Tafakuri ya FaizaFoxy 7: Shule za kusomea ujinga. Tanzania na propaganda za Udini Shuleni

Tafakuri ya FaizaFoxy 7: Shule za kusomea ujinga. Tanzania na propaganda za Udini Shuleni

Tatizo hawa ndugu zetu wanawachukulia waarabu wote kama Maswaaba katika umma wao ,waarabu hawafanyi makosa amini usiamin waarabu na wazungu wametutenda uovu sana and we will chant them down kwa muda mrefu sana
 
Kilatha,
Ali Aziz ikiwa unamkusudia huyu ambae alikuwa Immigration tukifahamiana lakini jina la mke wake silijui.

Mama yake Ali Aziz sisi tukimwita Mama Ali nikimfahamu pia akiishi Ilala.

Akina Kingui nawafahamu pia na Adam Kingui tumesoma sote St. Joseph's na tumekua pamoja Kipata Gerezani.

Dully Sykes ni mtoto wa Ebby Sykes na mimi na Ebby tumekuwa pamoja toka utoto wetu na anampata Dully mimi najua na nikimjua mama yake kutoka ukoo wa Aziz Ali.

Dully kwangu ni mtoto.

Mimi na Ebby Sykes babu zetu, bibi zetu na mama zetu walikuwa majirani toka miaka ya 1920s sisi hatujazaliwa.

Nimefurahi kuwa wewe ni mmoja wa koo hizi ambazo nami zimenihusu lau kwa mbali.

Nimehifadhi kumbukumbu nyingi za koo hizi na ningependa sana kujifunza zaidi kutoka kwako.

Mimi nimezaliwa Kipata 1952 mtaa ambao amezaliwa Hamza Aziz.

Namzunguzia Aziz Ali aliekuwa police commissioner.

Well mama yake Dully Sykes uhusiano wake na Aziz Ali; bibi yake Dully Sykes mzaa mama ukoo wa Aziz Ali.

Marehemu Adam Kingui ni mjomba wangu kwa wanaonijua kwa jina they can see why ........ndio maana nikamuuliza huyu bibi wa kiarabu anaijua kweli Kariakoo, Gerezani na Ilala, ama anaropoka tu.

Anyway wacha nikuwache maalim tatizo huyu FaizaFoxy kuna wasaa anakera kama hii mada yake ya kukataa facts za historia ya utumwa na kutaka kujifanya mswahili kushinda waswahili wenyewe wakati kaamia mtaa wa Mdoe miaka ya sabini tu.
 
Unaonesha ujinga uliosomeshwa umekujaa tele. Hata kuitazama video hujaitazama umeshapata majibu.

Hakuna Profesa wa "kidini" hapo, sema kweli tu, ujinga uliojazwa unashindwa kutumia neno Wakiislam, ndiyo hayo hayo yanayoongelewa kwenye hiyo video.
Tuache kwanza, tupo na kazi ya mama, katutuma tunamtafutia wakunaji mahiri.
 
Waarabu walikuwa wafanyabiashara wakubwa wa biashara ya utumwa na ujangili wa wanyamapori.
Hiyo historia itabaki hivyo, penda usipende.
Sio walikuwa ni mpaka sasa waarabu wengi ndo biashara zao,na ndo maana ni rahisi kumkuta mwarabu anaishi vijijini kabisa lakini hakosi gobore nyumbani kwake.maisha mazuri lakini utamsikia anasema ami wake kutoka oman anawapa misaada.
 
Mbona unajitetea sana lakini mada iliyopo hujaijadili.

Kama mumemo kashindwa kukupa hata kifurushi ujifaraguwe kwa raha zako, tatizo liwe langu? Au huna mume?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
[emoji23][emoji3][emoji23][emoji23][emoji3][emoji23][emoji3] bibi ana mipasho huyu khaaaah.
 
Waarabu walikuwa wafanyabiashara wakubwa wa biashara ya utumwa na ujangili wa wanyamapori.
Hiyo historia itabaki hivyo, penda usipende.
Kule Angola na Msumbiji Wamisionari wa Katoliki wa Kireno ndio waliokuwa wakiongoza operesheni kamata watumwa na kuwasafirisha kupitia Bahari ya Atlantic katika kile kilichoitwa Trans Atlantic Slave Trade. Ilifikia mahali Malkia Nzinga Mbandi wa Angola akaanzisha vita dhidi ya Wareno ili kuwahami watu wake. Kwa miaka 400 Waafrika wameuzwa utumwani na Wazungu lakini huwezi kusikia hata humu watu wakiwatuhumu Wazungu kwa utumwa na hii ni ishara ya udini pia.
 
Waarabu walikuwa wafanyabiashara wakubwa wa biashara ya utumwa na ujangili wa wanyamapori.
Hiyo historia itabaki hivyo, penda usipende.
Utumwa ulitamalaki bara Ulaya na America, ushaidi upo hadi leo ndio maana tunawaona Mike Tyson na wengine.
 
