KERO Taarifa Binafsi: Kampuni ya mkopo mtandaoni (online loan app) imenidhalilisha sana

KERO Taarifa Binafsi: Kampuni ya mkopo mtandaoni (online loan app) imenidhalilisha sana

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Hiyo access uliwapa wewe mwenyewe....
Mara ya kwanza ulipoanza kutumia hiyo app ilikutaka uruhusu matumizi kama location,storage na some authority options ndio maana yamekutokea hayo....

Hao dawa yao simu inakua rooted,Una remove acces ya contact unawaomba mkopo,wanakupa....
Unafungua lucky patcher unaedit custom firmware za app halafu unafuta na application
Unaonekana unafaham mengi sana, emb nijuze kuhusu ku root simu
 
Wanakupunguzia heshima!

Wapo watu wanakuheshimu na ni muda hawajasikia kutoka kwako so wakiona sms dizain hiyo wanasema huyu jamaa alivyokuwa smart siku hizi amekuwa tapeli anatapeli mpaka mitandaoni?basi siyo wa kumuamini tena na hata siku ukiwatafuta kwa ishu serious hawakusikilizi.
Tuwe wakweli sisi watanzania hatuna hulka ya kulipa mikopo kwa wakati, mfano wewe hiyo 42,000 umeomba mkopo na kupewa siku hiyo hiyo, ukaondoa shida yako. Sasa ni kwa nini usilipe hiyo pesa ndani ya muda au hata Kabla ya siku 7 kwisha?? Mwisho kila ikifika mwisho wa mwaka jitahidi ku edit phone book [emoji428] yako ili ufute Namba ambazo hazina umuhimu kwako, afadhali ubaki na majina 50 ya muhimu kuliko 200 hewa.
 
Tuwe wakweli sisi watanzania hatuna hulka ya kulipa mikopo kwa wakati, mfano wewe hiyo 42,000 umeomba mkopo na kupewa siku hiyo hiyo, ukaondoa shida yako. Sasa ni kwa nini usilipe hiyo pesa ndani ya muda au hata Kabla ya siku 7 kwisha?? Mwisho kila ikifika mwisho wa mwaka jitahidi ku edit phone book [emoji428] yako ili ufute Namba ambazo hazina umuhimu kwako, afadhali ubaki na majina 50 ya muhimu kuliko 200 hewa.
Haya mtoa mada kakuelewa.

Vipi kwa upande wa Kampuni iyo kutuma izo SMS ni sawa?
 
Mkuu wewe ni mtu na nusu sana ani.

Umenifanya fikra zangu zikafunguka.

Nimeingia website ya BOT kama ulivyosema kuwa kule kuna ufafanuzi.

Nimekuta orodha ya kampuni za micro-y finance zenye leseni ya BOT, ziko kama kampuni 1500 na point kidogo.

Kati ya hizo 1500 zenye leseni, MKOPO FASTA (PESA M LOAN) haipo.

Alafu pia nikasoma notice ikiyotolewa na BOT mwezi january 2024, inaagiza kwamba micro finance yeyote inayokukopesha ikupe nakala ya MKATABA, mimi sina MKATABA wao.

Kumbe nimekuja kugundua ni wahuni ambao wanavuna pesa kihuni.
Kwa 97% ukienda na huu ushahidi mahakamani unapotea.

Mkopo Fasta na Pesa M loan siyo kampuni ni products za kampuni. Ambazo wewe unazipata kama applications playstore.

Kampuni ina jina lake. Kama hiyo doc ya BOT ungekua nayo ningeisoma nikutajie kama hii kampuni ipo au haipo.

Waziaa JamiiForums wawe na app ya kukopesha iitwe JamiiPesa. So hautakuta jina la JamiiPesa BOT bali Jamiiforums. Pia wewe umekopeshwa online, mkataba ni zile yes ulizobonyeza muda unakopa.

Pia, kampuni mpya inaweza operate wakati inasubiri vibali. Kikubwa maombi yawe yalishafanywa.

So jiangalie
 
Zachini chini, wanapiga pesa ndefu kwenye kuwatisha watu kuwa watavujisha picha na video zao za uchi au ngono,..hivyo kuna watu wanalipa kila mwezi hata baada ya mkopo kuisha....
Toa evidence juu ya hii ishu.

Hebu fikiria kwa akili ya kawaida.

Mtu anayekopa 42,000 ana influence gani kwa jamii kiasi tukiona picha yake tushangae?

Unajua kama blackmailing ni kosa kisheria?
 
Huenda ni mimi nilifanya makosa kwa kutopitia terms & conditions vizuri ila hawa jamaa walicho nifanyia ni uzalilishaji mkubwa sana.

Kuna app moja mtandaoni (play store) inaitwa "PESA M FINANCE".

Hawa jamaa walinikopesha elfu 42 mtandaoni kwa muda wa siku 7.

Siku jana nilitakiwa ndiyo nilipe, na jana hiyo nilikuwa kazini nikitegemea nitoke kazini jioni niwalipe pesa yao.

