Napatikana Ilala Banana Dar es salaam ,
Mkuu Ni wiki km Tatu sasa Hatuna Umeme Sababu Mita No. Ni Mbovu Tulichukua hatua ya Kuwataarifu TANESCO Waweze Kufanya Marekebisho Lkn walisema inatakiwa Kubadilishwa tupatiwe nyingine mpya Lkini Tunaishia Kuambiwa Tutakuja Kesho . TAMBUENI KUWA UMEME NI KILA KTU KWA MAISHA YA SASA.., So can You tell me Hata km ni Wewe UTAWEZANA kukaa Bila umeme For a Month...?[emoji40]

Sent from my AUM-AL00 using Tapatalk
 
Poleni na majukumu, mimi ni mkazi wa dar es salaam maeneo ya Mbweni NHC jirani na Faraja Pub.
Nawaletea malalamiko yangu toka jana saa 9 mchana hatuna umeme ni baadhi ya nyumba. Nimetoa taarifa Tanesco tawi la tegeta lakini cha kusikitisha toka jana hakuna jitihadazozote zilizotekelezwa mpaka muda huu naleta malalamiko yangu humu. Wanatoa majibu mepesi mafundi watakuja bila kujali hali ilivyo kwa sasa dar es salaam tumeambiwa tukae ndani, kutokana na ugonjwa wa hatari Corona, tuna akiba ya vyakula vinaharibika kwenye mafridge simu hazina charge tv na radio hazifanyi kazi huko ndani tunakaaje na mh. Waziri Kalemani alisema umeme usikatike. Tunaomba mtusaidie watanzania wenzenu tunateseka kuweni na huruma basi

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Tanesco Kindly respond to this....
 
Tanesco huku mlikofikia sio uungwana kabisa!!

Ni kama week ya pili sasa Uyole,Mbeya mnatukatia umeme kwa zaidi ya masaa 10-12 bila kuwepo taarifa maalumu

Tuhurumieni wengine tutakufa njaa tunaotegemea umeme yaani Corona itupotezee hela na nyie pia

Huo sio uungwana kabisa au kwasababu mnategemea mwisho wa mwezi! Tunaoathirika ni sisi na nimeandika haya kwa hasira na ghadhabu ikiwaka juu yenu.
 
Ukiuziwa nguzo utaunganishiwa umeme?
Mfano umeuziwa tu nguzo peke yake utaifanyia nini? Kupasua kuni, kujengea banda ama nini? Na ukiuziwa nguzo dai risiti ya nguzo.
Ninavyo fahamu TANESCO wana charge kutokana na umbali wako. Nguzo ni baadhi tu ya vifaa ambavyo hutumika pale umbali unapozidi mita 30.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
 
TANESCO kimara mwisho tumelala giza umeme umerudi asubuhi.Nilipiga simu usiku wakaniambia kuna hitilafu sababu ya mvua.
Asubuhi umerudi,saa hizi saa saba na nusu umekatika tena,nawapigia wanasema vile vile hitilafu.
Hizi hitilafu zenu zinaisha lini?in a scope of 24 hours tayari umeme umekatika mara mbili kwa vipindi vya masaa mengi.Mna shida gani nyinyi?Narudia neno lile lile mvua ni asili ya dunia,tunazo hadi kiama,mnaposingizia mvua kwa hitilafu mnataka kusemaje?hebu jifunzeni kuendana na mazingira.Umeme ni kitu sensitive.Acha mvua zinyeshe lakini umeme uwepo.
 
Magomeni Kilosa Morogoro,tunahitaji umeme,na tumefanya tàratibu zote,imebaki kulipia tu.Ili umeme ufike kwangu inahitajika nguzo moja.Nimefuatilia ili nilipe hiyo 27000,naambiwa nguzo hazipo.nitulie kwanza Hadi zitakapokuja.Huu ni mwaka sasa bado naambiwa nisibiri nguzo!Sasa sijui hizi nguzo zitakuja lini!Nauliza;hizo nguzo zinapatikana nchi gani?Na zitakuja lini?Au sisi hatupo katika hiyo ya 27000?Namba zangu ni hizi 0754-384 094

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu yangu kama umbali ni zaidi ya mita 30 na huo umbali lazima kuwepo na nguzo na nguzo hitajika ni moja bora uombe wakupe quotation tu ambayo itakuwa around 340,000/= au na zaidi kidogo. Ukisubiri hiyo 27,000 unaweza ukajikuta maishani hupati umeme. Kama unapenda umeme fanya hivyo nilivyokushauri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba kuna kitu nijuzwe kuhusu tanesco, amesikika mara kwa mara waziri wa nishati kwamba nguzo ni bure na ni kazi ya tanesco, inachotakiwa kwa mteja ni kufanya maandalizi tu ya nyumba yake halafu anaomba umeme, swali je ni kweli nguzo bure? Swali la pili imekuwa kawaida ya tanesco kwamba ukiomba umeme kuwekewa huwa inachukua mda mrefu mapaka wakuwekee, sijajua tatizo ni nini na je bado mnaendelea na hii tabia au mmebadilika, asante, naomba majibu kwa wahusika tafadhari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
tanesco jaman mbezi kwa msuguri karibu na kanisa la Roma hatuna umeme siku ya tatu leo chanzo ni moundo mbinu zenu zimepata shida kidgo tafadhalo tunawaomba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
...dah, kulikoni wajameni?
Huku nikiendelea kuji lockdown hapa kuna kitu cha ajabu ambacho kinaendelea kutokea ambacho sijawahi shuhudia!
Huu umeme yaani kila baada ya dakika moja unarudi na kukatika, umeshakatika na kurudi zaidi ya mara 65!
Hata wakati naaza kuandika huu uzi umekatika na kurudi mara tatu!
Je wadau, huko mliko hili tatizo mnalipata?
Juzi ulikuwa ukifanya hivyo hivyo mwishowe ukaniunguzia radio, kwa sasa chombo cha umeme kama tv, friji sithubutu kabisa kuwasha!
TANESCO kuna nini leo...!?


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Your browser is not able to display this video.
 

Je katika hivyo vifaa nguzo haipo kwenye hesabu?


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…