Mwenye makosa ni mteja au ni watoa fomu?? Lakini huu sio mjadala wakuendelea kujadili mm ninachokiomba ni kujua tu miundo mbinu itanifikia ln lkn kunambia misubiri hapo ndo inakuwa kasheshe kwan kusubiri ni kusubiri tu pengine lbd hadi 2025Fomu ikishatolewa kupitia mfumo inakuwa kwenye mfumo muda wote
Tafadhali onyesha namba ya simu kwa mrejesho zaidiNinaomba majibu yenu TANESCO
Katika mkoa wa Songwe,wilaya ya Mbozi,Mji wa Vwawa kata ya Hasanga kuna mitaa haijapata umeme mpaka leo.
Mitaa hii ni:Iyela, London,mtakuja na Hasanga.
Katika mtaa wa Mtakuja watu kadhaa waliandika barua na kujaza form kwaajili ya kuomba kuwekewa nguzo,kuanzia mwaka 2018, lakini mpaka leo hakuna majibu.Nataka kujua yafuatayo
1.Mitaa hii ipo ktk mfumo wa REA?
2.Kama haipo ktk mfumo wa REA ni kwanini?
3.Ni kwanin mpaka leo Umeme haujasambazwa ilhali maeneo haya yapo sehemu ya makao makuu ya mkoa?
NB:kuwapatia Umeme watu ni kuongezea idadi ya wateja kwenu.Naomba majibu please.
JINSI YA KUONDOA ERROR 77 KWENYE MITA ZINAZOANZA NA NAMBA 2421...Naingiza namba za Luku kwenye mita lakini inaandika Error - 77,nifanyeje
wanakujaNawaheshimu TANESCO makao makuu. Kupitia hii thread nimepata msaada wa namba ya malipo ambayo nilikuwa nikizungushwa Sana na watu wa wilayani zaidi ya nusu Mwaka, lakini baada ya kulalamika hapa, mlinisaidia kuwasiliana nao na mwanzoni mwa mwezi huu nimepata msaada wa namba ya malipo na nimeweza kulipia siku hiyo hiyo! Kwa Sasa BADO nasubiri waje wanifungie umeme.
Nilichokuja kufahamu katika hili, TANESCO makao makuu mpo serious Sana katika utendaji wenu kuhakikisha mnafanikia strategic plan ya serikali kuhusu nishati ya umeme. Kinachowapunguzia kasi ni utendaji legevu wa TANESCO ngazi za chini.
Nashauri katika mfumo wa uongozi wa TANESCO, kuwe na monitoring and evaluation experts ambao watapima na kuratibu utendaji kazi wa watumishi wenu hususani ngazi za chini na ku report kila wiki makao makuu. Mfano, customer care wa TANESCO wamekuwa na kauli na majibu ya kikatili kwa wateja wao, Jambo linalopelekea si tu maudhi na kupungua kwa kasi ya kuenea kwa Huduma ya shirika, Bali pia kupungua kwa Uhusiano mwema Kati yenu na jamii. Mfano, sisi tukipiga simu kuulizia mchakato wa Huduma ulipofikia mnatujibu-jibu Kama mnavyotaka nyie alafu mtarajie tukiona watu wanaohujumu miundombinu ya shirika tutoe taarifa kwenu,Hapana! Lakini kungekuwa na wataalam wanaofuatilia maongezi ya customer care ngazi za chini na wateja na kuyaratibu wangekuwa wanachunga kauli zao
Tunashukuru sana kwa ushauri tunaendelea kuboresha huduma zetuNawaheshimu TANESCO makao makuu. Kupitia hii thread nimepata msaada wa namba ya malipo ambayo nilikuwa nikizungushwa Sana na watu wa wilayani zaidi ya nusu Mwaka, lakini baada ya kulalamika hapa, mlinisaidia kuwasiliana nao na mwanzoni mwa mwezi huu nimepata msaada wa namba ya malipo na nimeweza kulipia siku hiyo hiyo! Kwa Sasa BADO nasubiri waje wanifungie umeme.
Nilichokuja kufahamu katika hili, TANESCO makao makuu mpo serious Sana katika utendaji wenu kuhakikisha mnafanikia strategic plan ya serikali kuhusu nishati ya umeme. Kinachowapunguzia kasi ni utendaji legevu wa TANESCO ngazi za chini.
Nashauri katika mfumo wa uongozi wa TANESCO, kuwe na monitoring and evaluation experts ambao watapima na kuratibu utendaji kazi wa watumishi wenu hususani ngazi za chini na ku report kila wiki makao makuu. Mfano, customer care wa TANESCO wamekuwa na kauli na majibu ya kikatili kwa wateja wao, Jambo linalopelekea si tu maudhi na kupungua kwa kasi ya kuenea kwa Huduma ya shirika, Bali pia kupungua kwa Uhusiano mwema Kati yenu na jamii. Mfano, sisi tukipiga simu kuulizia mchakato wa Huduma ulipofikia mnatujibu-jibu Kama mnavyotaka nyie alafu mtarajie tukiona watu wanaohujumu miundombinu ya shirika tutoe taarifa kwenu,Hapana! Lakini kungekuwa na wataalam wanaofuatilia maongezi ya customer care ngazi za chini na wateja na kuyaratibu wangekuwa wanachunga kauli zao
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)Yaaani watu wa Moshi tunateseka sana na hili shirika. Kila siku umeme unakatika masaa 12 usipokata mchana unakata usiku. Kwa nini mnatuonea na kama kuna mgao si muwe wazi mseme ili tujipange?