*SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)*


*TAARIFA KWA WATEJA WETU WA GONGO LA MBOTO*

*MACHI 30, 2020*

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Ilala linawaomba radhi Wateja wake wa Gongo la Mboto na maeneo jirani kwa katizo la umeme lililotokea leo Jumatatu Machi 30, 2020, saa 5:11 asubuhi.

*Sababu* Hitilafu kutokana na "jumper" (Kiungio) kukatika kwenye line ya 132kv inayotoka Kinyerezi.

*Maeneo yanayoathrika:*
Kampala University, kwa Mkolemba, Moshi Bar, kwa Mwanaharusi, Msalaba mwekundu, Sukuma land, kwa Diwani, Kanyigo, baadhi ya maeneo ya Kivule, Mbondole, Frame Kumi,Nyang’andu, kwa kichonge, Chakenge, baadhi ya maeneo ya Msongola,
Pugu Mikongeni, Pugu Mnadani,
Namera Group of Industry,
Gongo la mboto jeshini, mwisho wa lami, Majohe, Ulongoni B yote, mama Sakina, ukonga
sabasaba, STK, FQ, Said mwema, Gogo zembe na baadhi ya maeneo ya jirani.


Mafundi wetu na Wataalamu wanaendelea na kazi kuhakikisha huduma ya umeme imerejea.

*Tunawaomba Radhi wateja wetu kwa usumbufu unaojitokeza*

*Kwa mawasiliano*

Kituo cha miito ya simu Makao Makuu 0222194400 na 0768 985100

Tovuti: www.tanesco.co.tz

Mitandao ya Kijamii
Tanesco Yetu

Twitter, www.twitter.com/tanescoyetu,

Instagram: tanesco_official_page

YouTube: tanescoyetu

Tunaomba radhi kwa usumbufu unaojitokeza

Imetolewa na:-
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu




TANESCO Makao Makuu| 0768985100|customer.service@tanesco.co.tz
 
Ni siku ya nne leo hapa mjini Hedaru hamna umeme kisa nguzo mbili zilianguka na meneja yupo amekaa tu ofisi hawa ndio wanaomsumbua muheshimiwa Rais mwenye number ya Kalemani naomba anitumie sasa hivi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba nisaidiwe namba ya huduma kwa wateja TANESCO Mlandizi, tafadhali.
 
Tanesco kunani na huu mkato wa umeme kila siku,kumekuwa na katizo la umeme siku hizo kila siku,na mnaweza kukata hata Mara Tano kwa siku moja,hasa maeneo ya kigamboni, toangoma,Tunaomba mtujuze tanesco Kuna shida gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi Tanesco inakuwaje huu umeme au mgao kimya kimya? Twambieni basi kama ni mgao tuwe tuna andaa hata mishumaa, kama leo saa 7-10 jioni, inafika saa 1 hao mmebeba tena mpaka saa 2 maisha gani hayo hamtaki tujue taarifa twambieni basi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanesco mnasikitisha sana.Mambo yale yale tunazungumzia kila siku humu na waziri kawaambia lakini waapi.
Sasa hivi hapa imepiga radi moja tu,umeme hakuna Kimara.
Mnasikitisha kwa kweli.
 
Habari.
Miaka miwili iliyopita,waziri wa nishati, medard kalemani, alifanya ziara eneo LA bulale kata ya buhongwa jijinj mwanza, ikiwa ni maagizo ya waziri mkuu wakati akifungua zahanati ya bulalebaada ya wananchi kulalamika kuhusu ukosefu wa umeme katika eneo hili.
Katika ziara hiyo waziri aliagiza umeme uwake ndani ya wiki moja na katika kurahisisha zoezi hilo, Tanesco wafungue ofisi ya muda bulale ili wansnchi wapate huduma karibu.
Miaka zaidi ya miwili baadaye, wakazi wengi wamefanya "wiring" na kujaza fomu( mimj mmoja wao) nguzo zimewekwa transfoma imefungwa lakini umujitokeza ubaguzi kuwaunganisha wateja wapya.
Niko jirani na shule ya msingi Lumeke,eneo LA tarazo, nimeshuhudia jumanne ya wiki hii nyumba mbili zikifungwa umeme huku sisi tulio jirani na nyumba hizo tukibaki midomo wazi!
Iweje nyumba hizo, tena zilizojengwa nyuma yetu zipewe huduma hiyo ilihali, tuliojaza fomu na kuziwasilisha tanesco nyamagana, tumebaguliwa?
Vigezo gani vimetumika kuziunganisha nyumba hizo na huduma ya umeme na kutuacha wengine tena kwa kuruka nyumba nyingine?
Tunakusudia kuchukua hatua zaidi ikiwa hadi kufikia wiki ijayo, tutakuwa hatujapata maelezo sahihi ya kwanini baadhj yetu tumerukwa kupata huduma hii ilihali wengine katika eneo LA ndani ya mita 10, 20, 30 na ambako tayari kuna nguzo kwa zaidi ya miezi sita sasa hatupati huduma hizo.
 
Kweli Kuna muda mnaonekana kikwazo hivi leo weekend watu wanatulia na familia zao majumbani mmeukata umeme tokea saa nne kimara baruti hakuna umeme tatizo nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TANESCO walipewa maelekezo ya kutoruka makazi ya watu pindi wanaposambaza umeme.

Katika eneo la Naliendele mkoani Mtwara umeme uko ktk mitaa ya Pwani, Mnali halafu wakaruka nyumba 400+ zilizopo pachoto A na Pachoto B wakaenda kuweka Sogea.

