DOKEZO Tabora: Wanafunzi wafukuzwa kwa kujirekodi picha za utupu na kuzisambaza

DOKEZO Tabora: Wanafunzi wafukuzwa kwa kujirekodi picha za utupu na kuzisambaza

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kamii utaistawisha vipi wakati wizara yako haina mkakato wowote wa kuhakikisha watoto kuanzia wadogo mpaka wanakuwa watu wazima hawana viwanja vya michezo, sehemu na maeneo ya michezo?

Si wataishia kufanya mchezo wa baba na mama?

Waziri wa wizara ya ustawi wa jamii haelewi maana ya ustawi wa jamii.
 
Bora wewe unachambua tatizo. Na ndiyo maana serikali ya Awamu ya sita katika kukabiliana na umaskini imeendelea kuboresha mikopo nafuu na juzi tumepokea fedha kwa ajili ya kwenda kutoa mikopo ya Wafanyabiashara ndogo ndogo kupitia NMB mtu mmoja mmoja na siyo kikundi. Watoa komenti wengi unaona kabisa wanapitwa na taarifa nyingi ila wanatoa komenti kama vile labda wanafahamu mikakati yote. Na mikakati yenyewe tukitoa taarifa views hata mia hazifiki. 😀

Ila lete Sasa habari ya taharuki, nusu sasa Uzi wamesoma 1K

Ni jambo jema Mama kama mko na dhamira kweli ya dhati kuuondoa umasikini, iwe dhamira kweli na sio namna ya kutafuta kura na kushinda uchaguzi.

Kumaliza umasikini sio tu kutoa mikopo bali nakupunguza gharama za maisha pia, kuangalia maeneo yoote yanayopandisha gharama za maisha na kutafuta namna ya kudumu ili mwananchi apate unafuu.

Kuondoa umasikini ni pamoja na kuhakikisha watanzania wengi wanakwenda shule na kupata elimu bora itakayowawezesha kujiajiri na kuajirika ndani na nje ya mipaka yetu.

Kuondoa umasikini ni pamoja na kulinda ajira za wazawa na kuhakikisha wigo mpana wa uwekezaji unawekwa na serikali itengeneze fursa nyingi kwa watu wake Kwa kuboresha vichocheo vyote kama demokrasia, kodi rafiki, sera nzuri za uwekezaji, upatikanaji wa nishati ya uhakika na nafuu.

Kwenye kipengele cha elimu bora ndio tunawashape vijana kimaadili kuanzia shule ya msingi mpaka chuo kikuu lakini pia vichwa vyao vinakuwa smart na kutokuwa manipulated na utandawazi.

Tatizo la utandawazi lipo na litaendelea kuwepo, tunapaswa nasi kuongeza kasi kukabiliana nalo ili lisitudhidi na kuwa ndio maisha yetu, mwisho wake tunakuwa Taifa la kijinga ambalo linaweza kuchukuliwa mateka ndani ya ardhi yake.
Kwenye vikao vyenu vile Cabinet bila shaka Mama unapaswa kuhighlights hii ya mmomonyoko wa maadili ni red flag ambayo inaweza kupelekea Taifa kuanguka maana hatuna tena jamii serious zaidi ya wapenda mizaha na wafanya mizaha.

Asante
 
Suala la kuwa na viongozi incompentence nafikiri ni la muundo mzima wa kiungozi nchini. Embu tuachane na huyu waziri, je ni eneo lipi kama nchi tumeweza kulimudu efficiently kiasi kwamba dunia inaweza kujifunza kutoka kwetu?
kama hauna jamii yenye ustawi wa maana basi huko kwengine kote sahau.

Hii wizara ndiyo moyo wa raia, lakini naamini hata waziroi mwenyewe haelewi hilo.

Kwa mwendo unaoenda wizara hii, subirini kama hamkuona kesi za kina milembe na za kina anti J zinapelekwa ustawi wa jamii kutatuliwa.
 
Basi haina haja ya kuwa na wizara ya ustawi wa jamii, Ifutwe, au siyo?
Mwenye jukumu la kuhakikisha mtoto anakuwa na maadili ni mzazi ,hivi mzazi unamnunulia smartphone mtoto wa miaka 14 ili aifanyie nn ?
 
