TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Wapendwa wateja wa TANESCO, tunaomba radhi Kwa katizo la Umeme la dharura lilosababishwa na hitilafu ya kiufundi katika kituo chetu cha usambazaji kunduchi.

Wataalamu wetu wanashughulikia kuhakikisha Umeme unarejea kwa wakati.

Maeneo yanayoathirika ni Madale, Tegeta, Mbweni, Bahari Beach, Ununio, Boko na Bunju.

Uongozi unaomba radhi Kwa usumbufu uliojitokeza.

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Kumetokea hitilafu ya umeme Moshi mjini ,
Line ya m2 na m3 zipo nje kutokana na kukatika kwa waya eneo la kibosho Hospital na Moshi club. Mafundi wapo eneo la tukio wakiendelea na marekebisho. Maeneo yanayoathirika ni. Shant yote, kibosho Hospital, na karanga.

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO ) linawatangazia wateja wake wa Wilaya ya Hanang'/ Katesh kuwa patakuwa na katizo la umeme siku ya Jumatano 23/08/2017 na Ijumaa 25/08/2017 kuanzia saa 3.00 Asubuhi hadi saa 11.00 Jioni.SABABU:

Marekebisho ya miundo mbinu ya umeme . Maeneo yatayoathirika ni Wilaya yote ya Hanang', Haydom, Maghang, Getanyamba, Mandi na Sabilo .Uongozi unaomba radhi Kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Kumetokea hitilafu ya umeme Moshi mjini ,
Line ya K 20 haina umeme.Mafundi wanaendelea na jitihada za marekebisho.

Maeneo yanayoathirika ni. Shant yote, Karanga, mail sita, Kibosho manushi, Sambarai minara ya ITV, Machame yote, Weruweru, Shirimgungani na Newland.

Shirika linaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Kumetokea hitilafu ya umeme Moshi mjini ,
Line ya K 20 haina umeme.Mafundi wanaendelea na jitihada za marekebisho.
Maeneo yanayoathirika ni. Shant yote, Karanga, mail sita, Kibosho manushi, Sambarai minara ya ITV, Machame yote, Weruweru, Shirimgungani na Newland.

Shirika linaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
Umeme umerejea tayari
Tunaomba radhi

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Kumetokea hitilafu ya umeme Moshi mjini ,
Line ya m2 na m3 zipo nje kutokana na kukatika kwa waya eneo la kibosho Hospital na Moshi club. Mafundi wapo eneo la tukio wakiendelea na marekebisho. Maeneo yanayoathirika ni. Shant yote, kibosho Hospital, na karanga.

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
Umeme umesharejea
Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)

TAARIFA YA KUTOKEA HITILAFU KITUO CHA KUPOZA NA KUSAMBAZA UMEME KUNDUCHI

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake wa Mkoa wa Kinondoni Kaskazini kuwa imetokea hitilafu katika Kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Kunduchi majira ya Saa 8:34 Mchana.

JITIHADA ZILIZOFANYIKA

Mafundi wamefanya jitihada za kurejesha umeme katika hali ya kawaida na majira ya Saa 9:03 Alasiri hitilafu ilirekebishwa na Wateja kupata umeme isipokuwa wanaopata kupitia njia ya umeme ya TG3 na TG5.

MAENEO YANAYOKOSA UMEME NI:
Kunduchi, Mtongani, Uninio, Boko, Bahari Beach, Bunju, Madale, Wazo na Mbweni.

Tafadhali usiguse waya uliokatika au kuanguka toa taarifa kupitia namba za simu zifuatazo:

Kituo cha miito ya simu Makao Makuu 0222194400 na 0768 985100

Tovuti: www.tanesco.co.tz

Mitandao ya Kijamii
www.facebook/twitter.com/tanescoyetu

Imetolewa na:-
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu
23 Agosti 2017

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)

*TAARIFA YA KATIZO LA UMEME LAINI YA VIWANDA*

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoani Shinyanga linawataarifu Wateja wake wa Shinyanga kuwa, Umeme utazimwa siku ya Alhamisi tarehe 24/08/2017 kuanzia saa 2:00 Asubuhi hadi saa 11:00 Jioni.

*SABABU*

Kupisha kazi ya kubadili nguzo zilizooza, kunyoosha nguzo zilizolala, na kukata miti iliyosogelea laini.

*MAENEO YATAKAYO ATHIRIKA NI*

Maeneo yote ya NBC, Ibinzamata, Mwanakapaya, Ndala Masekelo, Ndala Upongoji, Mwawaza, Kizumbi, Keshini, Nhelegani, na Chuo Cha Muccobs.

*TAHADHARI*

Tafadhali usiguse wala kukanyaga nyaya zilizokatika,Kama kuna tatizo lolote la huduma tafadhali tupigie tuelezee, tutakusikiliza na kukufikia.

Namba zetu:
0754 251 070, 0783 521 070 na 028 2762 120



Kituo cha miito ya simu Makao Makuu 0222194400 na 0768 985100

Tovuti: www.tanesco.co.tz

Mitandao ya Kijamii
www.facebook/twitter.com/tanescoyetu

Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza

Imetolewa na:-
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Shinyanga

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Je naweza kujifungia mita yangu binafsi maana hizi nyumba kupanga kuna mabifu mengi yanatokea kisa Luku na gharama ni kiasi gani na nikihama naweza ichukua hiyo mita yangu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaweza ghara inakuwa 177000 kwa vijijini na 320000 kwa mjini

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Mtwara mjini tungependa kujua kuna tatizo gani na umeme haukai saa moja bila kukatika zaidi ya mara 7 imekuwa kero zaidi ya miezi 3
 
Tanesco Moro mnamatatizo gani mbona umeme unakatika katika sana?
 
Tumeipokea mpendwa mteja

Sent using Jamii Forums mobile app
Habari ya leo nashukuru kwani tatizo langu limeshalekebishwa leo hii kumekuwepo na ushirikiano mkubwa katika suala hili na manager alifika kujionea mwenyewe suala hili jana na leo wamekuja mafundi kulirekebisha wamefanya kazi mzuri kwa ufupi nami natoa shuklani katika kufanikisha suala hili aksanteni sana Tanesco mkuranga sasa nasema kwa upand wangu hakuna tatizo tena

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanesco mnenipitishia waya za HT kwenye nyumba yangu nimekwenda mkuranga kulipot baada ya muda wakaleta nguzo ili waamishe wakaoneshwa pa kuhamishia lakini hao wakalazomish wapitishe sehemu ya mtu mwingine wanayotaka wao sasa mwenyewe kagoma cha kushangaza wanalazimisha waya zibaki hapo hapo kwangu ishafika mahali siwaelewi sasa kilichobaki najiandaa kwenda mahakani nikaone sheria ya kulazimisha kupitisha HT nyumban kwa mtu mumetoa wapi tena waya ziko chini chini si mnataka kuniuwa na familia yangu ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo langu lishatatuliwa natoa shuklani sana kwa mafundi na manager wao kwa kulijali suala hili manager alikuja jana baada ya kuona suala hili leo kaleta mafundi na tayari washarekebish

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom