Tamko la Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Dar es Salaam (DCPC) kumtaka Freeman Mbowe kuomba radhi

Tamko la Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Dar es Salaam (DCPC) kumtaka Freeman Mbowe kuomba radhi

Mbowe keshatengenezewa zengwe la kiutu uzima. Leo ACT mkutano wote umeonyeshwa, maana yake mzee wa Hai keshawekwa kwenye kona ya kutakiwa kujitetea.

Siasa ni lazima uisomee na ufaulu mitihani ya vyuoni.
 
Wapeleke upuuzi huko.

Hakuna mtu atawaomba radhi hao wazee wa bahasha za kaki, hizo njaa zao wazipeleke huko CCM.
Leo kwenye mkutano wa ACT wamekata sauti wakati bwege anananga udhalimu wa utawala huu dhalimu kuhusu kuzulumu wakulu,watumishi,kumiliki wasiojulika
 
Wangekua na nia njema wangekua wanakemea madhila waaliopata kina Azory Gwanda au wangepigia kelele hii sheria ya vyombo vya habari inavyotumika kukandamiza vyombo vya habari kupitia idara ya habari maelezo chini ya Dr. Abassi.

Na najua wamekuja na hili 'Tamko' ili wengi Wao wasikike tu na 'Boss' Wao Dkt. Abbas aweze Kuwaombea 'Uteuzi' kwa 'Bwana Mkubwa' Serikalini.
 
Mmawia,
Wanateseka sana kuona lissu anajaza mikutano pasipo kutumia nguvu ya vyombo vya habari na wasanii. Mwaka huu kawashika kubaya mno.
Wamekuja na sheria za kutumia drone sababu ya lisu syndrome, yote ni kumuhofia.mzungu anatengeneza drone mwafrika anatengeneza sheria kuzuia matumizi ya drone kwa sheria za maagizo hazijapitia hata bungeni
 
Wamekuja na sheria za kutumia drone sababu ya lisu syndrome, yote ni kumuhofia.mzungu anatengeneza drone mwafrika anatengeneza sheria kuzuia matumizi ya drone kwa sheria za maagizo hazijapitia hata bungeni
Mamlaka zinazoundwa na serikali huwa na nguvu ya kisheria. Drones zinaweza kugeuka kuwa silaha, zikiwa mikononi mwa mtu mwenye nia mbaya ni za hatari sana kiulinzi.

Marekani anawauwa magaidi wake kwa kuzitumia hizo hizo drones. Huyo Lissu umemuona mtu muhimu sana mpaka mamlaka za nchi zifanye kazi kwa kumuogopa?.
 
Kiukweli
Wapeleke upuuzi huko.

Hakuna mtu atawaomba radhi hao wazee wa bahasha za kaki, hizo njaa zao wazipeleke huko CCM.
TBC wanatakiwa kujitathimin, pamoja na kwamba yawezekana mbowe aliotoa maamuzi kwa hasira, maana kila ukitazama TBC haipiti dakika tano bila kuona au kusikia maneno ya mheshimiwa akielezea mafanikio katka utawala wake. Kitu ambacho sidhan kama n sahihi wakati huu wa kampen , maana toka aingie madarakan alikataza maswala ya siasa bas tukaridhika kumwona yeye tu. Na sasa tena tuendelee kumwona yeye tuuuuu?
 
Mamlaka zinazoundwa na serikali huwa na nguvu ya kisheria. Drones zinaweza kugeuka kuwa silaha, zikiwa mikononi mwa mtu mwenye nia mbaya ni za hatari sana kiulinzi.

Marekani anawauwa magaidi wake kwa kuzitumia hizo hizo drones. Huyo Lissu umemuona mtu muhimu sana mpaka mamlaka za nchi zifanye kazi kwa kumuogopa?.
Mbona sheria nyingi kipindi hiki,so mwenye nia ovu akitaka si anachukua kibali tu na kulipia,sema kama lengo ni kutunisha mapato ya kampeni kila mkoa unalipa kwa hela ya mabeberu na si madafu
 
Mbona sheria nyingi kipindi hiki,so mwenye nia ovu akitaka si anachukua kibali tu na kulipia,sema kama lengo ni kutunisha mapato ya kampeni kila mkoa unalipa kwa hela ya mabeberu na si madafu
Siku hizi kuelekea uchaguzi kila kitu kinatazamwa kwa jicho la kisiasa. Kumbuka kuwa hizi drones zimechangia katika kuongeza mapato makubwa ya mamlaka ya anga tangu awamu ya tano ilipoanza.

Pesa imeanza kupatikana kwa wingi kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita, uchaguzi ni mchakato wa kupita tu sio kila kitu maishani.
 
Ulimwengu wa Wanahabari na Watanzania kwa ujumla ulipigwa na butwaa pale Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na
Mimi ni Mtanzania..., Sikupigwa na butwaa...!!! Ila kila siku napigwa na butwaa hiki chombo kinachoendeshwa kwa ruzuku ya Kodi ya watanzania wote kinavyotumika kama chombo cha Propaganda...
 
Siku zote mti wenye matunda ndio hupigwa mawe, hatusikii lingine kila kitu ni ccm. All in all kizuri hughasiwa, mzee magu mi5 tena💪.

Mbowe ukaombe radhi, kitendo kile si uungwana, ulihatarisha usalam wa vyombo vya wanahabari wa tbc. Ukiawa kama msomi lazima mambo upekeke kisomi, sas nashangaa na chama cha kukuamini kua mwenye kiti alafu leo hii umekua wa kukurupuka.
 
Mbowe keshatengenezewa zengwe la kiutu uzima. Leo ACT mkutano wote umeonyeshwa, maana yake mzee wa Hai keshawekwa kwenye kona ya kutakiwa kujitetea.

Siasa ni lazima uisomee na ufaulu mitihani ya vyuoni.
Muongo mkubwa, hotuba ya mheshimiwa Bwege waliikata yote
 
Kuamini Lissu atakuwa rais wa nchi hii ni kuonesha wewe una akili za kuvukia barabara tu. Mwenye akili timamu hawezi dhani Lissu atakuja apishwa kuwa rais. Labda kuapishwa kuwa mwenyekiti wa kijiji flani...😂😂😂

Cdm hatuna cha kupoteza kwenye hili. Na hao hao makanjanja wajiandae siku mh Lissu akisha apishwa.
 
Umeandi upumbavu. Kuamini Lissu atakuwa rais wa nchi hii ni kuonesha wewe una akili za kuvukia barabara tu. Mwenye akili timamu hawezi dhani Lissu atakuja apishwa kuwa rais. Labda kuapishwa kuwa mwenyekiti wa kijiji flani...[emoji23][emoji23][emoji23]
Hata wewe kuamini kuwa mgombea kutoka ccm ndiyo pekee mwenye haki ya kupata urais wa nchi hii ni upumbavu wa kiwango cha SGR.
 
Kwani wao hawakuona jinsi TBC wanakata sauti inabaki picha tu anaongea mtu humsikii.Mbona wakiwa wanaonesha ccm hawajati?

Na ACT Leo walikuwa wanawakatia.kama yule jamaa alikuwa ana ghani ushairi alikatiwa
 
Back
Top Bottom