KERO Taarifa Binafsi: Kampuni ya mkopo mtandaoni (online loan app) imenidhalilisha sana

KERO Taarifa Binafsi: Kampuni ya mkopo mtandaoni (online loan app) imenidhalilisha sana

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Hiyo ni wazi,mahakamani hawawezi kukupeleka kwa sababu watajiharibia wenyewe.
1. Ni kweli,unapokopa wanasaidia. Na si kwamba watu hawawezi kurudisha. Ila kama mnataka biashara iende vizuri(wakopeshaji)

-jaribuni kupunguza liba.
-kuweni wastaarabu. Ikibidi,onaneni na mkopaji,kukwama si ajabu,anaweza lipa hata nusu nusu na akamaliza.
-acheni ujinga na uhuni. Mkidai watu,utakuda tena si namba ya kampuni husika inayokudai, unaanza kutumiwa sms na namba nyingi sana. Kiofisi,hiyo itawashushia hadhi na kuwafanya muonekani hamjielewi.

2. Kuruhusiwa kuaccess contacts na sms, hakuwapi mamlaka ya kuwatafuta waliomo kwenye simu. Kisheria,hizi taasisi haziruhusiwi kudukuwa mawasiliano ya mtu,ukizingatia hazitambuliki. Ukikutana na mteja mjanja, kesi ni hot keki na inalipa sana.

3. Mkiona mtu harudishi hiyo hela, kuna mawili. Huenda kakosa kabisa. Kaeni nae,mpendi hata option ya kulipa kwa awamu.
Vinginevyo, huenda haogopi kudhalilika. Je,dunia ya leo,ataulizwa ulikopa? Atajibu ndio. Atauliza walokukopesha unawajua? Atajibu siwajui.
Kama siyo benki,si taasisi inayojulikana, utamdhalilisha kwa nani?

Uzi huu wameanzisha wao,na kujibizana wao.
Wekeni utaratibu wa kistaarabu. Kama mkopaji anachukua 20,000 anarusisha 35,000 wakiwa wengi mmekomboa hasara ya asiye lipa. Fanyeni arudishe hata 25,000 muone kama watu hawatawalipa.

Pili,hela za kugawa kama njugu mtandaoni,mnazitoaga wapi?! Basi ongeeni na Voda,Tigo na mitandao mingine wawe wanakata wateja na kuwalipa!
Castr pita hapa
 
Twin_Kids

Mahakamani unaweza kupelekwa na kesi ikawa against your favor.

Ukienda BRAC au NMB kukopa unaweka dhamana kitu. Online hauweki kitu, in theory tunatarajia hitaji lako la next loan ndilo litakupush ulipe (in practice ni mchanganyiko na sitaandika)

a) Ili nijue riba ya kampuni natakiwa kujua principal amount aliyopokea mleta uzi na alichotakiwa kurudisha. Riba imo ndani ya maelekezo ya BOT.

b) Mkopo ni wa online. Kuonana, kunaua logic ya msingi ya mkopo wa online.

c) Unatumiwa SMS/ Unapigiwa na namba tofauti kwakua mteja una stages. Kuna stage 0 (Kabla haujaoverdue), stage 1 (baada ya kuoverdue kwa siku 1 mpaka 3 au 7), stage 2 (umeoverdue kuanzia siku 4 n.k) so ni lazima utapigiwa na namba tofauti kwakua hizo stages zote zina staff tofauti.

2) Upo sahihi. Kuna namna za kuongea na mteja na emergency contacts. Hizi contacts ambazo wamepata access sijui sheria inasemaje. Hizi siwezi kuzisemea, kama unahisi unaweza kushinda mahakamani jaribu kumshirikisha mwanasheria.

3) Taasisi zinajulikana. Nilielezea ni kwanini mnafeel hazijulikani but zinajulikana. So kutojulikana usiutumie kama msingi, as I said earlier ni ngumu online platform na mteja kukutana kudiscuss malipo, ikiwa mteja anaona kuna umuhimu huo ni bora akapokea simu na kujielezea.

