Ndugu Mteja!Siku hizi mbona mnakata tu umeme jamani kama leo kutwa nzima daa!
Ndugu Mteja
Tumekupigia simu kwa namba iliyopo kwenye taarifa yako haipatikani, Tafadhali tujulishe namba ya kuwasiliana na wewe kwa huduma bora
Ahsante
TANESCO mimi ni mkazi wa mwanza wilaya ya nyamagana mtaa wa mwananchi nahudumiwa na kituo chenu cha nyakato.
Tangu tarehe 5 June nimetoa taarifa ya emergency ya nguzo iliyooza na imedondoka, bahati nzuri ipo karibu na mti kwahiyo imeegemea mti ndio maana haijafika chini, namba ya taarifa ni 0707.
Mafundi walikuja tarehe 8 June wakaiangalia angalia then wakaniambia wataibalisha, ila ikipita wiki kama itakua bado hawajaibadilisha niwakumbushe kwa kutoa tena taarifa.
Bahati mbaya kweli wiki ilipita na nguzo haikubadilishwa nikatoa tena taarifa tarehe 18 June, simu alipokea mdada akaniambia taarifa imefika na itafanyiwa kazi.
Tangu siku hiyo sijaona fundi yeyote wa tanesco na nguzo bado inaning'inia.
Tarehe 6 August nikatoa tena taarifa kwenye banda la tanesco nanenane, nikiwa hopo bandani wahudumu walipiga simu kwenye kituo chenu na kuulizia taarifa yangu. Taarifa yangu ilikuepo na taarifa ya mafundi waliokuja kuiangalia nguzo pia ilikuepo, nikaahidiwa tena kwa mara ya tatu kua tatizo litashughulikiwa leoleo.
Hadi nimeamua kupost hapa kwenye thread yenu ni kwamba tatizo halijashughulikiwa na mbaya zaidi nguzo inazidi kuinama. Maybe hadi patokee janga ndio mtaibadilisha.
Ni kitu cha ajabu sana mtu unatoa taarifa ya emergency mara zaidi ya tatu halafu inapita miezi almost miwili bila tatizo kutatuliwa.
Tafadhali TANESCO kuweni wawajibikaji shughulikieni hili swala.
Nafuta hii comment yangu ya kutoa shukrani kwasababu mmenikera.TANESCO asante sana kwa kushughulikia swala langu! leo mafundi wenu wamenipigia na wamekuja kubadilisha nguzo japokua bado hawajafunga waya ila nina matumaini kesho watakamilisha kazi.
@TANESCO hili ombi languTANESCO TANESCO
Kilimanjaro Wilaya ya rombo kuna shida gani mbona
Mnatufanyia hivi wateja wenu
Nmelipia kuunganishiwa umeme tangu tarehe 25 mwez wa Tatu mwaka 2022 Lakin cha ajabu mpaka Leo
Umeme cjaunganishiwa jaman
Mkoa: Kilimanjaro
Wilaya: Rombo office ya tarakea tanesco
Jina : Aristidis S Shirima
Namba +255745140560
Hii n kama kubadilisha vocha iweNilitaka kumnunulia mteja wangu umeme badala ya 1000 nikamnunulia 10,000 naomba kujua kama naweza kubadilisha hizo token kwenda kwenye mita nyingine au kurudisha pesa.
Duuuuh changamoto kweli kweliHii n kama kubadilisha vocha iwe
Pesa uitoe ngumu Sana Kwa hawa jamaa
TANESCO Kibaha, bado tunasubiri nguzo Mwanalugali-Kwa niaba ya wakazi wa Mwanalugali (kiwanja cha hisia Kali), tunashukuru Menejiment ya TANESCO Makao Makuu na TANESCO Mkoa wa Pwani,hususani Meneja wa TANESCO Kibaha.
-Siku moja baada ya idara ya huduma kwa wateja Makao Makuu kupokea taarifa yetu na kuahidi kuifanyia kazi , utekelezaji wake tumeuona.
-Tunatoa shukrani kwa Management ya TANESCO Kibaha kwa kutuma mafundi kuja kutandaza nyaya kwenye nguzo tisa ambazo,zilisimikwa tarehe 13July2022.
-Wananchi wa Mwanalugali (kiwanja cha hisia Kali) tunashukuru kwa kusikia kilio chetu cha muda mrefu.
Lakini, Mradi wa Mwanalugali (kiwanja cha hisia Kali) ,ulikuwa unahitaji nguzo 15
- lakini kwa kuwa tarehe 30.06.2022 wakati wa kufunga mwaka Shirika lilikuwa na nguzo chache site, Mradi huu ulipatiwa nguzo 9 kwa kuanzia.
-Wakazi wa Mwanalugali (kiwanja cha hisia Kali) tunaomba Management ya TANESCO kumalizia nguzo 6 zilizosalia.
-Vifaa vingine vilibaki,labda kama vilihamishwa kupelekwa site nyingine.
-itapendeza kama nguzo zilizosalia zitaletwa na kujengwa,
- Mwezi September 2022 wakazi wa Mwanalugali tuje kulipia service line ya shs320,960.
-Kwa mara nyingine tena, wakazi wa Mwanalugali tunashukuru Management ya TANESCO kwa huduma nzuri. Mwenyezi Mungu awabariki.
Ombi
1). Tunaomba Manejiment ya TANESCO Makao Makuu, Mkoa wa Pwani na Kibaha kuleta nguzo zilizosalia tunaamini,hili lipo chini ya uwezo Regional Manager Kibaha
2). Menejiment ya TANESCO Kibaha,wapitie michoro ya mradi huu wa Mwanalugali (kiwanja cha hisia Kali).
3). Regional Manager Pwani, kama suala letu, lipo nje ya uwezo wako,tufikishie kwenye Mamlaka husika,
NB: Projects has always the time frame to finish.it is high time this project is brought to an end.
Kama ulivyosema hizo ni tetesi na zitaendelea kuwa tetesi, Bahati nzuri Juzi saa3 kamili nilifuatilia hayo mahojiano, January Makamba alikuwa anafafanua anasema kwamba serikali kwa wastani inamgharamia kila mtu sh. Laki8 kupata umeme, yani ukiona umeme umewaka kwako ujue serikali imetumia laki8 ili wewe kupata umeme, alivyochanganua hiyo laki8 alisema kwamba ule waya ambao unafungiwa kwako kwa mita moja serikali inaununua 15,000 na minimum akasema wengi ni mita30 ina maana 30×15,000=450,000.Kuna tetesi kuwa kuunganishiwa umeme kuanzia tarehe 10/9/2022 bei itakuwa 800,000/=. Kuna ukweli wowote?
Kweli TANESCO mwezi wa tatu huu nasubiri control number nilipie na nikipata control number kuna miezi mingi tu ya kusubiri kuwekewa umeme uwake.Ndugu mteja, Tafadhali tujulishe tatizo ni nini, Wilaya gani na namba ya ombi/simu kwa hatua zaidi
Ndugu Mteja, Tafadhali onesha namba ya ombi au namba ya simu uliyofanyia maombi ya kuunganishiwa umeme kwa hatua zaidiKweli TANESCO mwezi wa tatu huu nasubiri control number nilipie na nikipata control number kuna miezi mingi tu ya kusubiri kuwekewa umeme uwake.
300622-0987Ndugu Mteja, Tafadhali onesha namba ya ombi au namba ya simu uliyofanyia maombi ya kuunganishiwa umeme kwa hatua zaidi
TANESCO