TANESCO walipewa maelekezo ya kutoruka makazi ya watu pindi wanaposambaza umeme.
Katika eneo la Naliendele mkoani Mtwara umeme uko ktk mitaa ya Pwani, Mnali halafu wakaruka nyumba 400+ zilizopo pachoto A na Pachoto B wakaenda kuweka Sogea.
Wananchi wa Pachoto A na Pachoto B wanaamini kuwa walirukwa makusudi na wanasema nyumba za Sogea zinamilikiwa na vigogo wa taasisi mbalimbali ndomaana mradi wa REA wa Pachoto A na Pachoto B ukakimbizwa kule.
Wanatamani siku Mh Rais atakapokuja wamwombe awasaidie umeme kwa gharama yoyote hata kamasi wa REA
Wanaamini watendaji wa
TANESCO Mtwara wana laana.
TANESCO Tanzania kazi kwenu. Meneja wenu alimuuziaga transformer mwekezaji Mh Rais akaingilia, leo mnafanya tena uhuni ngoja aje tena maana hamwezi bila kusukumwa.
Mh Rais karibu sana Mtwara baada ya likizo, karibu ili umkague mkandarasi wa barabara ya Mtwara-Newala, karibu ushangae maajabu ya
TANESCO
Sent using
COVID-19