Of course kampuni nyingi hua zinaweza kumfanyia exemption mteja mfano badala ya 35K akalipa 25K. Kwa ulichoandika hapa naona haujui Fintech inafanyaje kazi kwa % kubwa.

Hela za kugawa kama njugu? Hili swali ni la kitoto mno sioni kama ni level yangu ya uelewa kulijibu. Kama mitandao ya simu itakua inakata pesa kutakua hakuna haja ya uwepo wa debt collectors.
 
Twin_Kids

Mahakamani unaweza kupelekwa na kesi ikawa against your favor.

Ukienda BRAC au NMB kukopa unaweka dhamana kitu. Online hauweki kitu, in theory tunatarajia hitaji lako la next loan ndilo litakupush ulipe (in practice ni mchanganyiko na sitaandika)

a) Ili nijue riba ya kampuni natakiwa kujua principal amount aliyopokea mleta uzi na alichotakiwa kurudisha. Riba imo ndani ya maelekezo ya BOT.

b) Mkopo ni wa online. Kuonana, kunaua logic ya msingi ya mkopo wa online.

c) Unatumiwa SMS/ Unapigiwa na namba tofauti kwakua mteja una stages. Kuna stage 0 (Kabla haujaoverdue), stage 1 (baada ya kuoverdue kwa siku 1 mpaka 3 au 7), stage 2 (umeoverdue kuanzia siku 4 n.k) so ni lazima utapigiwa na namba tofauti kwakua hizo stages zote zina staff tofauti.

2) Upo sahihi. Kuna namna za kuongea na mteja na emergency contacts. Hizi contacts ambazo wamepata access sijui sheria inasemaje. Hizi siwezi kuzisemea, kama unahisi unaweza kushinda mahakamani jaribu kumshirikisha mwanasheria.

3) Taasisi zinajulikana. Nilielezea ni kwanini mnafeel hazijulikani but zinajulikana. So kutojulikana usiutumie kama msingi, as I said earlier ni ngumu online platform na mteja kukutana kudiscuss malipo, ikiwa mteja anaona kuna umuhimu huo ni bora akapokea simu na kujielezea.

Of course kampuni nyingi hua zinaweza kumfanyia exemption mteja mfano badala ya 35K akalipa 25K. Kwa ulichoandika hapa naona haujui Fintech inafanyaje kazi kwa % kubwa.

Hela za kugawa kama njugu? Hili swali ni la kitoto mno sioni kama ni level yangu ya uelewa kulijibu. Kama mitandao ya simu itakua inakata pesa kutakua hakuna haja ya uwepo wa debt collectors.
Overdue gani mimi watu wametumiwa sms asubuhi saa nne wakati nilitakiwa nilipe saa kumi
 
Wanakupunguzia heshima!

Wapo watu wanakuheshimu na ni muda hawajasikia kutoka kwako so wakiona sms dizain hiyo wanasema huyu jamaa alivyokuwa smart siku hizi amekuwa tapeli anatapeli mpaka mitandaoni?basi siyo wa kumuamini tena na hata siku ukiwatafuta kwa ishu serious hawakusikilizi.
Wanafanya kusudi hao wakopeshaji...lengo tu ili endelee kuwa mateka wao wa kuwakopa maana washakuchafua kwa jamaa zako lazima kurudi kwao kukopa.

Kudhibitisha hilo, mwenzetu hapo katueleza kuwa PS wao alilipa deni lakini bado wakamtangaza kwa jamaa zake hajalipa.
 
Pole kwa yaliyokukuta ndugu Putin;

Kwa sasa wewe walipe pesa yao kwanza; halafu rudi kwenye Vigezo na Masharti ya mkopo, inawezekana hukusoma vizuri ama ulisoma vizuri na hakuna popote ambapo kulikuwa na suala la Contacts kwenye simu yako kujulishwa juu ya kushindwa kwako kulipa mkopo.
Kutokulipa mkopo kwa wakati sio utapeli.