Lakini nashangaa jana mida ya mchana saa saba, watu wanaanza kunitumia kunipigia simu na kunifoadia sms kuwa nadaiwa.

Kumbe hii kampuni ilichofanya baada ya kunikosa hewani jana mda flani, wakatuma sms kwa watu wote walioko kwenye phone book yangu (watu zaidi ya 200) kuwajuza kuwa wananidai na nataka kuwatapeli.

Nikawa napata simu ngingi sana kutoka kwa hao watu waliotumiwa hiyo sms.

Aisee niliona ni udhalilishaji sana hii kampuni imenifanyia.

Sasa nikajiuliza walipataje majina yaliyopo kwenye simu yangu, hapo ndipo nilipokumbuka kwenye app yao ukiwa unafungua kuna sehemu itaandika "allow access to your contacts, messeges n.k" hapo ndipo walipopata majina ya phone book yangu.

Sasa tangu jana hiyo nimekosa raha kabisa baada ya kuzalilishwa na mimi nimeamua kutowalipa mpaka sasa.

Nimepata wazo la kutafta mwanasheria nikawafungulie kesi ya kunidhadhalisha wanilipe fidia, kwanini wanidhalilishe wakati dead line ya malipo ilikuwa bado haijapita.

View attachment 2910966View attachment 2910967
Wapeleke Mahakamani kama hakuna kipengele hicho
 
Huenda ni mimi nilifanya makosa kwa kutopitia terms & conditions vizuri ila hawa jamaa walicho nifanyia ni uzalilishaji mkubwa sana.

Kuna app moja mtandaoni (play store) inaitwa "PESA M FINANCE".

Hawa jamaa walinikopesha elfu 42 mtandaoni kwa muda wa siku 7.

Siku jana nilitakiwa ndiyo nilipe, na jana hiyo nilikuwa kazini nikitegemea nitoke kazini jioni niwalipe pesa yao.

Lakini nashangaa jana mida ya mchana saa saba, watu wanaanza kunitumia kunipigia simu na kunifoadia sms kuwa nadaiwa.

Kumbe hii kampuni ilichofanya baada ya kunikosa hewani jana mda flani, wakatuma sms kwa watu wote walioko kwenye phone book yangu (watu zaidi ya 200) kuwajuza kuwa wananidai na nataka kuwatapeli.

Nikawa napata simu ngingi sana kutoka kwa hao watu waliotumiwa hiyo sms.

Aisee niliona ni udhalilishaji sana hii kampuni imenifanyia.

Sasa nikajiuliza walipataje majina yaliyopo kwenye simu yangu, hapo ndipo nilipokumbuka kwenye app yao ukiwa unafungua kuna sehemu itaandika "allow access to your contacts, messeges n.k" hapo ndipo walipopata majina ya phone book yangu.

Sasa tangu jana hiyo nimekosa raha kabisa baada ya kuzalilishwa na mimi nimeamua kutowalipa mpaka sasa.

Nimepata wazo la kutafta mwanasheria nikawafungulie kesi ya kunidhadhalisha wanilipe fidia, kwanini wanidhalilishe wakati dead line ya malipo ilikuwa bado haijapita.

View attachment 2910966View attachment 2910967
Kama changamoto ya Elfu 42 unashindwa itatua au walokuzunguka kukusaidia kuitatua basi achana na kuwaza mwanasheria
Amua moja kulipa au kuwarusha
 
Aisee, hao waduanzi kwani wangapi wanakopa. Ningekuwa mimi nisingewalipa maana wameshatumia silaha yao ya mwisho.

Alafu haina haja ya wewe kujisikia vibaya kwani sms katumiwa mtu mmoja mmoja kwahiyo kila mtu ataielewa kwa anavyo kufahamu ni rahisi kumjibu kuwa hao ni matapeli
Nilitumiwa na Sunloan kuwa rafiki yangu mmoja wa kike ni mdaiwa[emoji1787] nilipomuuliza akajibi simple tu kuwa matapeli hao
 
Kwa 97% ukienda na huu ushahidi mahakamani unapotea.

Mkopo Fasta na Pesa M loan siyo kampuni ni products za kampuni. Ambazo wewe unazipata kama applications playstore.

Kampuni ina jina lake. Kama hiyo doc ya BOT ungekua nayo ningeisoma nikutajie kama hii kampuni ipo au haipo.

Waziaa JamiiForums wawe na app ya kukopesha iitwe JamiiPesa. So hautakuta jina la JamiiPesa BOT bali Jamiiforums. Pia wewe umekopeshwa online, mkataba ni zile yes ulizobonyeza muda unakopa.

Pia, kampuni mpya inaweza operate wakati inasubiri vibali. Kikubwa maombi yawe yalishafanywa.

So jiangalie
Kubonyeza YES ndiyo mkataba wa maandishi ambao BOT imeelekeza ?

Nini maana ya BOT kusema "mkopeshaji akupe nakala ya mkataba wa maandishi ubaki nayo"
 
Silipi jomba na hamna kitu watanifanya.

