TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Mimi nilishalipia umeme wa 27,000 x2 kwaajili ya nyumba zangu mbili kijijini huko kigoma lakini siishi huko nimekuwa nikizungushwa na fundi aliyejifanya ni fundi wa REA bila mafanikio nikawasiliana na tanesco kigoma wakasema hawamjui huyo fundi baadae fundi huyo kishoka wa REA akanipigia kuwa anazo mita za nyumba zangu ila wire wa kuingizia moto ndiyo hamna hivyo nimtumie hela 50,000/= ili mkandarasi wa REA aje nao,nikatuma hiyo hela lakini hakuna kilichofanyika hadi leo.

Baadae nikapata namba ya mkandarasi wa REA nikamueleza kila kitu kuwa kuna fundi umeme anadai ni wa REA ana mita zangu na nimeshampa hela ya waya mkubwa 50,000/= kama ulivyodai lakini sijaingiziwa huo umeme na mita anazo inakuwaje?

Mkandarasi huyo wa REA alinifokea sana na kunitukana kuwa naleta ujuaji hivyo sitafungiwa umeme kamwe hata kama nimelipia.

Napenda kujua swala hili nalifikisha wapi kwa usumbufu na je ni sawa kinachofanyika?

Napia huyu kishoka alipataje hizo mita zangu?
 
Shirika la Umeme Tanzania - (Tanzania Electric Supply Company Limited - TANESCO), Tunaomba mtupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri kupitia huu uzi nasi tutawajibu.

Tunawaomba mzingatie yafuatayo ili kurahisisha ufafanuzi na ufumbuzi wa tatizo au taarifa husika;

1. ENEO HUSIKA

(Mnaweza kuwa eneo moja lakini mnahudumiwa na transfoma au njia ya kusambaza umeme (feeder) tofauti)

2. NAMBA YA SIMU

(Wakati mwingine umeme upo kote isipokuwa kwako hivyo na rahisi kuwasiliana na wewe)

3. KARIBU NA NINI

(Kuna alama vitu au watu mashuhuri karibu na eneo lako mfano ofisi ya Serikali ya Mtaa, Mahakama, Kituo cha Polisi nk)

4. JINSI YA KUFIKA MAKAZI YAKO

(Toa ufafanuzi wa jinsi ya kufika makazi yako,chukulia unamuelekeza mtu ambaya hajawahi kufika kabisa)

5. MKOA,WILAYA NA KITONGOJI/KIJIJI

(Taarifa hii ni muhimu sana kusaidia kubaini eneo husika lipo wapi kwani yapo maeneo yanayofanana kwa majina lakini yapo Mikoa tofauti mfano Magomeni ipo Dar es Salaam na Mkoa wa Mtwara pia.)

6. KAMA NI TATIZO LA MITA NINI KINATOKEA UKIWEKA UMEME

(Kila mita ina ujumbe wake unaoashiria kitu fulani hivyo kubainisha ujumbe kunamsaidia mpokea taarifa kukupatia maelezo sahihi mfano mita namba 24339173921 inaonyesha error 77)

7. KAMA NI KUSHINDWA KUNUNUNUA UMEME UNAPATA UJUMBE GANI NA UNANUNUA KWA NJIA GANI

(Ujumbe huu ni muhimu sana kuweza kubaini chanzo cha tatizo pamoja na njia iliyotumika kununulia umeme mfamo Mpesa, Tigopesa, Maxcom nk)

TUNAENDELEA KUWASIHII WATEJA WETU KUZINGATIA UTOAJI WA TAARIFA SAHIHI NA FASAHA KWA HUDUMA BORA ZAIDI KUTOKA TANESCO.

ENDELEA KUFURAHIA HUDUMA BORA KUTOKA TANESCO

Vilevile pitia threads hizi kupata Maelezo ya ziada;

LUKU:Mfumo wenye Tija kwa Wateja na TANESCO

Fahamu mita za LUKU zinazofungwa majumbani

Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

Kw mawasiliano Kituo cha Miito ya Simu (+255) 22194400 or (+255) 768 985 100 Mitandao ya kijamii Tanescoyetu (@tanescoyetu) | Twitter Facebook: Tanesco Yetu

HAPA CHINI NI NAMBA ZA SIMU ZA MIKOA

Ofisi ya Mkoa wa Mbeya Simu ya Mkononi (+255) 757 529 380 ya Mezani (+255) 252 504 219

Ofisi ya Mkoa wa Ilala Simu ya Mkononi (+255) 784 768 586 ya Mezani (+255) 222 133 330

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kusini (Magomeni) Simu ya Mkononi (+255) 715 271 461/ (+255) 784 271 461