Kama una muda wa kutosha kushughulikia hili basi endelea na kesi; ila nikushauri tu kwa sasa jipe muda kwanza walau siku tatu ukae na utafakari.

Nikupe ushauri tu; kwa kweli usiwaze sana kuhusu kudhalilika kwa sababu hao watu unawaona na kudhani kuwa hawana mikopo wapo ambao wanayo mikopo. Na hata wale ambao hawana mikopo bado hawawezi kushangaa kudaiwa 50,000/- ni maisha tu na matukio yake.
 
Overdue gani mimi watu wametumiwa sms asubuhi saa nne wakati nilitakiwa nilipe saa kumi
Overdue ni siku siyo saa.

Kama unatakiwa kulipa Ijumaa.

Alhamis utakumbushwa.

Ijumaa utadaiwa. So hata kama ni Ijumaa saa 1 asubuhi tayari ni Ijumaa
 
Watu wengi hawajui vitu ila wanaandika kama wanajua.

Hii ndiyo shida ya online.

Katika watu wote kuna jamaa anaandika lakini naona ni anaandika kwa hisia huku hana taarifa sahihi.

Vladmir Putini elewa kila nilichoandika. Nimekuandikia vingi nimegusa hadi hiyo option ya mahakama ambayo kuna member anasema wakipata kauzu atapiga hela.
 
Watu wengi hawajui vitu ila wanaandika kama wanajua.

Hii ndiyo shida ya online.

Katika watu wote kuna jamaa anaandika lakini naona ni anaandika kwa hisia huku hana taarifa sahihi.

Vladmir Putini elewa kila nilichoandika. Nimekuandikia vingi nimegusa hadi hiyo option ya mahakama ambayo kuna member anasema wakipata kauzu atapiga hela.
Ki ufupi mahakamani siendi, na deni silipi, nimeshakopa makampuni 8 sasahivi na sina mpango wa kuwalipa, mahakamani waanze wao kwenda
 
Overdue ni siku siyo saa.

Kama unatakiwa kulipa Ijumaa.

Alhamis utakumbushwa.

Ijumaa utadaiwa. So hata kama ni Ijumaa saa 1 asubuhi tayari ni Ijumaa
Hivi unajua maana ya overdue unayoizungumzia wewe.

Mimi nnachojua overdue ni kupitiliza siku/mda ulitakiwa kulipa.

Leo ni jumatatu natakiwa kulipa leo jumatatu pesa, alafu iweje asubuhi tu uamke uanze kuwatumia sms watu mimi ni tapeli.

Ungesubiri jumanne ifike ndiyo useme nime overdue
 
Pole kwa yaliyokukuta ndugu Putin;

Kwa sasa wewe walipe pesa yao kwanza; halafu rudi kwenye Vigezo na Masharti ya mkopo, inawezekana hukusoma vizuri ama ulisoma vizuri na hakuna popote ambapo kulikuwa na suala la Contacts kwenye simu yako kujulishwa juu ya kushindwa kwako kulipa mkopo.
Kutokulipa mkopo kwa wakati sio utapeli.

Kama una muda wa kutosha kushughulikia hili basi endelea na kesi; ila nikushauri tu kwa sasa jipe muda kwanza walau siku tatu ukae na utafakari.

Nikupe ushauri tu; kwa kweli usiwaze sana kuhusu kudhalilika kwa sababu hao watu unawaona na kudhani kuwa hawana mikopo wapo ambao wanayo mikopo. Na hata wale ambao hawana mikopo bado hawawezi kushangaa kudaiwa 50,000/- ni maisha tu na matukio yake.
Ushauri wako mzuri, ila kuwalia siwalipi, wanadharau sana hao jamaa.

Nimepoteza vingi sana kwa sababu ya sms yao
 
Ushauri wako mzuri, ila kuwalia siwalipi, wanadharau sana hao jamaa.

Nimepoteza vingi sana kwa sababu ya sms yao
Well, unaweza kuamua usiwalipe naamini ipo ndani ya uwezo wako.

