TANESCO imeisamehe Zanzibar deni la umeme la bilioni 60

Zenj,inaingia kwa Mkoa wa kagera mara Tano,Haina viwanda vingi bili yake ya umeme ni sawa na matumizi ya umeme kwa kata ya kawe Dar,it's drop of water In a ocean!!ni pesa kidogo sana.
Uktegemea wanaotawala zenj,wote ni mamluki kutoka bara,waliamia huko in 1940s,
Zenj tuione kama wilaya ya kaliua au mbogwe tu
 
Ukweli ni kwamba hii sio mara ya kwanza deni la umeme Zanzibar linafutwa nafikiri ni mara tatu au nne hivi madeni yao yamefutwa. Kitu cha ajabu Zanzibar wanalo shirika lao la umeme na wanatoza bili za umeme sasa zile fedha wanazokusanya wanapeleka wapi? Pili kuna kipindi walinunua au walipewa majenereta makubw ya kuzalish umeme wao wenyewe imekuwaje wasizalishe au ndio wanasubiri wa bure jamani hii Tanganyika sasa kesho bungeni utasikia wanaliponda shirika la Tanesco linatia hasara......maajabu ya Firauni
 
Kama ni ukweli 😭😭😭😭😭
 
Hii ndio faida ya Muungano ulioletwa Nyerere.
 
Ukienda kuuza ndizi huko, toka Tanganyika unambiwaje?

Samaki wa huko Tanganyika hawaliwi na watu bora walioko huko visiwani?

Hopeless Kabisa!

Tanganyika inanunua Muungano na watu wasiotaka kuungana?

Na huyu mama ndio kabisa, anadhani muungano ni kuipa manufaa zaidi Zanzibar, na siyo zaidi ya hapo.
 
Huu muungano ni wa uchaguzi au? Bora kila mtu akae kwake kwa kweli
 
Waswahili wanakwambia ukikipata kitumie. Wakati wao huu wa kutamba.

Ni vile chamwino ilishaanza kujengwa kipindi cha Magu kinyume na hapo hata ikuli ingehamishiwa huko huko pia.
 
Hii ndio faida ya Muungano ulioletwa Nyerere.
Nyerere hakuleta muungano wa namna hii, tusiwe tunalaumu na kusema mambo yasiyokuwa kweli.Haya wanayofanya hawa sasa hivi ni ya kwao, siyo ya muungano uliokusudiwa uwepo.
Elekeza lawama kwa hawa waliopo sasa, na kushindwa kuendelea kuujenga muungano uliokusudiwa toka awali.
 
Tunawalipia deni kwa njia tozo, dah ,inauma sana.
 
Sasa muungano una faida gani kwa bara? Kwanini tusiwe na serikali ya Tanganyika kama walivyo na serikali ya Zanzibar au tuwe na serikali moja ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania?

Muundo wa muungano unatakiwa uwe wa Serikali moja au Tatu. Wakikataa wanakwenda kwao
 
Hapa sasa ninakusikiliza, kuliko kule mwanzo ulipotoa lawama tu.

Huu muungano ni wa serikali moja, hayo mengineyo ni kuendeleza kujiona kwa baadhi ya watu kuwa bora zaidi ya wengine katika muungano huo.
 
Kazi kula urojo na kuruka sarakasi tu pale forodhani, wazenji tuondoleeni ujinga wenu lipeni umeme mliotumia maana kuisamehe deni Zenji si haki, Ili muungano ukae sawa na bara pia inabidi umeme uwe Bure!
Hahahahaaa..... eti kuruka sarakasi.
 
Wizara za muungano huwa zinadaiwa madeni na TANESCO...hawalipi....tunashangaa nini kusamehewa kwa Zanzibar ilihali ni sehemu ya Muungano?!!
 
Hapa sasa ninakusikiliza, kuliko kule mwanzo ulipotoa lawama tu.

Huu muungano ni wa serikali moja, hayo mengineyo ni kuendeleza kujiona kwa baadhi ya watu kuwa bora zaidi ya wengine katika muungano huo.
Sasa ni nini kifanyike?
 
Wizara za muungano huwa zinadaiwa madeni na TANESCO...hawalipi....tunashangaa nini kusamehewa kwa Zanzibar ilihali ni sehemu ya Muungano?!!
Wizara zote zilitakiwa ziwe chini ya muungano na tuwe na Serikali moja ya muungano.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…