Tetesi: Taarifa za ndani kabisa nilizopenyezewa zinasema huenda Feitoto akacheza Kariakoo isiyo na Mafuriko SC siku si nyingi

Fei toto kwa Simba ata wafaa, Sera za Yanga kwasasa ni tofauti kidogo wao wanataka mtu akiondoka basi wapate mchezaji aliye juu zaidi kuliko aliye ondoka.

Ata Saidoo ni mchezaji nyota pale msimbazi, Yanga kwasasa wana hangaikia replacement ya Mayele na wakifanikiwa kupata mtu zaidi ya Mayele itakua balaaa kubwa.
 
nasisitiza pasina kumung'unya maneno, katika soka la Tz kijana is no more fire,
atalazimishwa kudandia na kuruka hapa na pale, kwa zawadi nono ya fedha na mali,
lakini ndani ya kichwa na moyo wake akifarakana na kugandamizwa na majutrooo makubwa sana,
anajitajidi kurejea kwenye reli, lakini akichungulia nje anakutana na kelele za vishindo vya kukatisha tamaa,
kichwa inapasuka zaidi....

Ukweli Usemwe,
Ukweli ni kitu mbaya sana,
Mwili uko radhi moyo nnzito....
 
Sera na uwezo wa kuzitekeleza ni vitu viwili tofauti. Wewe mwenyewe umekiri kuwa wanatafuta mbadala wa Mayele, lakini uwezo ndio unawafanya waishie kuwachukua akina Konikoni
 
Sera na uwezo wa kuzitekeleza ni vitu viwili tofauti. Wewe mwenyewe umekiri kuwa wanatafuta mbadala wa Mayele, lakini uwezo ndio unawafanya waishie kuwachukua akina Konikoni
Yanga eneo la usajili wapo vizuri , Konkon alisajiliwa baada ya kushindwana ki maslahi na Mcameroon aliyetaka pesa ndefu baada ya mawakala wake kugundua Yanga imepiga fedha ndefu kwa Mayele.

Muda ukawa mchache na uhitaji ulikua mkubwa ila unao endana na budget, ukawapelekea Yanga kwenda kwa plan B ambayo mpaka sasa haija lipa.

Kwenye mpira hayo utokea ila kwa ujumla yanga wako vizuri katika usajili na January watarudi na mtu wa ukweli.
 
Ni ngumu kwa Feisal kwenda Simba, vipengele vya kimkataba vinawabana Azam na labda kuendelea tu na porojo za kujifurahisha hapa jf, yanga wao wanajua mkataba wao wa mauziano ya Feisal ulivyo ndio maana wametulia, hizi porojo za jf hapa acha ziendelee kuchangamsha jukwaa
 
Azam watamuuza Feisal kwa bei ndogo kwenda Coastal Union kwa mkataba wa miezi sita, halafu Coastal union watamtoa kwa mkopo wa hiyo miezi sita kwenda Simba, halafu akimaliza miezi sita anakuwa huru kujiunga Simba Julai mwakani. Hiyo ni biashara itakayofanyika kwenye makaratasi kuliruka sharti la wananchi. Biashara halisi itafanyika gizani
 
Hata plan A ingesingeweza kulipa pia. Kwenye soccer kuna mambo mengi yasiyotarajiwa hutokea. Mfuatilie Onana au lile forward pande la mtu pale chamanzi
 
Unavyo ongea kama vile wewe ndio Popat! yaani umuuze mchezaji kwa bei ndogo ili iweje? kwamba Azam wao wapo kuifurahisha Simba,?
 
Kilicho tokea ni ubahiri nothing more, haya kwa Adebayor, Aziz K, na Sopu ni kipi?
Tatizo unadhani ukihitaji mchezaji na yeye anakuhitaji. Aziz Ki na Sopu hawakuwa machaguo, Adebayor waarabu walimpagawisha kwa fedha kama ambavyo walimpagawisha Msuva hapa juzi akaiacha Yanga. Usajili ni mutual agreement, sio hela tu
 
Unavyo ongea kama vile wewe ndio Popat! yaani umuuze mchezaji kwa bei ndogo ili iweje? kwamba Azam wao wapo kuifurahisha Simba,?
Sikuanzisha uzi mimi. Nadhani unatakiwa umtolee mapovu aliyeanzisha huu uzi wenye title "Taarifa za ndani kabisa nilizopenyezewa zinasema huenda Feitoto akacheza Kariakoo isiyo na Mafuriko SC siku si nyingi"
 
Sikuanzisha uzi mimi. Nadhani unatakiwa umtolee mapovu aliyeanzisha huu uzi wenye title "Taarifa za ndani kabisa nilizopenyezewa zinasema huenda Feitoto akacheza Kariakoo isiyo na Mafuriko SC siku si nyingi"
Moto wangu anaujua vyema tu. Athubutu....!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…