DOKEZO Tabora: Wanafunzi wafukuzwa kwa kujirekodi picha za utupu na kuzisambaza

DOKEZO Tabora: Wanafunzi wafukuzwa kwa kujirekodi picha za utupu na kuzisambaza

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Utandawazi na athari zake.

Kifupi utandawazi umetukuta off-guard.

Bahati pia umezikuta familia nyingi kwenye umasikini mkubwa na kuwafanya walezi/wazazi kuwa busy kutafutia familia ugali na mwisho wa siku watoto wanakosa uangalizi.
Bora wewe unachambua tatizo. Na ndiyo maana serikali ya Awamu ya sita katika kukabiliana na umaskini imeendelea kuboresha mikopo nafuu na juzi tumepokea fedha kwa ajili ya kwenda kutoa mikopo ya Wafanyabiashara ndogo ndogo kupitia NMB mtu mmoja mmoja na siyo kikundi. Watoa komenti wengi unaona kabisa wanapitwa na taarifa nyingi ila wanatoa komenti kama vile labda wanafahamu mikakati yote. Na mikakati yenyewe tukitoa taarifa views hata mia hazifiki. 😀

Ila lete Sasa habari ya taharuki, nusu sasa Uzi wamesoma 1K
 
Wewe nani kakuambia Hawa hawatasoma tena? Mbona hata huko mahabusu za watoto wanasoma. Mbona mnapotosha ukweli kuwa ilibidi waondolewe pale wakarekebishwe tabia ndiyo waende tena kuanza shule? Mlitaka waachwe pale waharibu wote au?

Halafu mbona mimi nimekuta walishaondolewa shuleni kitambo? Au mnadhani mimi ndiyo jana nimewaondoa? Mbona chanzo cha taarifa nacho kimedanganya? Au nacho nikishtaki?
TUnahoji kulingana na taarifa kuwa wamefukuzwa mama
 
OK hongera

Je Mh umefikiria swala la kuajiri wanasaikolojia mashuleni ambao watahakikisha wanaweka sawa swala la malezi na Afya ya Akili ya wanafunzi!?


Kuna mambo mengi Sana yanayoendelea mashuleni nisingependa kuyaandika hapa .

Kwanini msifikirie kitu Kama hiki
Hoja yako nzuri sana ila vigumu kupata ajira zote hizo kwa wakati mmoja. Kumbuka, kama ni ajira nasi tunaomba wizara ya utumishi ambao huajiri kulingana na wage bill na mahitaji ya sekta zote. Hiyo zinazopatikana ndiyo hizo zinaenda. Na kumbuka, wizara haziajiri Bali ajira ziko halmashauri. Muwe mnakumbuka hili jambo. Hivyo, sisi ni watunga sera na miongozo ya kisera. Hivyo, kwa sasa ndiyo maana kuna madawati ya ulinzi wa watoto shuleni, waalimu nao wamesomea kozi za uangalizi wa watoto, wazazi nao nyumbani wanao wajibu na kwenye kata, Kijiji, mitaa kuna kamati za ulinzi wa watoto. Wote Hawa wakibaini tatizo wanapeleka rufaa kwa ustawi wa jamii. Ni kama afya tu kuwa, ukiona mgonjwa unampeleka wapi au taarifa unapeleka wapi? Je mbona mtoto akiugua nyumbani tunabaini, vipi akiwa na tabia mbaya tusibaini? Hatuwajibiki?
 
Bora wewe unachambua tatizo. Na ndiyo maana serikali ya Awamu ya sita katika kukabiliana na umaskini imeendelea kuboresha mikopo nafuu na juzi tumepokea fedha kwa ajili ya kwenda kutoa mikopo ya Wafanyabiashara ndogo ndogo kupitia NMB mtu mmoja mmoja na siyo kikundi. Watoa komenti wengi unaona kabisa wanapitwa na taarifa nyingi ila wanatoa komenti kama vile labda wanafahamu mikakati yote. Na mikakati yenyewe tukitoa taarifa views hata mia hazifiki. 😀

Ila lete Sasa habari ya taharuki, nusu sasa Uzi wamesoma 1K
Mkitaka mfanikiwe katika mambo yenu hakikisha mnatafuta watu makini wenye uwezo mzuri wa kufikiria Great thinkers .

Hamna wizara wala taasisi ya serikali inayofanya vuzuri

Umasikini mnashindwa kuuondoa kwakuwa hamna mikakati sahihi ya kuboresha Akili za watu.

Huwa nawaaambia hamtokaa mlete matokeo chanya Kama mtaendelea kuendesha nchi kisiasa.

Sisi hapa Jamiiforum tumewashauri hadi tumechoka.
 