Kwanini wanitangaze wakati dead line ilikuwa bado haijafika
doctor unakalia mbususu unashindwa kusave chochote matokeo yake umegeika tapeli. Lipa pesa ya watu mzee ama waombe chawa wenzio humu kina lucas wakusaidie kufukia mashimo... Ila wambie kabisa umebadili jina umerudia lile jina la zaman ili wakutambue wakulipie
 
Kubonyeza YES ndiyo mkataba wa maandishi ambao BOT imeelekeza ?

Nini maana ya BOT kusema "mkopeshaji akupe nakala ya mkataba wa maandishi ubaki nayo"
Trust me Bro.

Kama ushahidi wako ni ule. Unaenda kupotea.

Notice BOT kaelekeza hivyo kwaajili ya Microfinance.

Digital Lending Platforms zina sera na sheria zake ambazo ni tofauti na microfinance.

Anyway, nishachangia sana huu uzi wako kwa ninachokijua.
Kama utanielewa au hautanielewa katika nilichosema hapo ni juu yako.
 
View attachment 2911035
benki kubwa wanaonya watu kila siku
Hiyo ni wazi,mahakamani hawawezi kukupeleka kwa sababu watajiharibia wenyewe.
1. Ni kweli,unapokopa wanasaidia. Na si kwamba watu hawawezi kurudisha. Ila kama mnataka biashara iende vizuri(wakopeshaji)

-jaribuni kupunguza liba.
-kuweni wastaarabu. Ikibidi,onaneni na mkopaji,kukwama si ajabu,anaweza lipa hata nusu nusu na akamaliza. Sasa,unatuma meseji,imejaa lugha za kihuni na vitisho,unategemea nini? Kuna watu hawaogopi kudhalilika.
-acheni ujinga na uhuni. Mkidai watu,utakuda tena si namba ya kampuni husika inayokudai, unaanza kutumiwa sms na namba nyingi sana. Kiofisi,hiyo itawashushia hadhi na kuwafanya muonekani hamjielewi.

2. Kuruhusiwa kuaccess contacts na sms, hakuwapi mamlaka ya kuwatafuta waliomo kwenye simu. Kisheria,hizi taasisi haziruhusiwi kudukuwa mawasiliano ya mtu,ukizingatia hazitambuliki. Ukikutana na mteja mjanja, kesi ni hot keki na inalipa sana.

3. Mkiona mtu harudishi hiyo hela, kuna mawili. Huenda kakosa kabisa. Kaeni nae,mpendi hata option ya kulipa kwa awamu.
Vinginevyo, huenda haogopi kudhalilika. Je,dunia ya leo,ataulizwa ulikopa? Atajibu ndio. Atauliza walokukopesha unawajua? Atajibu siwajui.
Kama siyo benki,si taasisi inayojulikana, utamdhalilisha kwa nani?

4. Kama mnahitaji kuwa msaada kwa watu,elimisheni basi hata matumizi ya pesa. Watu wawe hata kikundi, kiwe na biashara inayoeleweka, kisheria,wakopesheni. Ila sasa,mti mmoja mmoja,liba kubwa.
Kwa anaewajua,anajua nyie ni wezi. Uzuri hamjifichi. Mnadaigi hela za wachina walikuja kuwekeza.
Mchina ana huruma gani na mbongo? Japo pia wana akili. Kwenye 100,000 yeye kupata 5,000 hana hasara. Kwa njaa zenu, kwenye hiyo laki,mnataka liba ya 47,000. Wapi na wapi!

Uzi huu wameanzisha wao,na kujibizana wao.
Wekeni utaratibu wa kistaarabu. Kama mkopaji anachukua 20,000 anarusisha 35,000 wakiwa wengi mmekomboa hasara ya asiye lipa. Fanyeni arudishe hata 25,000 muone kama watu hawatawalipa.

Pili,hela za kugawa kama njugu mtandaoni,mnazitoaga wapi?! Basi ongeeni na Voda,Tigo na mitandao mingine wawe wanakata wateja na kuwalipa!

Af cha ajabu,namba zote zinazodai,zikiwa whatsapp, ni picha za micharuko tuuuu. Haina shida, badhi yetu wanajipatia huduma kimasihara. Ajirimi watu wanaojielewa,wastaarabu. Mtu katukana mteja. Mnatarajia nini!! Sasa kama umemdhalilisha,unamdai wa nini wakati umeshajilipiza ujinga?

Wekeni mchanganuo wa malipo tuone na ushuru wa TRA.
Af,ongeeni na BOT.

Meseji inayowatumia watu,inawakost nyie,hamjui tu. Ina maanisha hamruhusiwi kukopa.
Na mahakama itamuamuru mtuhumiwa kulipa,lakini haimuwekei kiwango. Neva.
 
doctor unakalia mbususu unashindwa kusave chochote matokeo yake umegeika tapeli. Lipa pesa ya watu mzee ama waombe chawa wenzio humu kina lucas wakusaidie kufukia mashimo... Ila wambie kabisa umebadili jina umerudia lile jina la zaman ili wakutambue wakulipie
Wanipeleke mahamani wakanifunge kama wanaweza.

Silipi hata kumi hata kama uwezo wa kulipa nnao
 
Back
Top Bottom