Pale ambapo yule anayetakiwa kusaidia hajui cha kufanya.Kuwafukuza ni njia ya mkato ya kukwepa majukumu.Hawa ni Watoto na wanahitaji sana kupata msaada wa sisi tuliokomaa akili.Tatizo la hawa Binti zetu lipo Duniani kote,mpaka Mtu unajiuliza hawa Watoto hukutana na nini,isitoshe ni ujinga wanaofanya wengi wao tofauti ni kujirekodi tu.Juzi tu hapa tulikuwa tunashabikia kurudishwa shuleni kwa waliojifungua sasa hawa tunawafukuza kwamba wangekua salama kama wangepata mimba?Au huko waendako wapambane wapate mimba wajifungue ndio tuwarudishe darasani?
Mbona tumeshasema wanaenda marekebisho ya tabia kisha warejee kwenye shule ingine? Mbona kama naandika kiswahili fasaha tu, shida Iko wapi. Mlitaka waachwe hapo ugonjwa uenee kwa watoto wote? Mnajua kuwa watoto hao wengine wasiofanya hayo nao Wana haki zao za kulindwa? Mbona hamuwasemei? Mnatakaje kwani. Hivyo ndiyo imekuwa sasa, wataenda marekebisho ya tabia kwanza na wengine watalindwa, na kokote kwingine tukiona mambo haya pia hatua za Sheria ya mtoto kupitia ustawi wa jamii zitachukuliwa tu. Ahsante kwa mchango wako.
 
kama hauna jamii yenye ustawi wa maana basi huko kwengine kote sahau.

Hii wizara ndiyo moyo wa raia, lakini naamini hata waziroi mwenyewe haelewi hilo.

Kwa mwendo unaoenda wizara hii, subirini kama hamkuona kesi za kina milembe na za kina anti J zinapelekwa ustawi wa jamii kutatuliwa.
Kwa hatua tuliyopo ni ustawi wa jamii unatakiwa kuwa imara tupate viongozi wazuri au tunatakiwa kuwa na viongozi wazuri ndio waweke misingi ya ustawi wa jamii imara?
 
Mwenye jukumu la kuhakikisha mtoto anakuwa na maadili ni mzazi ,hivi mzazi unamnunulia smartphone mtoto wa miaka 14 ili aifanyie nn ?
Basi haina haja ya kuwa na wizara ya ustawi wa jamii, Ifutwe, au siyo?
 
Mwenye jukumu la kuhakikisha mtoto anakuwa na maadili ni mzazi ,hivi mzazi unamnunulia smartphone mtoto wa miaka 14 ili aifanyie nn ?

Wao wazazi na Walezi hawana makosa. Makosa yako serikalini tu.

Na ukiangalia, uovu mwingi unaenda sambamba na kuanguka kwa Imani ya Mungu ambalo ni jukumu la msingi la wazazi. Hofu ya Mungu ikiishaisha huku duniani, maovu yote hustawi na kumea. Sijui kama hili nalo tunalikumbuka kama ni jukumu la wazazi katika malezi na makuzi ya watoto.
 
Basi haina haja ya kuwa na wizara ya ustawi wa jamii, Ifutwe, au siyo?
Wizara hii ina kazi zingine nyingi siyo hili tu. Sasa sijui ikifutwa, sijui nani atatekeleza mengine kwa mujibu wa hati idhini yake ya kuanzisha wizara hii. Halafu nimegundua watu hawajui hii wizara wanadhani kazi yake ni hii tu. Tusome hati idhini na hotuba za bajeti bungeni mzijue idara zake sita na majukumu yake
 
Shenzi kabisa hilo ndio onyo sahihi kwao .hao ukiwabakisha wata waaribu wengine
Mmhh usiseme hivyo kuteleza kupo, pengine wamelishana ujinga tu na kufanya waliyofanya. Mtt kusoma ni haki yake ya msingi.
Kuwafukuza shule pia wakabaki mtaani wanaweza pia kuharibu jamii ya sehemu wanakoishi.
Mkuu watt wetu wanafanya mengi sisi wazazi hatuyajui, hakuna alo salama.
Na ukute kuna chanzo pia cha wao kufanya hivyo, kitafutwe. Unaweza kuta leo wamekamatwa wao kumbe humohumo shuleni mambo maovu yanaendelea
 
Wao wazazi na Walezi hawana makosa. Makosa yako serikalini tu.

Na ukiangalia, uovu mwingi unaenda sambamba na kuanguka kwa Imani ya Mungu ambalo ni jukumu la msingi la wazazi. Hofu ya Mungu ikiishaisha huku duniani, maovu yote hustawi na kumea. Sijui kama hili nalo tunalikumbuka kama ni jukumu la wazazi katika malezi na makuzi ya watoto.
Waziri kwa sasasa ulitakiwa uwe juu ya kutafuta "mchawi nani" kwa kuwa na mipango na utelezaji bora wa hiyo mipango. Siyo kungoja moto uwake ndiyo ukazime.
 
Ulijuwaje kama ni wazazi au mabazazi ndiyo wamewanunulia?
Jukumu la mzazi ni kumlinda mtoto kujiepusha na hayo yote. Na hayo yanafanyika kwenye umri wa miaka Hadi nane ya awali, ubongo unapokuwa Hadi 90%. Sasa kama hatufanyi hayo kipindi hicho, ni kazi Sana huku mbele akiondoka mikononi mwako akaenda duniani huko ikiwemo mashuleni nk
 
Back
Top Bottom