TUnahoji kulingana na taarifa kuwa wamefukuzwa mama
Kuweni makini na taarifa sasa na pia, pendeni kujipa fursa ya Imani na kusema Waziri njoo tujibu kabla hatujaanza kupiga spana konki. Anyway, nilishawazoea wapendwa wangu, sina shaka mtakuja kunikumbuka na mimi sina shaka nitakuja kuwa miss, kitambo kidogo tu kipite😍😍😍
 
Mkitaka mfanikiwe katika mambo yenu hakikisha mnatafuta watu makini wenye uwezo mzuri wa kufikiria Great thinkers .

Hamna wizara wala taasisi ya serikali inayofanya vuzuri

Umasikini mnashindwa kuuondoa kwakuwa hamna mikakati sahihi ya kuboresha Akili za watu.

Huwa nawaaambia hamtokaa mlete matokeo chanya Kama mtaendelea kuendesha nchi kisiasa.

Sisi hapa Jamiiforum tumewashauri hadi tumechoka.
Lete ushauri huo tafadhali. Yuko mmoja alitoa ushauri critical kuhusu beach boys huko, na nilimpongeza na tulifanyia kazi. Ni gentamicin huyu. Ushauri ni jambo jema tu mbona, nani huyu anakataa ushauri, mbaya Sana kukataa ushauri
 
Hoja yako nzuri sana ila vigumu kupata ajira zote hizo kwa wakati mmoja. Kumbuka, kama ni ajira nasi tunaomba wizara ya utumishi ambao huajiri kulingana na wage bill na mahitaji ya sekta zote. Hiyo zinazopatikana ndiyo hizo zinaenda. Na kumbuka, wizara haziajiri Bali ajira ziko halmashauri. Muwe mnakumbuka hili jambo. Hivyo, sisi ni watunga sera na miongozo ya kisera. Hivyo, kwa sasa ndiyo maana kuna madawati ya ulinzi wa watoto shuleni, waalimu nao wamesomea kozi za uangalizi wa watoto, wazazi nao nyumbani wanao wajibu na kwenye kata, Kijiji, mitaa kuna kamati za ulinzi wa watoto. Wote Hawa wakibaini tatizo wanapeleka rufaa kwa ustawi wa jamii. Ni kama afya tu kuwa, ukiona mgonjwa unampeleka wapi au taarifa unapeleka wapi? Je mbona mtoto akiugua nyumbani tunabaini, vipi akiwa na tabia mbaya tusibaini? Hatuwajibiki?


Kuweni na vipaumbele serikali inabidi kujua wapi ifanyinke allocation kulingana na uhitaji .

Leo mnazalisha watoto ambao hawana maadili ndo hao wanaishia kucheza picha za ngono .


Mimi nimekaa katika sectors ya elimu naelewa Sana .
 
Lete ushauri huo tafadhali. Yuko mmoja alitoa ushauri critical kuhusu beach boys huko, na nilimpongeza na tulifanyia kazi. Ni gentamicin huyu. Ushauri ni jambo jema tu mbona, nani huyu anakataa ushauri, mbaya Sana kukataa ushauri


Naomba katika bajeti ya serikali 2025/2026

Muandae bajeti ya kuajiri wanasaikolojia mashuleni na kila shule wawepo wanasikolojia wawili wa kike na wa kiume .

Nategemea kupata mrejesho mzuri .

Mwalimu hana uwezo wa kufundisha na kudeal na malezi ya mtoto Kwa wakati mmoja .
 
Hiyo ni adhabu kubwa Kwa watoto
Tushajua ni watoto na walifanya utoto
Wawape adhabu hata ya viboko
Lakini wawape fursa ya kusoma tena
Mtu hubadillika, wanaweza kubadilika na kuwa wema

Sio hekima hiyo kumfukuza mtoto shule
Kwamba hawatapewa fursa ya kusoma tena, ni hoja za wazushi tu wenye chuki zao sijui dhidi ya nani. Kwa kuwa wako watoto kwenye mahabusu zetu tano nchini na kwenye makao ya watoto waliofanya mambo magumu kusimulia huwezi na wanaendelea na elimu baada ya tabia zao kurekebishwa kitaalamu. Haya mengine ni spana tu za watu na yao
 
Dunia ya sasa ni uamuzii wa mtoto kujitambua yani inasikitisha sanaa unawezaa mkaba mtoto na kumfunza unavyoweza ila akienda shule ndo huko anaharibikia, kwenye magari wanafunzi wana smart phone wanaperuzi muda wote yani hali ni mbayaa sanaa tena bora ujue kabisa mwanangu ana simu ucontrol matumizi yake lakini otherwise ni hatari sana kizazi kimepotoka mnoo wameona kuangalia pekee haitoshi sasa wanajirekodi
 
Kuweni na vipaumbele serikali inabidi kujua wapi ifanyinke allocation kulingana na uhitaji .

Leo mnazalisha watoto ambao hawana maadili ndo hao wanaishia kucheza picha za ngono .


Mimi nimekaa katika sectors ya elimu naelewa Sana .
Bunge la mwaka jana ulifuatilia kuhusu huu mjadala Hadi waziri wa utumishi akasimama?
 
