TANESCO inaweza ikatengeneza faida kubwa sana endapo wataanza kukopesha units za LUKU. Hii ni ngumu kwa mteja kukwepa marejesho

TANESCO inaweza ikatengeneza faida kubwa sana endapo wataanza kukopesha units za LUKU. Hii ni ngumu kwa mteja kukwepa marejesho

Umeangalia kwa mtazamo mmoja. Kwa wenye nyumba tu lakn haujaangalia kwa wapangaji. Mtu amepanga fremu au nyumba nzima. Siku anakaribia kuondoka anakopa umeme wa 20,000. Na halipi deni.
Hiyo hela atalipa nani? Siyo rahisi kama unavyofikiria ndiyo maana hauajatoa maelezo yaliyojitosheleza na njia zake ndiyo maana umekimbilia kukopesha.
Hii italeta migogoro sana, na siafiki suala hili la kukopa umeme hata kwa 100%
Hili wazo mbona linatekelezeka tu tena kirahisi bila shida. Hapa nitatoa mfano hai;

Kipindi tunaanza masomo form 1 kulikuwa na fedha ya tahadhari unalipa na fedha hii hurudishwa pindi unapohitimu form 4 baada ya kusainiwa clearance form na kubainika hakuna deni/hasara/uharibifu uliofanya katika kipindi chote cha masomo.

Kwa namna hii hii TANESCO wanaweza kwa kushirikiana na serikali za mitaa kuwaelekeza wamiliki wote wa nyumba za kupanga ku-introduce pesa ya tahadhari kwenye kodi ya pango ambayo inalingana na kiwango ambacho Tanesco wanakopesha.

Kwa namna hiyo, dhamana ya deni inabaki kwa mwenye nyumba na endapo mpangaji/wapangaji wanahama bila kuwa na deni pesa ile (ya tahadhari) inarejeshwa kwa muhusika.

Kama wapangaji wako zaidi ya mmoja, fedha ile inagawanya mf. wako watano na kiwango cha kukopa ni 25,000/= basi kila mpangaji kwenye kodi yake ya mwanzo ataongeza elfu 5 kama hela ya tahadhari na siku akiwa anahama na hakuna deni anarejeshewa pesa yake.

Nadhani ni good idea kwa zama hizi kwa Tanesco na hata mamlaka zingine za serikali, itawaongezea wigo wa mapato kupitia riba.

Mbali na hii pia wanaweza kuanzisha utaratibu wa kuwakopesha wateja gharama za kuunganisha huduma na kuweka interest pia, hii itasaidia kupunguza hasara na utegemezi wa ruzuku kwenye uendeshaji wa hizi mamlaka.
 
Zanzibar (TUKUZA) upo umeme wa mkopo. Mkopo huo ni wa units kadhaa tu, ambapo ni rahisi kwa mkopaji kuresha pasi usumbufu.
 
Tumepokea ushauri tunashukuru sana mpendwa mteja wetu

TANESCO , Makao Makuu
Na kingine kwanini msiwe mnawakopesha kuwaunganisha wateja umeme then kwenye kununua umeme muwe mnawakata kidogo kidogo mpaka watakapo maliza deni liwe kama zile unit za kuanzia???
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wa humu JamiiForums.

Kwanini TANESCO haikopeshi units za umeme wa LUKU kwa wateja wake? Mimi ninaona kama mchakato huu utawawezesha kupata faida kubwa sana kama riba kwa maana ni ngumu sana kwa mteja kukwepa marejesho.

Tofauti ya mteja wa TANESCO na mteja wa mtandao wa simu za mikononi kama Vodacom na Tigo ni kwamba, mteja wa mitandao hii ana nafasi kubwa sana ya kutokulipa deni kwa maana anaweza kubadili simcard au anaweza kufa kisha deni likawa limepotea tofauti na mteja wa TANESCO ambaye deni linakuwa limebebwa na nyumba kiasi kwamba hata akifa, deni litakatwa wakati wa ku-transfer property ownership.

Mteja wa mitandao ya simu za mikononi anaweza akakopa Vodacom kisha akahama mtandao akaanza kutumia Tigo, lakini mteja wa TANESCO hawezi kubadili number yake ya mita ya LUKU. Kama alikopa umeme wa 5,000/= kwa kutumia M-PESA inakuwa ngumu sana kukopa tena kwa kutumia mtandao mwingine kama vile TIGO PESA kwa maana atatumia number ile ile ya mita hivyo computer system itakataa kufanya muamala wa kumpa units.

