Pre GE2025 Tamaa ya Tundu Antipas Lissu, Kuutaka uwenyekiti wa CHADEMA taifa ni utashi wake binafsi au shinikizo kutoka nje ya nchi kwa wanao mbackup!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Sifa ya kiumbe hai chochote ni kukua, kuongezeka na kujongea Na mwisho ni kiachia ngazi. Ndio maana hata kwenye maisha halisi, tunazaliwa, tunaongezeka, tunakuwa vijana Na mwisho ni kifo.

Hivyohivyo Na maisha ya kisiasa ndivyo yalivyo
 
unamanisha mbowe aendelee azima yake bado(20 yrs of )
angeweza kumuachia mwingine lakini sio kwa namna ambavyo wanaotaka nafasi hiyo wanavyojipambanua na kumzodoa hadharani kwa fedhaha na dhihaka namna ile..

Infact,
uchaguzi wa ngazi za juu Chadema unaweza kuahirishwa hadi baada ya uchaguzi mkuu October 2025πŸ’
 
Sifa ya kiumbe hai chochote ni kukua, kuongezeka na kujongea Na mwisho ni kiachia ngazi. Ndio maana hata kwenye maisha halisi, tunazaliwa, tunaongezeka, tunakuwa vijana Na mwisho ni kifo.

Hivyohivyo Na maisha ya kisiasa ndivyo yalivyo
kama ukuaji uko hivyo, basi ukuaji wa siasa za Tundu Lisu ni wa mwendokasi dah!

Jioni anautaka umakamu mwenyekiti, asubuh anautaka uenyekiti kamili wa chama dah 🀣
 
kama ukuaji uko hivyo, basi ukuaji wa siasa za Tundu Lisu ni wa mwendokasi dah!

Jioni anautaka umakamu mwenyekiti, asubuh anautaka uenyekiti kamili wa chama dah 🀣
Unafahamu nini kuhusu uyoga na mwanzi?
 
Tunakuja na Lissu!
Dume linalotembea na risasi mwilini,he has nothing to loose, siasa nyepesi hazitaipeleka hii nchi mahali!
ndivyo Lisu anavyomkoromea chairman Mbowe hivyo sio gentleman?

48 laws of power ya Robert Greene itamuhukumu.
Time Will tell.

The second Augustine Lyatonga Mrema is around the corner πŸ’
 
Mwaka huu mpaka uteme nyongo! Lissu amewashika makende na bado hujasema!
 
Wewe huna hoja na ramli zako zisizo na maana, Chadema hamna shida yoyote Mbowe yuko tayari kuachia uwenyekiti lakini kwa mtu anayejitambua ambaye hataweza kupelekwa mnadani na ccm yenu iliyochosha watu.

Sisi tunachotaka ni kuona ccm ikiondoka na kama hawawezi kuondoka kupitia makaratasi wanayodharau basi hata kwa coup d'etat lakini ili mradi tu waondoke.

We're deeply tired of this repressive regime that has no interests of this country at heart.
 
una mambo mengi moyoni kama Lisu tu dhidi ya uenyekiti wa chairman Mbowe Chadema..

hata hivyo,
makasiriko na muhemko ni nonsense.

kuichoka CCM ni uvivu wako binafsi tu, na huenda ndio sababu ya umaskini wa fikra ulionao, et coup d'etat!🀣
 
Tundu lissu anaumisha watu vichwa sana hata wasiompenda kila siku wanamuota.
 
Nje ya mada kidogo....
Lissu ni haki yake ya msingi na kikatiba kugombea nafasi yoyote aitakayo ndani ya chama, pia Mbowe ni haki yake ya msingi na kikatiba kugombea nafasi yoyote aitakayo ndani ya chama.

Jambo linaloshangaza hasa kwa wafuatao wa CHADEMA katika mitandao ya kijamii ni kutaka Mbowe asigombee amuachie Lissu. Kwanini wasiwapigie kura wote na wengineo watakaojitokeza ili apatikane mshindi halali? Je, Mbowe katiba ya CHADEMA haimruhusu kugombea awamu nyingine?
 
Tundu lissu anaumisha watu vichwa sana hata wasiompenda kila siku wanamuota.
wabobevu Lazima tuzungumze na kueleza kwa kina mambo haya kinagaubaga, itakua haina maana kukaa kimya na utaalamu wako kwenye mambo haya badala ya kueleza kwa faida ya wadau πŸ’
 
uko ndani ya mada gentleman na umepiga utosini kabisa tena bila kuegemea upande wowote baina ya mafahali hawa wawili ndani ya chadema.

Ni muhimu ubabe wao ukaamuliwa kwenye sanduku la kura bila masharti yoyote πŸ’
 

Kwani nani ndani ya CCM ambaye moyo wake hauko huko Magharibi
 
Mbowe hajali hayo mambo ya credibility, ingekuwa hivyo kina Kitila Mkumbo, Zitto Kabwe, Dr Slaa, etc wote bado wangekuwa CHADEMA.

Kwa Mbowe CDM ni mfereji (sio mrija) wa kipato cha uhakika, kumbuka kuna kipindi wabunge wa CDM walikuwa wanachangia ela kila mwezi kwenye moshahara yao, ila mwisho wa siku ela zinarudi kwa Mbowe na team yake.

Wengi humo ndani washamchoka, angalia matendo ya John Mnyika, Godbless Lema, John Mrema, Mwita, etc wote ni kama wamejitenga na chama ila bado wapo chamami.

Zitto alijaribu fanya mabadiriko CHADEMA ila akaangukia pua, hawa wa sasa wakiangukia pua jua CHADEMA ipo vipande viwili.
 
Na ile ya fomu moja kule ina shinikizo kutoka nje?
 

Kama uliwahi kusikia kuna uwendawazimu, basi ni kama huu uliouandika.

Isije siku nyingine ukasema kuwa na Rais Samia anagombea Urais kutokana na shinikizo kutoka mataifa mbalimbali anayoyatembelea, chawa wake watakuteka na hatutakuona tena.

Hata kama una akili kidogo, jitahidi utumie vizuri akili ndogo uliyopewa kuliko kila wakati kuandika vitu vya kijinga kama unavyofanya.

Mwenzio Mwashambwa siku hizi kajirudi kidogo, haandiki upuuzi wa kufikia kiwango chako.
 
Mbowe awajibike tu.

Kama Mwenyekiti ameshindwa kukipeleka chama to the promised land(Magogoni)

Wameshindwa Uchaguzi huu mdogo uliopita.

...na mengine mengi tu.

Awajibike. Ajing'oe kwenye kinyang'anyiro cha Uenyekiti wa CHADEMA na abakie kuwa Mshauri/Caretaker tu

Hatahivyo,

Tundu Lissu nae awaachie wengine-Atakilipua chama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…