Labda nikuulize, ulichelewa kuwalipa wakaamua kukudhalilisha kwa ndugu jamaa, marafiki, business partners, wafanyakazi wenzako, majirani, bodaboda, mashemeji na wakwe zako.
Wao wataendelea kutuma hizo meseji kwa hao watu mfululizo kwa siku hata kwa wiki kadhaa. Ipi bora kwako, kulipa na kuendelea na maisha yako au hao contacts zaklo waendelee kupokea meseji za kwamba wewe ni Tapeli?
Mambo ya kuzingatia yapo kwenye haya maswali
1. Je ni kweli ulikopa? - Wakati uliopita
2. Je ni kweli ulikuwa na nia ya kulipa? - Jukumu la sasa

Hakuna atakayeshangaa wewe kukopa na kudaiwa ila kila mtu atashangaa kwamba ulikopa na sasa hutaki kulipa.

Sijui una umri gani ila maisha yamenifundisha kuwa ni rahisi kuishi kama utaruhusu mambo yaishe. Katika hili kuruhusu kuisha ni kukubali kulipa.

Zingatia kuwa siungi mkono suala la hii kampuni kutuma hizo meseji kwa contacts zako.
 
K
Well, unaweza kuamua usiwalipe naamini ipo ndani ya uwezo wako.

Labda nikuulize, ulichelewa kuwalipa wakaamua kukudhalilisha kwa ndugu jamaa, marafiki, business partners, wafanyakazi wenzako, majirani, bodaboda, mashemeji na wakwe zako.
Wao wataendelea kutuma hizo meseji kwa hao watu mfululizo kwa siku hata kwa wiki kadhaa. Ipi bora kwako, kulipa na kuendelea na maisha yako au hao contacts zaklo waendelee kupokea meseji za kwamba wewe ni Tapeli?
Mambo ya kuzingatia yapo kwenye haya maswali
1. Je ni kweli ulikopa? - Wakati uliopita
2. Je ni kweli ulikuwa na nia ya kulipa? - Jukumu la sasa

Hakuna atakayeshangaa wewe kukopa na kudaiwa ila kila mtu atashangaa kwamba ulikopa na sasa hutaki kulipa.

Sijui una umri gani ila maisha yamenifundisha kuwa ni rahisi kuishi kama utaruhusu mambo yaishe. Katika hili kuruhusu kuisha ni kukubali kulipa.

Zingatia kuwa siungi mkono suala la hii kampuni kutuma hizo meseji kwa contacts zako.
Ni kweli nilikopa.

Ni kweli nilikuwa na nia ya kuwalipa.

Na kitu kingine ni kwamba sikupitiliza mda wa kuwalipa.

Mfano : natakiwa kulipa deni leo jumatatu, then wao wakaamka asubuhi hiyo jumatatu wakasambaza sms kwa contact zangu kuwa mimi nina nia ya kuwatapeli.

Sms hizo zilifanya niingie doa sana kwa baadhi ya watu nna heshimiana nao wakiamini kwamba mimi niliwaweka kama wadhamini.

Ni kibaya zaidi wakawa wanawapigia baadhi simu wakiwaambia wananidai laki 5 instead of 56,000/=

Hali hiyo ilinivuruga na kunipa msongo wa mawazo na ndiyo hapo nia ya kutowalipa ilipoondoka kabisa.

Maana nikaona kama kudhalilika nishadhalilika alafu hao hao walionidhalilisha eti niwalipe tena, kwangu mimi hapana.

Nikuulize wewe swali, kwenye muktadha wako wa kukubali yaishe, unadhani nikiwalipa ndiyo udhalilishaji walionifanyia utafutika na kurudisha heshima yangu kwa watu hao kama mwanzo ?

Kama jibu itakuwa ni hapana, unadhani kwanini sasa niwalipe ?
 
Hivi unajua maana ya overdue unayoizungumzia wewe.

Mimi nnachojua overdue ni kupitiliza siku/mda ulitakiwa kulipa.

