zaidi.
Leo hii ukiniambia kuondoa wahamiaji haramu walioko kagera ndio priority hasa baada ya msigano kati yake na kagame nitakuona u-mnafiki wa kutupwa.
Jambo hili halitasukuma maendeleo ya kiuchumi ukilinganisha na mambo niliyoyataja hapo juu,sanasana litazorotesha uchumi na uhusiano wetu wa kidiplomasia.
TUSIWE WANAFIKI!!!
naamini mwanakijiji anaishi marekani kama mhamiaji haramu na hana any legal documents zakumfanya aishi huko!! kwa maana kama anaelewa athari za wahamiaji haramu asingeongea huu utumbo aliouandika, ulaya nzima kwa sasa kampeni za kisiasa hutawaliwa na ishu ya kuhandle wahamiaji haramu, uingereza, ufaransa,italy,spain,sweden nakadhalika kote huku wahamiaji haramu wanawekwa maeneo maalum wanachunguzwa sababu za uhamiaji wao na kama hawakidhi vigezo wanakuwa deported back to their countries!!
tuseme haya mwanakijiji hayafahamu? au kujitia hamnazo tu ili apate sababu ya kupinga serikali? hana tofauti na Dr Slaa kwamba yeye kila kitu cha serikali basi ni kupinga tuuu, hizi ni akili za kawaida au akili za kukariri? wana tofauti gani basi hawa na wabunge wa CCM ambao hupinga kila mchango wa mbunge wa upinzani?
unafiki ni janga kubwa tulilonalo Tanzania, na kama hakuna uzalendo wa dhati basi hatuna chetu tena
Hivi kuna mtu hatari kuliko Mwigulu Nchemba? ni wapi na lini Mzee Mwanakijiji alituhumiwa kupanga na kutekeleza njama za mauaji kama afanyavyo Mwigulu?Mwanakijii anaendeshwa na chuki aliyo nayo juu ya Rais wetu.
Hakuna kingine.
Hata Kikwete angesema "tuwavumilia wahamiaji toka nchi jirani mpaka serikali zao zitakapokuwa tayari kuwahcukua" pia angeandika article ya kupinga.
Watu kama hawa kwenye jamii hawakosekani, ila tatizo ni kwamba kwa Tanzania ya sasa watu kama hawa ni hatari sana.
Kwa mfano anapomlinganisha Nyerere na Kikwete lengo lake ni kujustify nini? Hivi tukifikia conclusion kwamba Nyerere alifanya maamuzi bora zaidi ya Kikwete, then what?
Chuki inampeleka kubaya sana Mwanakijiji.
Naomba kuuliza, hivi mtu mwenye silaha za kivita na anayeua raia(kwa mujibu wa maelezo yako)hata kama ni mhamiaji adhabu yake ni amir jeshi mkuu kuyaagiza majeshi kumuondoa nchini au ni kumkamata na kumfikisha mahakamani?(nimelipuuza tusi lako kwa Mwanakijiji​😉
Hivi kuna mtu hatari kuliko Mwigulu Nchemba? ni wapi na lini Mzee Mwanakijiji alituhumiwa kupanga na kutekeleza njama za mauaji kama afanyavyo Mwigulu?
Hapa tuweni wakweli tu, waliolengwa kwenye huo mwavuli wa wahamiaji haramu ni wanyarwanda, tuacheni unafiki.
Kama hakulenga wanyarwanda, kwa nini azungumzie kwenye wahamiaji wengi wanyarwana asiende kuzungumzia mpaka wa Namanga?
jokaKuu,
Mimi nimemwelewa Mwanakijiji. Of course Nyerere hajawahi kufukuza mkimbizi yeyote iwe ametoka Kenya, Uganda hata Malawi. Ndio point ya Mwanakijiji hiyo. Waganda waliosaidiwa ni wale waliokimbia kutoka utawala wa Idd Amin. Hivi huoni kuwa ni ajabu kwa rais Kikwete kutaka wakimbizi wasio halali warudi kwao wakati huu wa ugomvi wake na Kagame? Je, atafanya msako pale Kariakoo kuwaondoa Wachina, wahindi na wapakistan walioko Tanzania kinyume na sheria. Kwa nini wanaoondoka ni Wanyarwanda peke yao?
Tuanze na kumkemea kwa nguvu zetu zote unyama na ushenzi wa Mwigulu Nchemba na siasa zake chafu za kiuaji, hivi wewe binafsi huuoni unyama wa Mwigulu? Mzee Mwanakijiji katoa hoja yake watu wachangie, lakini Mwigulu katenda unyama dhahiri.Hivi Mwanakijiji alivyofanya uchochezi wa kumtaka Kadinali pengo aitishe vita vya kidini sio njama ya uuaji?
Mwanakijiji inabidi ajue kuwa haya maandishi yake ya kichochezi siku kikilipuka atajumuishwa the Hegue kama yule mtangazaji wa Kenya...
Umemsahau na Lwakatare ha ha haaHivi kuna mtu hatari kuliko Mwigulu Nchemba? ni wapi na lini Mzee Mwanakijiji alituhumiwa kupanga na kutekeleza njama za mauaji kama afanyavyo Mwigulu?