DOKEZO TAHADHARI: Afisa TRA ahatarisha maisha ya wakazi Mbezi Juu Kwa Sanya kwa kujenga ghorofa 4 bila kibali, kwenye msingi dhaifu wa nyumba ya chini

DOKEZO TAHADHARI: Afisa TRA ahatarisha maisha ya wakazi Mbezi Juu Kwa Sanya kwa kujenga ghorofa 4 bila kibali, kwenye msingi dhaifu wa nyumba ya chini

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
View attachment 2630959View attachment 2630960


Afisa wa Mamlaka ya Mapato ya Tanzania (TRA), Boniventure Pascal Madia (pichani), maarufu kama Boni amezua taharuki kubwa kwa wakazi wa Mbezi Juu kwa kujenga jengo la ghorofa 4 bila kibali cha Manispaa na bila kufuata viwango vya kitaalamu vya ujenzi na kutishia maisha ya wakazi hao kwa hofu ya jengo hilo kuanguka siku zijazo.

Wakazi wa Mbezi Juu/Goba bado wana kumbukumbu ya kuanguka kwa gorofa eneo la Goba kwa Awadhi mwaka 2021 na kuuwa watu wanne na sasa wanahofia maafa mengine kwenye Mtaa wa Nia Njema eneo la Mbezi Juu kwa Sanya.

Hofu ya wakazi wa eneo hilo ni kuwa afisa huyo wa TRA anajenga magorofa hayo chini ya viwango kwa kutumia nondo zenye milimita ndogo na mafundi wa mtaani bila kibali cha ujenzi cha manispaa.

Wakazi wa Mbezi Juu wanasema Boni alinunua nyumba ya chini iliyojengwa kwa msingi hafifu halafu akaigeuza kuwa jengo la gorofa 4 kwa kupandisha gorofa juu, huku akitumia mafundi wa mtaani, bila kibali cha ujenzi na bila kujenga msingi madhubuti unaoweza kujenga jengo la gorofa 4.

Hofu kubwa ya wakazi hao ni kuwa jengo hilo la gorofa linaloendelea kujengwa chini ya viwango huenda litadondoka siku zijazo na kuuwa watu kwenye eneo hilo.

Kila siku, wakazi hao wanapigwa na butwaa kuona afisa huyo wa TRA akiongeza gorofa kupanda juu kwenye jengo hilo, huku wakijua kuwa limejengwa kwenye msingi hafifu wa nyumba ya chini.

Viongozi wa serikali ya mtaa wa Mbezi Juu Kwa Sanya na Mtaa wa Nia Njema wameshindwa kuchukua hatua yoyote kuepusha maafa hayo na wanaachia gorofa hilo liendelee kujengwa bila kibali na chini ya viwango na kuhatarisha maisha ya wananchi.
Sasa huyu ndio aje kuchukua kodi utajua hujui na anaujenzi huo..
Anakufilisi kabisa huyu.
 
Nchi hii Ukiwa Mtumishi wa Umma usipoiba unazomewa ukiiba unapongezwa kwasababu ni ngumu Sana kuendesha kesi dhidi ya MAFISADI na wabadhilifu wanatumia technicalities za kisheria kulinda uovu wao na kuwaambukiza WATOA MAAMUZI utajiri na kuwatoa kwenye mstari.
Ni vigumu pia katika mazingira ya Haki za Binadamu na Demokrasia kupambana na Aina ya MAFISADI WALIOPO Afrika.
 
Wivu tu unakusumbua.
Ukiona ghorofa imesimama hadi hapo jua ana kibali tayari vinginevyo ungeshakuta Alama nyekundu.
Kuna afisa mmoja wa TRA alikuwa anatudai kodi miaka kadhaa iliyopita. Baada ya majadiliano ya muda mrefu, wakaja na options zao kama kawaida. Hii ya Kaizari na hii ya kwetu. Tukalipa ya Kaizeri. Pressure ikawa juu lazima wao walipwe Chao.
Bila kujua, kuna group lingine wadau wanalima pamoja. Ikaja issue ya kulipia ardhi. Jamaa anatoa ahadi zake ila bado kuna mdeni wake hajalipa.
Ni hivi sio wivu kama kila kitu ni halali. Mtu anafunga biashara ya mtu mwingine kwa dhuluma ili atusue kimaisha.
Ndio haya mambo ya kujenga vitu visivyoeleweka uchochoroni, wakidhani wamejificha
 
Wivu tu unakusumbua.
Ukiona ghorofa imesimama hadi hapo jua ana kibali tayari vinginevyo ungeshakuta Alama nyekundu.
huyu dogo km ni kweli ni naona hana akili. vilevile nchi hii isipotungwa sheria km za China kuwa huyu ikithibitika ni kweli adhabu yake ni kunyongwa na mali inataifishwa hakuna adhabu inayoweza kuwafaa zaidi ya hiyo. Sasa km hili dogo tu linajenga ghorofa, wakubwa zake je, na wako wangapi. Sasa mchwa km hawa watatosheka kwa uchumi upi. Na huyu mpaka kustaafu kwake atakuwa amejenga maghorofa mangapi.

Ikishindikana sheri za kunyongwa basi afilisiwe mali zake zote na afukuzwe kazi mara moja aende kutumikia kifungo cha maisha jela km tuko serious kweli. Kuwafilisi na kuwapeleka jela maisha kutawakatisha tamaa kujikusanyia mali nyingi za uwizi. Shida nani atamfunga majaji wenyewe wanakula rushwa balaa.
 
Ikishindikana sheri za kunyongwa basi afilisiwe mali zake zote na afukuzwe kazi mara moja aende kutumikia kifungo cha maisha jela km tuko serious kweli. Kuwafilisi na kuwapeleka jela maisha kutawakatisha tamaa kujikusanyia mali nyingi za uwizi. Shida nani atamfunga majaji wenyewe wanakula rushwa balaa.
kama ripoti ya CAG ilianikwa uwanjani kweupe, na wezi wakajulikana maramoja
lakini C-in-C kahitimisha kwa kusema "hizo pesa mlizochukua hamtazikwa nazo"
wewe unategemea nini hapo ?
 
Nchi hii Ukiwa Mtumishi wa Umma usipoiba unazomewa ukiiba unapongezwa kwasababu ni ngumu Sana kuendesha kesi dhidi ya MAFISADI na wabadhilifu wanatumia technicalities za kisheria kulinda uovu wao na kuwaambukiza WATOA MAAMUZI utajiri na kuwatoa kwenye mstari.
Ni vigumu pia katika mazingira ya Haki za Binadamu na Demokrasia kupambana na Aina ya MAFISADI WALIOPO Afrika.
Uko sawa.
Kupambana na mafisadi wa Afrika ni ngumu..
 
Issue hapa sio gorofa kujengwa mtaani ila aliyejenga ni afisa tra alafu, ni hivi tu watu wanalalamika kuhusu rushwa iliyo kithiri kutoka kwa baadhi ya maofisa Wa tra wakitumia mwanya Wa sheria mbaya za kodi kujinemeesha Wao binafsi na kuharibu mitaji na future za watu.
Hoja ya mwandishi ni udhaifu wa kazi hajagusia kipato cha Boni ila mijadala imehama. Nafikiri hoja zake zinalenga kuepusha vifo ambavyo vinaweza kuathiri sisi wana jf au ndugu na marafiki. Kikubwa serikali ifuatilie.
 
Back
Top Bottom