Leo ni jumatatu natakiwa kulipa leo jumatatu pesa, alafu iweje asubuhi tu uamke uanze kuwatumia sms watu mimi ni tapeli.

Ungesubiri jumanne ifike ndiyo useme nime overdue
Upo sahihi; hawakuzingatia muda wa mkopo
 
K

Ni kweli nilikopa.

Ni kweli nilikuwa na nia ya kuwalipa.

Na kitu kingine ni kwamba sikupitiliza mda wa kuwalipa.

Mfano : natakiwa kulipa deni leo jumatatu, then wao wakaamka asubuhi hiyo jumatatu wakasambaza sms kwa contact zangu kuwa mimi nina nia ya kuwatapeli.

Sms hizo zilifanya niingie doa sana kwa baadhi ya watu nna heshimiana nao wakiamini kwamba mimi niliwaweka kama wadhamini.

Ni kibaya zaidi wakawa wanawapigia baadhi simu wakiwaambia wananidai laki 5 instead of 56,000/=

Hali hiyo ilinivuruga na kunipa msongo wa mawazo na ndiyo hapo nia ya kutowalipa ilipoondoka kabisa.

Maana nikaona kama kudhalilika nishadhalilika alafu hao hao walionidhalilisha eti niwalipe tena, kwangu mimi hapana.

Nikuulize wewe swali, kwenye muktadha wako wa kukubali yaishe, unadhani nikiwalipa ndiyo udhalilishaji walionifanyia utafutika na kurudisha heshima yangu kwa watu hao kama mwanzo ?

Kama jibu itakuwa ni hapana, unadhani kwanini sasa niwalipe ?
Usiwalipe kama ambavyo umeamua.
 
Huenda ni mimi nilifanya makosa kwa kutopitia terms & conditions vizuri ila hawa jamaa walicho nifanyia ni uzalilishaji mkubwa sana.

Kuna app moja mtandaoni (play store) inaitwa "PESA M FINANCE".

Hawa jamaa walinikopesha elfu 42 mtandaoni kwa muda wa siku 7.

Siku jana nilitakiwa ndiyo nilipe, na jana hiyo nilikuwa kazini nikitegemea nitoke kazini jioni niwalipe pesa yao.

Lakini nashangaa jana mida ya mchana saa saba, watu wanaanza kunitumia kunipigia simu na kunifoadia sms kuwa nadaiwa.

Kumbe hii kampuni ilichofanya baada ya kunikosa hewani jana mda flani, wakatuma sms kwa watu wote walioko kwenye phone book yangu (watu zaidi ya 200) kuwajuza kuwa wananidai na nataka kuwatapeli.

Nikawa napata simu ngingi sana kutoka kwa hao watu waliotumiwa hiyo sms.

Aisee niliona ni udhalilishaji sana hii kampuni imenifanyia.

Sasa nikajiuliza walipataje majina yaliyopo kwenye simu yangu, hapo ndipo nilipokumbuka kwenye app yao ukiwa unafungua kuna sehemu itaandika "allow access to your contacts, messeges n.k" hapo ndipo walipopata majina ya phone book yangu.

Sasa tangu jana hiyo nimekosa raha kabisa baada ya kuzalilishwa na mimi nimeamua kutowalipa mpaka sasa.

Nimepata wazo la kutafta mwanasheria nikawafungulie kesi ya kunidhadhalisha wanilipe fidia, kwanini wanidhalilishe wakati dead line ya malipo ilikuwa bado haijapita.

View attachment 2910966View attachment 2910967
Walisha haribikiwa kisaikolojia kwamba ukichelewa Tu kuwalipa hata kama ni siku tatu kabla ya siku za rejesho wanaanza vitimbi vya kizalilishaji.

Mimi nilivyoona wameanza huo ujinga niliachana na mamikopo Yao. Yaani walisha athirika na kutapeliwa tatizo Lao ni Liba kubwa muda mfupi MTU mwenye njaa anaona Acha akope hivyo hivyo.
 
Back
Top Bottom