Namzunguzia Aziz Ali aliekuwa police commissioner.

Well mama yake Dully Sykes uhusianp wake na Aziz Ali; bibi yake Dully Sykes mzaa mama ukoo wa Aziz Ali.

Marehemu Adam Kingui ni mjomba wangu kwa wanaonijua kwa jina they can see why ........ndio maana nikamuuliza huyu bibi wa kiarabu anaijua kweli Kariakoo, Gerezani na Ilala, ama anaropoka tu.

Anyway wacha nikuwache maalim tatizo huyu FaizaFoxy kuna wasaa anakera kama hii mada yake ya kukataa facts za historia ya utumwa na kutaka kujifanya mswahili kushinda waswahili wenyewe.
Kilatha,
Nadhani unamkusudia Hamza Aziz aliyekuwa Inspector General of Police (IGP).

Screenshot_20220505-101157_Photos.jpg
 
Nimeisoma na kuielewa sana! Inasikitisha,Ila humu kuna wahusika na Vibaraka wao Hawatakuelewa maana wana malengo yao....
Wacha tuendelee kupelekana tu,Nyama tutazikuta chini.
Ahsante miss ingawa humu wanakuita Bibi sina uhakika na hilo.
 
Wazungu hawafichi na wanakiri wazi na wanatufundisha kuwa walifanya biashara haramu ya utumwa duniani na hasa barani Afrika
Tupe story yake, usifikiri kila mtu anakielewa ulichojazwa nacho wewe ujinga na ndiyo maana nimeweka video hapa ili tusiendelee kujaana ujinga.

Historia yote uliyosomeshwa shule ni uongo mtupu, juu chini, chini juu. Hivi upewe elimu na Mwingereza, mzungu, halafu yeye ajiponde? Fikiri japo kiduchu.
 
Faiza naona umekuja na hii video ili kujiridhisha na kile ulichokileta ukitaka kuwaaminisha watu kwamba walichojua mwanzo ulikuwa ni uongo.

Lakini ukipewa mifano mingine nje ya hiyo video yako unakuwa mgumu kukubali, mfano kina Tippu Tipu na picha zinazowaonesha waliovaa kanzu na barakashia wakiwa na watumwa.

Kama hao watu kina Tippu Tipu sanamu zao ziko makumbusho Zanzibar kwanini unakuwa mgumu kuamini walihusika na biashara ya utumwa? Zanzibar ina utamaduni wa kiislamu, unataka kusema wale waislamu wenzako nao hawakuwa wakweli?

Usilazimishe kubadili nyeupe iwe nyeusi, wewe pekee na video yako hauwezi kuubadili ukweli huu, hapa unacholeta ni ubishi tu, kubali hata baadhi ya waislamu kama walivyo wakristu walikuwa na mabaya yao.
 
nimeangalia hii video lakini niwe muwazi huyu profesa yupo biased sana, ndio anakiri kuwa watu wote wa pwani ya Afrika Mashariki walihusika na biashara ya utumwa (wabantu, washirazi, waswahili, waarabu n.k) ila anasisitiza kuwa waliohusika zaidi ni wazungu na wabara!! (angalia dakika ya 9:01 mpaka 9:13). Ni ngumu sana kuacha kuihusanisha biashara ya utumwa na uislamu kwani hata huko arabuni ambako misingi ya dini hii iliwekwa ilikuwa ikifanyika lakini hilo sio jambo ambalo linaleta mantiki kwani hakuna msikiti uliokuwa unafanya biashara hiyo bali baadhi ya watu wenye imani hiyo hivyo kwangu sio sawa.

ila ukweli uwe wazi waarabu walifanya shughuli hiyo sana Zanzibar na Bara na hakuna mbantu ambae alisafirisha watumwa kutoka bara au alimiliki jahazi la kwenda arabuni kupeleka watumwa, bali waarabu ndio walikuja kukamata na kuwanunua, na hao ndio walimiliki mashamba ya karafuu pemba na unguja na kuwatumikisha waafrika.
 
Profesa Ibrahim amekiri kuwa Waarabu walihusika na biashara ya Utumwa ila anadai ni kwa kiwango kidogo Kuliko wazungu

Amedai kuwa Arabuni Ni jangwa na hakuna shughuli za kilimo hivyo isingeliwezakana kupeleka watumwa wengi huko

Amekiri kuwa waliohusika kuchukua watumwa Ni masheikh ambao waliwatumia watumwa hao kwa kazi za kuwatengea kahawa

Kwa ufupi "Profesa" wetu anashida na michoro au picha tunazoonyeshwa kwa madai zinapotosha japo anakiri Mwarabu alifanya biashara ya Utumwa
 
Utumwa umetajwa hata kwenye Biblia

Mwanzo: 21:10

Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka
 
Back
Top Bottom