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kaskazini (Mikocheni) Simu ya Mkononi (+255) 784 768 584 / (+255) 716 768 584 ya Mezani (+255) 222 700 367/ (+255) 222 701 602 / (+255) 222 774 098

Ofisi ya Mkoa wa Temeke Simu ya Mkononi (+255) 712 052720 / (+255) 758 880155 / (+255) 732 997361

Ofisi ya Mkoa wa Pwani Simu ya Mkononi (+255) 78 5122020 / (+255) 65 7108782ya Mezani (+255) 23 2 402 386

Ofisi ya Mkoa wa Arusha Simu ya Mkononi (+255) 75 8 174 343 Mezani (+255) 272 506 110

Ofisi ya Mkoa wa Tanga Simu ya Mkononi (+255) 658 122 412/ (+255) 687 677 667 Mezani (+255) 27 2 646 779

Ofisi ya Mkoa wa Kilimanjaro Simu ya Mkononi (+255) 765 397 925/ (+255) 682 771 310 Mezani (+255) 272 755 007/8

Ofisi ya Mkoa wa Manyara Simu ya Mkononi (+255) 689 795 599 / (+255) 75 9 534 130 Mezani (+255) 272 530 590

Ofisi ya Mkoa wa Mwanza Simu ya Mkononi (+255) 759 777 786 / (+255) 687 910 202 Mezani (+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

Ofisi ya Mkoa wa Geita Simu ya Mkononi (+255) 744 085 696 Mezani (+255) 28 2520330

Ofisi ya Mkoa wa Kagera Simu ya Mkononi (+255) 78 5 787 898 / (+255) 75 3 120 701 Mezani (+255) 282 220 061

Ofisi ya Mkoa wa Mara Simu ya Mkononi (+255) 762 165 087 / (+255) 732 985 672

Ofisi ya Mkoa wa Simiyu Simu ya Mezani (+255) 282 700 180

Ofisi ya Mkoa wa Dodoma Simu ya Mkononi (+255) 782 161 643 Mezani (+255) 262 321 728

Ofisi ya Mkoa wa Morogoro Simu ya Mkononi (+255) 68 4889272 / (+255) 65 4829046 Mezani (+255) 232 613 501/2

Ofisi ya Mkoa wa Singida Simu ya Mkononi (+255) 71 4 477 445 / (+255) 732 960 924 / (+255) 689 373 757 Mezani (+255) 262 502 133

Ofisi ya Mkoa wa Tabora Simu ya Mkononi (+255) 786 558 510 / (+255) 763 162 868

Ofisi ya Mkoa wa Shinyanga Simu ya Mkononi (+255) 754 521 070 Mezani (+255) 28 2762120

Ofisi ya Mkoa wa Kigoma Simu ya Mkononi (+255) 78 3720598 Mezani (+255) 28 2802668

Ofisi ya Mkoa wa Katavi Simu ya Mkononi (+255) 68 8345200

IMETOLEWA NA:- Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makauu.

NAMBA ZA SIMU ZA MADAWATI YA DHARURA YA TANESCO MIKOA YOTE

1. Ilala

0222133330/ 0784 768586/ 0715 768586.

2.Kinondoni Kusini (Magomeni)

0784271461/ 0715271461

3. Kinondoni Kasikazini(Mikocheni)

0784 768584/ 0716 768584

4. Temeke

0222138352/ 0732 997361/ 0758881055/ 0712 052720

5. Pwani
078 5122020/065 7108782/023 2402386

6. Mbeya
0759 777781/0787 023422


7.Arusha
0758174343/
0622612501/
+255 27 2506110

8.Tanga
0658 122 412/0687 677 667/ 027 2646 779

9. Kilimanjaro
0765 397 925/0682 771 310/ (+255) 272 755 007/8

10 Manyara
0689 795 599/ 0627938951

11. Mwanza
0759 777 786/0687 910 202/
(+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

12. Geita
0744 085 696/(+255) 28 2520330

13.Kagera
078 5 787 898 / 075 3 120 701/(+255) 282 220 061

14.Mara
0788 950 688/
028 262 2020/
0762 165 087

15.Simiyu
+255 282 700 180/0626383440/0745044072

16. Dodoma
0782 161 643/(+255) 262 321 728

17. Morogoro
068 4889272 /065 4829046/ (+255) 232 613 501/2

18 Singida
071 4 477 445 /0732 960 924 / 0689 373 757/(+255) 262 502 133

19. Tabora
0786 558 510 /0763 162 868

20. Shinyanga
0754 521 070/(+255) 28 2762120 /
0783 521 070

21. Kigoma
078 3720598/(+255) 2988226

22. Katavi
0688345200

23. Rukwa
0252161120/0768879813
24. Songwe
0684 611716/0763 430381.

25. Ruvuma
0252602281/0763 194 979/0787 758 986

26. Njombe
0744703988

27. Mtwara:
0789 999942/023 2333902

28. Iringa 0262702019/0739203015

29. Lindi
0752518247/0685692786


Kituo cha Miito ya simu/Call Centre Makao Makuu

0768 985 100/0222194400

Facebook
www.facebook.com/tanescoyetu

Twitter
www.twitter.com/tanescoyetu

Tovuti
www.tanesco.co.tz

Barua pepe
Customer.service@tanesco.co.tz

Imetolewa na:
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu
Nyumban kwangu kila umeme unapokua mdogo umeme unakata wakati kwa majirani unawaka
Niliita fundi kuangalia lakini ameniambia wiring haina tatizo