Naomba katika bajeti ya serikali 2025/2026

Muandae bajeti ya kuajiri wanasaikolojia mashuleni na kila shule wawepo wanasikolojia wawili wa kike na wa kiume .

Nategemea kupata mrejesho mzuri .

Mwalimu hana uwezo wa kufundisha na kudeal na malezi ya mtoto Kwa wakati mmoja .
Ndiyo maana wakati ajira zikiendelea hao hao wataalamu huketi kutafakari na kuja na mifumo saidizi. Niambie sekta moja yenye watumishi wote asilimia Nia na isiyo na mifumo saidizi tafadhali, niambie ipi hiyo
 
Kuweni makini na taarifa sasa na pia, pendeni kujipa fursa ya Imani na kusema Waziri njoo tujibu kabla hatujaanza kupiga spana konki. Anyway, nilishawazoea wapendwa wangu, sina shaka mtakuja kunikumbuka na mimi sina shaka nitakuja kuwa miss, kitambo kidogo tu kipite😍😍😍
Baki nasi mamy...
Hiyo kauli ya Yesu kuwa bado kitambo kidogo nipo nanyi na bado kitambo hamtaniona hebu ifute...hadi ukamilishe kazi ya kujenga ustawi wa kamii yetu😍😍
 
OK hongera

Je Mh umefikiria swala la kuajiri wanasaikolojia mashuleni ambao watahakikisha wanaweka sawa swala la malezi na Afya ya Akili ya wanafunzi!?


Kuna mambo mengi Sana yanayoendelea mashuleni nisingependa kuyaandika hapa .

Kwanini msifikirie kitu Kama hiki
Hivi mpaka serikali ianze kuangaika na yote hayo nyinyi kama wazazi mnafanya kazi gani ya kuhakikisha watoto wenu wanakuwa na maadili yanayo faa?

Siku zote tabia za mtoto ndo huwa zina akisi ni aina gani ya wazazi alio nao.
 
Pale ambapo yule anayetakiwa kusaidia hajui cha kufanya.Kuwafukuza ni njia ya mkato ya kukwepa majukumu.Hawa ni Watoto na wanahitaji sana kupata msaada wa sisi tuliokomaa akili.Tatizo la hawa Binti zetu lipo Duniani kote,mpaka Mtu unajiuliza hawa Watoto hukutana na nini,isitoshe ni ujinga wanaofanya wengi wao tofauti ni kujirekodi tu.Juzi tu hapa tulikuwa tunashabikia kurudishwa shuleni kwa waliojifungua sasa hawa tunawafukuza kwamba wangekua salama kama wangepata mimba?Au huko waendako wapambane wapate mimba wajifungue ndio tuwarudishe darasani?
 
Nijuavyo na ndiyo ukweli, maadili siyo jambo linaloshughulikiwa na mtu mmoja au kikundi kimoja au aina moja ya watu. Maaduli ni suala mtambuka. Maadili ni jukumu la jamii nzima. Jamii yote ikishiriki kwa dhati katika kujenga na kudumisha maadili, jamii inaona waazi kabisa ustawi wa maadili. Zamani wakati tunakua, tulikuwa watoto wa jamii. Ukiwa mbali na wazazi yulikuwa tunaogopa kufanya ujinga kwa maana mtu mzima yeyote akikukuta anakupa nidhamu sawa kabisa kama utakayopewa na baba/mama yako. Halafu kila mtu mzima alikuwa anajiona ana wajibu wa kuhahihisha watoto wanakuwa na mwenendo wenye nidhamu. Lakini siku hizi mambo yako tofauti kabisa. Wazazi tuko bize kupita maelezo. Hata watoto walioko ndani mwetu tunashindwa kuwalea vyema. Mpaka wengine tuna outsource malezi kwa kuwapeleka boarding wayoto wachanga au kuwaachia watoto wasichana wa kazi. Muziki ni mzito. Maana madhara mengi sana, lakini lililo kubwa ni kuwa watoto wa sasa wengi hawatakuwa na mapenzi ya dhati kama ambayo sisi wa zamani tuliyo nayo kwa wazazi wetu. Sababu kubwa ni kuwa, hatuna muda na watoto kwa sasa, nao pia wakiwa wakubwa hawatakuwa na muda na sisi. Hapo talaka haija gusiwa. Ngoja niishie hapa. Lkn ukweli suala la maadili na malezi ni shiriikishi. Siyo la waziri pekee.
Muulize mipango wa waziri wako ni ipi kwenye kuiboresha na kuistawisha jamii?

Niliwhi kuuliza hapahapa JGF akanambia ndiyo wapo mbioni kuichambuwa ya zamani.

Unajuwa maana yake nini hiyo? Hana jipya, anabadili tarehe na majina ya ile iliyoshindwa.

Hana ubunifu na haambiliki? Au anaelewa anapoyapeleka maadili.
 
Back
Top Bottom