TANESCO wanaweza kufanya special arrangement na kampuni husika ya mtandao wa simu kama Vodacom au Tigo kutoka mkopo wa pesa mahususi kwa kununua units za umeme tu na sio muamala mwingine wowote. Ukitumia pesa hiyo kwa muamala mwingine inakataa.

Mathalana TANESCO wanaweza kukukopesha umeme wa 4,000. Halafu utakatwa labda 25% kila utakaponunua tena mpaka deni liishe. Au ukiamua unalipa 100%.

Wataalam wa masuala ya uchumi pamoja na ICT mnaweza kulifafanua hili zaidi kwa maana hiyo sio taaluma yangu lakini ninapendekeza number itakayoruhusiwa kukopa iwe moja tu (Mmiliki wa nyumba) hususan kwa nyumba zenye wakazi (wapangaji) wengi

NB: Ndugu zangu waislam, Mungu awatangulie na kuwasimamia katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani. Siku zote 30 za mfungo zikawe za kheri na baraka kwenu. Wishing you courage and strength so that you win every challenge of this life.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Ndio maana niko "addicted" na JF na hasa GT, wengine tulipepesa macho huko kwa Wakoloni wetu, ni jambo la kawaida sana, fikiria umeme wakatika saa saba usiku na huna chochote kwenye mobile wallet wala ile mikopo yao?!
Brilliant idea ila kama uwajuavyo TANESCO wako kama DAWASA, wagumu kufikiria, hawafikiri nje ya boksi wala ku "brain storm" zile "grey cells" zao kichwani!
Tuombe watausoma huu uzi na kutafakari...
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wa humu JamiiForums.

Kwanini TANESCO haikopeshi units za umeme wa LUKU kwa wateja wake? Mimi ninaona kama mchakato huu utawawezesha kupata faida kubwa sana kama riba kwa maana ni ngumu sana kwa mteja kukwepa marejesho.

Tofauti ya mteja wa TANESCO na mteja wa mtandao wa simu za mikononi kama Vodacom na Tigo ni kwamba, mteja wa mitandao hii ana nafasi kubwa sana ya kutokulipa deni kwa maana anaweza kubadili simcard au anaweza kufa kisha deni likawa limepotea tofauti na mteja wa TANESCO ambaye deni linakuwa limebebwa na nyumba kiasi kwamba hata akifa, deni litakatwa wakati wa ku-transfer property ownership.

Mteja wa mitandao ya simu za mikononi anaweza akakopa Vodacom kisha akahama mtandao akaanza kutumia Tigo, lakini mteja wa TANESCO hawezi kubadili number yake ya mita ya LUKU. Kama alikopa umeme wa 5,000/= kwa kutumia M-PESA inakuwa ngumu sana kukopa tena kwa kutumia mtandao mwingine kama vile TIGO PESA kwa maana atatumia number ile ile ya mita hivyo computer system itakataa kufanya muamala wa kumpa units.

TANESCO wanaweza kufanya special arrangement na kampuni husika ya mtandao wa simu kama Vodacom au Tigo kutoka mkopo wa pesa mahususi kwa kununua units za umeme tu na sio muamala mwingine wowote. Ukitumia pesa hiyo kwa muamala mwingine inakataa.

Mathalana TANESCO wanaweza kukukopesha umeme wa 4,000. Halafu utakatwa labda 25% kila utakaponunua tena mpaka deni liishe. Au ukiamua unalipa 100%.

Wataalam wa masuala ya uchumi pamoja na ICT mnaweza kulifafanua hili zaidi kwa maana hiyo sio taaluma yangu lakini ninapendekeza number itakayoruhusiwa kukopa iwe moja tu (Mmiliki wa nyumba) hususan kwa nyumba zenye wakazi (wapangaji) wengi

NB: Ndugu zangu waislam, Mungu awatangulie na kuwasimamia katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani. Siku zote 30 za mfungo zikawe za kheri na baraka kwenu. Wishing you courage and strength so that you win every challenge of this life.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Salary advance🤣
 
Back
Top Bottom