Mimi natumia mita ndefu za tanesco zenye kutoa alarm majirani wanatumia vile vi box vidogo
Naomba ufafanuz
 
Ndugu mpendwa Mteja wetu

Tunafurahia kukuhudumia, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora.

Jina

Eneo

Wilaya

Namba ya simu

Tatizo

Toka lini

Namba ya taarifa

Ahsante sana

TANESCO Huduma kwa Wateja

SIMU : 0748550000
 
Nyumban kwangu kila umeme unapokua mdogo umeme unakata wakati kwa majirani unawaka
Niliita fundi kuangalia lakini ameniambia wiring haina tatizo
Mimi natumia mita ndefu za tanesco zenye kutoa alarm majirani wanatumia vile vi box vidogo
Naomba ufafanuz
Je umewahi kuitolea taarifa? Kama ndio tafadhali onesha namba ya taarifa kwa hatua zaidi
 
Ndugu mpendwa Mteja wetu

Tunafurahia kukuhudumia, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora.

Jina

Eneo

Wilaya

Namba ya simu

Tatizo

Toka lini

Namba ya taarifa

Ahsante sana

TANESCO Huduma kwa Wateja

SIMU : 0748550000
TANESCO Tunauliza tena Vifaa hasa Mita za Luku zinafika lini? Watu tumelipia tokea Mwaka Jana mwezi wa 10 na 11 lakini Leo tunaenda mwezi wa 6 Bila kuunganishiwa Huduma ya umeme.

Kila tunapofatilia katika ofisi za Ilemela Mwanza tunaambiwa Vifaa hakuna hivo tuendelee kusubiria... Wale wote tuliokua tumelipia mwaka Jana walitutukia SMS kua tutapatiwa huduma kabla ya tarehe 30/03/2022 lakini Leo ni April na hatujatumiwa SMS tena ili kama tuendelee kusubiri hadi lini?

Apa nafanya mpango wakupata No ya Waziri wa Nishati My January Makamba ili labda yeye ndo atatupa jibu sahihi kua inawezekanaje mteja asubirie zaidi ya miaezi 6 au mpaka tutoe Rushwa???
 
Msaada nimenunua umeme mara mbili ndani ya mwezi mmoja kimakosa ,nikatolewa KWENYE MATUMIZI ya kawaida!!
 
TANESCO hivi Wananchi wakiamua kuwafungulia kesi dhidi ya ucheleweshaji mnaoufanya makusudi wa kutokuwaunganishia wateja umeme ndani ya siku 14 mtapona kweli? Ngoja nimtafute wakili msomi level za Kibatala anipigie mahesabu tokea October last year to date napaswa kulipwa shilingi ngapi? Huenda nikalipwa ela ndefu kwakukiuka mkataba wenu... Kongole kwake CAG kwakututoa shimoni
FB_IMG_1650613992645.jpg
 
mkuu Shirika siku zote linapenda kusikia wateja wake wanafurahia huduma zetu. hivyo basi sio ukiona TANESCO wamekata umeme sehemu jua tu kuna tatizo au ni dharura.

Tunaomba radhi kwa hilo na tutahakikisha tutakuwa tunatoa taarifa mapema kwa wateja wet
Ukitoa taarifa ka mfumo uliotajwa hapo juu hata hapa jamii forum wataalamu wetu watifikish mkoa husik
NAOMBA KUJUA INACHUKUA MUDA GANI KUUNGANISHIWA UMEME BAADA YA KULIPIA?
 
TANESCO hivi Wananchi wakiamua kuwafungulia kesi dhidi ya ucheleweshaji mnaoufanya makusudi wa kutokuwaunganishia wateja umeme ndani ya siku 14 mtapona kweli? Ngoja nimtafute wakili msomi level za Kibatala anipigie mahesabu tokea October last year to date napaswa kulipwa shilingi ngapi? Huenda nikalipwa ela ndefu kwakukiuka mkataba wenu... Kongole kwake CAG kwakututoa shimoniView attachment 2196237
MIMI NILIAMBIWA INACHUKUA SIKU 60 NILIPOENDA KUCHUKUA CONTROL NO. SASA NAJIULIZA HIVI KWELI NI FAIR? NAOMBENI TANESCO MBORESHE HUDUMA ZENU MAANA NIMECHOKA KUSUBIRI SABABU NIMESHALIPIA GHARAMA ZA KUUNGANISHIWA UMEME ZAIDI YA MWEZI SASA.
 
