Hapo mimi naona vumbi tu kama si matope. Haiwezekani kuufuata mwongozo wa TAMISEMI halafu tukategemea kupata matokeo. Kuna somo mfano BIOLOGY, huwezi kufundisha mada kwa kuzingatia mpangilio wa mada za muhtasari, kwa sababu kuna baadhi ya mada ambazo mwalimu hutakiwa kuzifundisha kwa kuzingatia majira ya mwaka mfano masika, vuli au kiangazi ili kuongeza ufanisi wa somo kwa sababu ya upatikanaji wa zana halisi za ufundishaji na ujifunzaji. Mfano mada inayohusiana na maua haiwezi kufundishwa mwezi wa saba sababu wakati huo mimea mingi huwa imekauka kutokana na kiangazi. Hivyo mwalimu huirejesha nyuma mada hiyo hadi mwezi wa pili au wa tatu ili kurahisisha upatikanaji wa zana halisi mfano maua ambapo mwalimu hutakiwa kuwatoa nje wanafunzi na kuwapeleka katika mazingira yanayoizunguka shule na kujionea maua halisi, kuyagusa au hata kunusa na hivyo kuwajengea kumbukumbu ya muda mrefu juu ya somo husika. Huu mchezo wa wataalamu kujifungia ofisini na kutunga muongozo huu usiotekelezeka, utaua ama kudhoofisha elimu yetu.inabidi tuchukue hatua kali kabisa kama wadau wa elimu
Lengo ni nini?Nakuunga mkono ndugu mleta mada,semina hizi,jana zimefanyika hapa tanga, kesho Kuna mtu kanidokeza wilaya ya mkuranga,kwa kweli huwezi kumpangia mtu mpango kazi,wakati kazi anafanya yeye na hujui katika utendaji wake anakumbana na matatizo gani,hapa tamisemi wanakwenda kuua elimu jumla.tuhifadhi bandiko hili wakati mitihani itakapofanyika na matokeo kutoka ndiyo tutabaini ukweli.
Shule nyingi Zina upungufu wa walimu kwa hiyo kuwa sawa katika ufundishaji ni kitu kisichowezekana kabisa,kila eneo Lina changamoto zake.
Ajabu mpaka mitihani yote qamwpanga ifanyike wakati mmoja,ya mid term, terminal,na annual kwa Tanzania Zina. Kitu ambacho ni kigumu kutekelezeka.chukua mfano mwlimu z Ana matatizo ya kiafya,hajafika kazini siku tatu,kw hiyo atakapo Rudi atalazimika kwenda spidi ili kuwa sawia na azimio lake la kazi.
Unge-share na huo mwongozo.Habari wanajukwaa,
Mimi nimekuwa mhanga kwelikweli wa elimu yetu hii ya tanzania hasa huku chini.
Juzi TAMISEMI wametoa mwongozo mpya ambao unatakiwa kutumia kufundishia kuanzia darasa la kwanza mpakakidato cha 6, ambapo kila mwalimu anatakiwa kuandaa kalenda la kufundisha na kwamba wanatak kuweka equality kwa wnaafunzi kuwa kwa mwanafunzi aliepo mwanza kama leo Alhamisi kasoma heabu kugawanya basi na mwanafunzi aliyeko Dar awe amesoma hesabu ya kugawanya muda ule ule.
Lengo lao ni kuweka uniformity kwa Tanzania nzima ambapo swala hili kiutendaji ni gumu sana ukizingatia idadi ya walimu waliopo na idadi ya wanafunzi.
Mfano: Kuna shule ipo Kongwa ina walimu watatu ikiwa na wanafunzi 478,je wanafunzi hao wataweza kufundishwa kwa njia hizo?
mwongozo ulivyotoka ni kwamba walimu wanatakiwa kuandaa kila kitu upya ikiwa ni pamoja na azimio la somo ambalo tayari walikuwa wameandaa,je kwa hali hiyo mwalimu mmoja anaefundisha physcs form 1 to f6 ataweza kufanya majukumu yote haya?
katika semina hizo nikiwa kama observer nisiejulikana kuna mdau aliuliza whats this for?
jibu lililotoka ni kwamba wanataka kuhakikisha kwamba,wanafunzi wakimaliza level flani wajiajiri..kuliko kusubiriwa kujiajiri
Kwa taarifa za gizani ni kwamba huu ni mkakati wa mwanamama aliepewa ujasiri kwa kukataa div 5 na GPA Ndalichako.., Waziri mpya kaingia kakuta tayari mambo yalishaiva na mwongozo umeshaandaliwa hivyo ukapelekwa OR kwa utekelezaji.
naendelea...
nauleta usijaliUnge-share na huo mwongozo.
khasanet sana madamMi binafsi naomba Mama mheshimiwa Rais Samia anitafutie kitengo chochote angalau niweze kupambana na watu wazima,hisabati wanaelewa watoto wachache bila fimbo ...naadhibu but moyo wangu unajitengenezea chuki hasa nikiwa alone nimejituliza nahisi kama wanaumia tunavyowaadhibu.