Tabia ya kuwa na miadi sehemu na mwanamke, yeye anakuja na rafiki zake bado ipo?

Kuna demu nilikutana naye sehemu. Nikamuelewa tukabadilishana namba. Nikapanga siku nikutane naye sehemu tule, tunywe alafu tubadilishane mawazo. Cha ajabu akaja na rafiki yake. Walipofika tu, wanaanza kujilalamisha njaa. Nikawaambia agizeni mnachotaka. Nikajifanya nimepigiwa simu hivyo nahitaji kuongea na simu sehemu tulivu.

Sikugeuka nyuma na sijui ni nini kiliwakita wote wawili
 

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 

Me sikutaka kumuacha hivi hivi! Na wewe ulizingua!
 
Bado utajukuta umetumia gharama kubwa zaidi mkuu! Ni kuachana nao kiroho sana huku wakikutana huko walipo!
Ulichofanya ni cha maana sema na manzi nae ilibidi apate adhabu yake ili siku ingine asifanye huo upuuzi
 
Mkuu hata me yule manzi niliona hanifai nikatana nae mapema tu.
Yeah,mi nakuita labda kuna vitu vya msingi tukaongeee wewe unabeba nyomi la watu kama unaenda kufumania???sasa unaniletea nyomi la watu ili iweje?
 
Wengine wanafundishwa kwa vitendo,haya Mambo ya kubeba lundo la marafiki ni ya kipuuzi sana
 
Tabia ya wewe kuitwa wewe Kama wewe halafu wewe unakuja na kikundi wewe mahondaw unaona Ni nzuri .

Unaenda kukutana na mtu uliyenaye kwenye mahusiano halafu unabeba kikundi we unaona Ni njema .

Mwanamke alieitwa yeye kama yeye halafu akaja na kikundi huwa Ni mpuuzi tu dawa yake Ni waagize halafu unapotea kiana
 

Mkuu ndicho nilichofanya
 
Chama cha Wanaume Bahiri Tanzania (WaBaT) tunakuandia tuzo, mm kama mtunza hazina ngoja niwasiliane na Katibu tuone namna ya kukufikishia tuzo yako mkuu.
 
Hukufanya vizuri, bora ungemuweka wazi manzi ako mkaona namna ya kusema either kuna emegensi au laa!
Ni funzo kwao, sasa umeitwa peke yako unakuja na wapambe kibao....mtaongeaje mipango yenu sasa?
 
Kutokujielewa tu na ukiona unafanyiwa hivyo jua kabisa we mwanaume haupendwi unachunwa tu

Mwanaume unayempenda unaanzaje kumfanyia hivyo
πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… mbona povu mkuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…