Wananchi wa Pachoto A na Pachoto B wanaamini kuwa walirukwa makusudi na wanasema nyumba za Sogea zinamilikiwa na vigogo wa taasisi mbalimbali ndomaana mradi wa REA wa Pachoto A na Pachoto B ukakimbizwa kule.

Wanatamani siku Mh Rais atakapokuja wamwombe awasaidie umeme kwa gharama yoyote hata kamasi wa REA

Wanaamini watendaji wa TANESCO Mtwara wana laana.

TANESCO Tanzania kazi kwenu. Meneja wenu alimuuziaga transformer mwekezaji Mh Rais akaingilia, leo mnafanya tena uhuni ngoja aje tena maana hamwezi bila kusukumwa.

Mh Rais karibu sana Mtwara baada ya likizo, karibu ili umkague mkandarasi wa barabara ya Mtwara-Newala, karibu ushangae maajabu ya TANESCO

Sent using COVID-19
 
TUSAIDIE namba yako ya simu wataalamu wetu wafike kuangalia swala lako tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kawaida kabisa Tanesco kuruka maeneo yenye nyumba za wakazi ambao ni wanachama wa vyama vya upinzani.hata mkoa wa Geita Kuna vijiji vilivukwa na umeme.sio huko tu
 
Ni kawaida kabisa Tanesco kuruka maeneo yenye nyumba za wakazi ambao ni wanachama wa vyama vya upinzani.hata mkoa wa Geita Kuna vijiji vilivukwa na umeme.sio huko tu
Kuhusu Geita, Wala Sipingi.
Mfano mzuri ni eneo la chini ya Secondary Mwatulole.

Mwatulole centre kuna umeme, mwabasabi kuna umeme , ila hapa katikati hakuna.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kawaida kabisa Tanesco kuruka maeneo yenye nyumba za wakazi ambao ni wanachama wa vyama vya upinzani.hata mkoa wa Geita Kuna vijiji vilivukwa na umeme.sio huko tu
Na baadae wanakwambia MAENDELEO HAYANA CHAMA.
 
Hii kitu inasikitisha sana japo wao TANESCO watapinga lakn huo n ukweli maeneo ambayo wapinzan wanaongoza Mara nyingi wanarukwa kina clip moja mh kibajaji mbunge waMtera alikuwa akiongea na wananch nadhan Songea aliwaambia ukweli jinsi Ccm inavyofanya kukandamiza upinzan wakishirikiana na mawaziri

Hii kauli ya maendeleo hayana chama n changalamacho TANESCO n kama kama rubber stamp tu lakn mipango yao inapangwa na Ccm wao hawana maamuzi yoyote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mradi mwingine nimeukuta kule Nzega kata ya Sigili bado unaendelea.

Wameunganisha kwenye taasis za serikali tu,hakuna nyumba hata moja ya mtu imeunganishwa kata nzima.

Uongozi wa vijiji umeenda TANESCO (W) wameambiwa wasubiri awamu zijazo.

Ukisikia takwimu za REA kuungasha maelfu ya vijiji unafarijika lakini ukifuatilia uhalisia umejaa ubabaishaji tu.
 
Sasa hao chadema nao si wanalipa kodi kwanini wasipewe umeme!

Longolongo za waswahili hawa ni vituko tupu!

Typical uswahili : Majungu, wivu, visasi husuda na vijiba vya roho! Mwisho wake wote tunageuka kuwa taifa la wachawi.

Wengine wanaruka kwa sababu kuna ex wake huo mtaa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cha kushangaza na kufurahisha,waziri wa nishati, Mh medadi kalimani ni mbuge wa chato mkoa wa Geita, bado umeme kwenye mkoa wake wa Geita Kuna vijiji vinavukwa bila kupewa umeme wa REA,je vijiji vilivyoko mikoa mwingine itakuwaje? Kule losokonoi,lendenai wilaya ya shimanjiro mkoa wa manyara, umeme wa REA uliogharimu mabilioni ya shilingi unefungwa kituo cha afya na shule ya msingi ambayo haitumii umeme usiku na kutelekeza wananchi kata 320 bila kupewa umeme .tulilalamika awali wakati mradi ukiendelea meneja wa Tanesco simanjiro ,matokeo yake meneja alihamishiwa same na kupandishwa cheo. Tanesco inaendesha miradi ya kisiasa ambayo siomiradi sustainable.na wanamdanganya mh Rais .kituko kikubwa ambacho ni historia kwa Tanesco, mameneja wote wa mikoa ya Tanzania ni maengineer,pamoja na elimu nzuri waliyonayo wanasimamia miradi ya REA tunaeekewa tranfoma ni ndogo na mradi ni wa mabilioni,m ambapo eneo Hilo hata kiwanda kikifungwa umeme hautoshi kwani transfoma ni ndogo.zikifungwa mashine za kusaga za umeme mbili tu umeme hautoshi.tanesco Kuna vituko vingi sana sana.
 
Ni kawaida kabisa Tanesco kuruka maeneo yenye nyumba za wakazi ambao ni wanachama wa vyama vya upinzani.hata mkoa wa Geita Kuna vijiji vilivukwa na umeme.sio huko tu
Pachoto A na Pachoto B ni ngome ya CCM TANESCO waliparuka makusudi ili nyumba za vigogo za Sogea zipate umeme kwa 27,000 sasa Pachoto wako tayar kuwekewa hata kwa 300,000/= naamini Mh Rais atatusaidia akija wakati TANESCO wakisubiri namba za simu

Sent using COVID-19
 
Kuna kipindi nilisikia Tanesco kuna planners na engineers. Nadhani wote walitumbuliwa wakati wa vyeti feki, otherwise Tanesco wasingefanya kazi kama vile wanaongozwa na wajumbe wa chama cha ACT wazalendo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…