Ahsante kwa taarifa tafadhali onyesha namba yako ya simu na namba ya taarifa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tangu jana usiku mida ya saa mbili waya za umeme zimekatika hapa maeneo ya Tandale
Watu hawana umeme lakini pia usalama ni mdogo kwakua waya zipo chini tumewapigia sana simu kuja amtaki tatizo nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanesco tafadhali naomba mnipe ufafanuzi kuhusu swala la Tariffs maana Naona kama mnanishinda,Yani Nyumba yangu ina vyumba vitano natumia vyumba 3 umeme na nimefunga taa 3 nje na zote ni zile za umeme mdogo,Inakuwaje umeme wa 9000 napata Unit chache?
Pili mlolongo wa kubadili tariff kwanini tusiufanye Online hasa kwa kipindi hiki cha Mlipuko wa Ugonjwa wa Corona?
 
TANESCO Nimelipia umeme ,tarehe28/03, niliambiwa ndani ya mwezi baada ya kulipia utakuwa tayari imekuaje mpaka leo kimya.??

Na nguzo ipo nje kwangu..

Niliomba kisarawe, nyumba yangu ipo chanika..

Naomba majibu, au nichukue hatua gani zaidi.??

TANESCO TANESCO TANESCO

Msafwa,
Uporoto, Mbeya..
 
Ndugu TANESCO ,nilipitia process zote ili nipate umeme, na nikapewa C-number nikaenda kulipia Tarehe 28/03/2020..

Nikahaidiwa kuwa ndani ya siku30 nitaingiziwa umeme, maanayake ilipaswa niwe nimewekewa umeme kabla ya tarehe 28/04/2020..

Leo ni tarehe 7/05/2020 yaani mwezi na siku10, bado sijaingiziwa..

Nguzo ipo,..

Nifanye nini ili mtekeleze wajibu wenu kama mimi nilivyotekeleza wangu wa kulipia.????

Niliomba umeme Kisarawe kwasababu nyumba ipo Chanika mwisho..



Msafwa,
Uporoto, Mbeya..
 
Futuhi...
wanaweza wakuambie umeme upo bandarini unashushwa.
 
Nenda kamuone meneja wao hapo Kisarawe. Kuna jamaa mmoja msukuma yupo poa sana. Fasta tu utawekewa. Mie pia walikuwa wananifanyia danadana hizo, nikatimba pale, sikutaka maongezi na mtu yeyote zaidi ya manager. Siku hiyohiyo umeme ulikuja kufungwa.
 
Mkuu hao watafutie sukari kidogo tu kabla jua halijachwa utashangaa lijiumeme hilo linawaka. Ukienda kiofisi utapewa maneno kibao mara ngoja kwanza kuna walioomba kabla yako au nguzo hazipo. Acha ubahili jikusanye uwaone. Kuna jamaa yangu alitaka huduma hawakuja mwaka mzima. Siku amewalambisha tu walitokeza siku ya pili asubuhi kwelikweli wakamfungia kila kitu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nenda kamuone meneja wao hapo Kisarawe. Kuna jamaa mmoja msukuma yupo poa sana. Fasta tu utawekewa. Mie pia walikuwa wananifanyia danadana hizo, nikatimba pale, sikutaka maongezi na mtu yeyote zaidi ya manager. Siku hiyohiyo umeme ulikuja kufungwa.
Fata ushauri wa jamaa hapo juu👆 uko 💯
 
Personal interests vs national interests-hao ndo wanakwamisha maendeleo ya nchi,wamepewa mamlaka ya kuweka miundombinu ya serikali ili kuweza kukusanya Kodi toka vyanzo vya mapato ya serikali Leo mtu anachelewesha serikali isipate Kodi mapema,tupia humu jina la huyo mtu na kituo chake Cha kazi jumatatu uende pale utapokelewa Kama mfalme,tupia jina lake na kituo cha kazi
 

Hakuna kitu kinaudhi kama uwe umeshalipia huduma halafu unaendelea kukaa gizani huku ukipasia pasi ya mkaa na kwenda kunyenyekea kwa jirani uwekewe simu kwenye chaji. Halafu hapo eti ukaanze kutoa tena hela nyingine kuhonga wakati umeshalipa? Hell No!

Ewe mtu wa TANESCO, siku ukila rushwa yangu nakuhakikishia itakutokea puani maana ntakujia na TAKUKURU, TARURA, RITA, TRA na kadhalika.
 
Bro! Tupo katika hatua sawa, mm nasubiria mwezi mwingine katika siku 60 nililipia mwezi ulioisha

Ila rudi pale Tanesco waulize vp, mbona kimya jibu lao ukiona hawaeleweki muone meneja kama walivyoshauri humu.

Au la kuna ukurasa wao humu Jamii forum Tanesco hawana longolongo wanajibu fasta na kukupa msaada. Wamenisaidia hata hiyo kupata control number nasubiri siku 60 narudi mkuranga Tanesco Kisha napiga Jamii forum Tanesco mwisho wa matatizo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…