Hivi nyie tanesco mna roho ya uchawi ndani yake? Maana mtu anaehatarisha maisha ni kama mchawi.

Kwa nini mnapewa taarifa za hatari afu mnazichukulia kimasihara au furaha yenu mpaka muone maisha na Mali za watu zimepotea?

Ilitolewa taarufa juu ya nguzo kuoza na kubend ikiwa karibu na nyumba, mbaya zaidi nguzo ipo kwenye kimwinuko ikiface nyumba na wataalam wenu walikuja kuhakikisha na kwenye taarifa yenu wameeleza jinsi nguzo inavohatarisha maisha ya wakazi katika nyumba husika lakini siku mnaishia kupromice mnakuja mnakuja kuanzia kutolewa kwa taarifa April 1 na mafundi kufika within 2days kushuhudia na kuiandikia taarifa.

Namba ya taarifa ni 0135 nyumba ipo eneo la mbezi kibanda cha mkaa. Jaribuni kutofautisha taarifa za kuzuia hatari na taarifa za marekebisho and prioritize them. Na mvua hizi ni risk zaidi
 
Huduma bora kwa Tanesco ya Tanzania au ya nchi gani?
Napenda kuwapa pongezi kwa huduma zenu bora , namaswali mawili kwenu (1) ningependa kujuwa viwango vya malipo ya umeme vinakwaje mfano mimi natumia unit 65 kwa mwezi na anae tumia unit 80 wote ni sawa.
 
Hongereni Tanesco kwa kuanzisha mfumo mpya wa kufanya maombi ya umeme mtandaoni.

Lakini rekebisheni kwenye kipengele Cha kuulizana majina ya kati ya mama na taarifa nyingine binasfi.

Kingine kama huna kitambulisho Cha taifa/NIDA uwezi homba umeme, si Kila mtanzania ana namba ya NIDA.

Rekebisheni hapo Kila mtu ilimradi ana kitambulisho chochote halali awezi kupatiwa huduma ya umeme.
 
Mimi niwape pongezi kidogo. Huku mitaa ya kigamboni toangoma mmejitahidi hajmakata kipindi cha mvua hizi za uchwara. HONGERENI SANA.
 
Ibrahim Juma nipo Wilaya ya Newala, namba ya cm 0719496951.

Kuna tatizo kweny nyumba yangu, umeme mdogo taa zote na vifaa ningine havifanyi kazi, jirani zangu wote umeme upo vizuri.

Pia mita inatoa mwanga wa bluu then inazima, haiwaki taa ile nyekundu.
 
Ibrahim Juma nipo Wilaya ya Newala, namba ya cm 0719496951.

Kuna tatizo kweny nyumba yangu, umeme mdogo taa zote na vifaa ningine havifanyi kazi, jirani zangu wote umeme upo vizuri.

Pia mita inatoa mwanga wa bluu then inazima, haiwak taa ile nyekundu.
#TANESCO
 
Nyie jamaa majiendeshaje kibiashara wakati watu wanalipia umeme wenu kwa zaidi ya miezi miwili na hamuwafungii umeme? kungekua na mshindani mngefanya hivyo? imagine watu wamelipa hela zao tena wamelipa kwa gharama mpya wanambwela mbwela miezi kadhaa no service na wala hawahitaji nguzo wengi wao
 
TANESCO DODOMA JIJI MNAHUJUMIWA NA KISHOKA MWENYE NAMBA HII 0785675861..ameisajili kwa jina la mwanamke ila yuko na watu nyuma wasio waaminifu ambao humtuma kuunganisha umeme pasipo fuata taratibu,kuunga kuunga waya vipande vipande kwenye nguzo ambao hatari kwa nyumba za watu..Nguzo kuwekwa hovyo hovyo

pia watu wengi wametapeliwa baada ya kuwaletea nguzo kinyume na taratibu na kusababisha watu hao kushindwa kuunganishiwa umeme wanapoenda kulipa gharama za mita..(maana huwachangisha fedha na pia huwashawishi kwamba wataungiwa mapema huduma) kawaliza wengi kata ya chidachi,mkonze na mpunguzi
inaonekana kuna kikundi kipo nyuma yake
MKIMWEKEA TEGO MTAMKAMATA MAPEMA MNO SABABU ANAPENDA SANA HELA
 
Back
Top Bottom