Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
PoleDawa ni kusomea uhasibu au kodi kwa gharama yoyote . Utumishi ajira za tra zinatangazwa kila baada ya muda mfupi na wala hazina ugumu.
Sema maskini wengi waoga hukimbilia ualimu na udaktari ili wakashike maiti.
Hata mashamba ya ukoo uza jisomeshe au somesha mtoto
Huyo jamaa sijui anabwabwaja nini, udaktari haukimbiliwi hakuna kilaza anapeleka pua kule hata awe mtoto wa tajiri namna gani.Pole
Labda ana investment zake mbali na mshahara😂😂 au ndo kama kawaida kila mmoja ale KWA urefu wake mkuuAfisa wa TRA ana mshahara shingapi?
Huyo bwanamdogo mshahara wake ni kiasi gani, tanzie hapo.View attachment 2630959View attachment 2630960
Afisa wa Mamlaka ya Mapato ya Tanzania (TRA), Boniventure Pascal Madia (pichani), maarufu kama Boni amezua taharuki kubwa kwa wakazi wa Mbezi Juu kwa kujenga jengo la ghorofa 4 bila kibali cha Manispaa na bila kufuata viwango vya kitaalamu vya ujenzi na kutishia maisha ya wakazi hao kwa hofu ya jengo hilo kuanguka siku zijazo.
Wakazi wa Mbezi Juu/Goba bado wana kumbukumbu ya kuanguka kwa gorofa eneo la Goba kwa Awadhi mwaka 2021 na kuuwa watu wanne na sasa wanahofia maafa mengine kwenye Mtaa wa Nia Njema eneo la Mbezi Juu kwa Sanya.
Hofu ya wakazi wa eneo hilo ni kuwa afisa huyo wa TRA anajenga magorofa hayo chini ya viwango kwa kutumia nondo zenye milimita ndogo na mafundi wa mtaani bila kibali cha ujenzi cha manispaa.
Wakazi wa Mbezi Juu wanasema Boni alinunua nyumba ya chini iliyojengwa kwa msingi hafifu halafu akaigeuza kuwa jengo la gorofa 4 kwa kupandisha gorofa juu, huku akitumia mafundi wa mtaani, bila kibali cha ujenzi na bila kujenga msingi madhubuti unaoweza kujenga jengo la gorofa 4.
Hofu kubwa ya wakazi hao ni kuwa jengo hilo la gorofa linaloendelea kujengwa chini ya viwango huenda litadondoka siku zijazo na kuuwa watu kwenye eneo hilo.
Kila siku, wakazi hao wanapigwa na butwaa kuona afisa huyo wa TRA akiongeza gorofa kupanda juu kwenye jengo hilo, huku wakijua kuwa limejengwa kwenye msingi hafifu wa nyumba ya chini.
Viongozi wa serikali ya mtaa wa Mbezi Juu Kwa Sanya na Mtaa wa Nia Njema wameshindwa kuchukua hatua yoyote kuepusha maafa hayo na wanaachia gorofa hilo liendelee kujengwa bila kibali na chini ya viwango na kuhatarisha maisha ya wananchi.
Bongo nyongo sanaWivu tu unakusumbua.
Ukiona ghorofa imesimama hadi hapo jua ana kibali tayari vinginevyo ungeshakuta Alama nyekundu.
SawasawaHuu ugomvi wa wafanya biashara na TRA naona ndio kwanza bado mpyaa........☺
Basi comments ziwe fupifupi ili kuokoa muda..😊
Watu wanachomaa..Bongo nyongo sana
Sijui case ya huyu ila kuna mikopo ya ujenzi bank kutokana na mshahara wako.....unalipa taratibu up to 15 years....Kwamba yeye kwao ni masikini?
Wewe inakuhusu nini kipato chake! Mbona wewe muda wote unapoteza kwenye mitandao wakati wenzio wanapiga kazi! Kenge weweAfisa wa TRA ana mshahara shingapi?
Wamechomaa..Huyo bwanamdogo mshahara wake ni kiasi gani, tanzie hapo.
Inawezekana pia..Halafu ukute jamaa alienzisha huu uzi anakunywa na mshkaji kila weekend, akiwa na shida anaenda kwa jamaa kuomba msaada na kumsifia kila kukicha wakiwa wote. Na hata wakienda site anampamba kuwa kajenga mziga wa mjengo mtaani watamkoma. Kumbe moyoni anaungua.
Binadamu ni wanafiki sana.