Ni wiki sasa na siku kama tatu hivi hapa DSM,ubungo maeneo ya external,riverside,mabibo,NIT,mansese na njia ya kuelekea kimara kuna shida sana ya umeme.

Usipokatika jioni basi utakatika asubuhi. Au kuna matengenezo yanaendelea ambayo hayana taarifa kwa umma?
 
Tanesco mbna mnakata umeme bila taarifaa dharau hizooo
Ndugu Mteja!
Tunafurahia kukuhudumia, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora
Jina
Namba ya simu
Mkoa
Wilaya
Eneo
Namba ya meter
Tatizo
makao makuu 0748550000
 
Kwan leo wanekata tz nzima nn???? Au wanatuhamisha kijanjaa
Habari ndugu mteja
Shirika linaomba radhi kwa adha iliyojitokeza kutokana na kukosekana kwa umeme. Jitihada zinaendelea ili kuboresha huduma zetu.
TANESCO Huduma Kwa Wateja
SIMU: 0748 550000
 
Tabora nina wiki sasa kuna mgao wa umeme wa hatari bila hata ya notice, tatizo nini,
 
Habari ndugu mteja
Shirika linaomba radhi kwa adha iliyojitokeza kutokana na kukosekana kwa umeme. Jitihada zinaendelea ili kuboresha huduma zetu.
TANESCO Huduma Kwa Wateja
SIMU: 0748 550000
Mshatudharau sana waTz!
Hili tangazo uchwara linatakiwa kutolewa baada ya tukio au kabla?
 
Habari ndugu mteja
Shirika linaomba radhi kwa adha iliyojitokeza kutokana na kukosekana kwa umeme. Jitihada zinaendelea ili kuboresha huduma zetu.
TANESCO Huduma Kwa Wateja
SIMU: 0748 550000
TANESCO Kuomba radhi ni jambo moja lakini kutupatia taarifa ya kwanini kumekuwa na hali hii ni njambo lingine hivyo tunaomba taarifa ya kwanini hali hii imeanza kujirudia tena?
 
na hapo maintanance imekamilika na mabwawa yamejaa maji sijui sasahivi watakuja na kisingizio gani.
 
Muwe mnaotoa taarifa rasmi kwenye kurasa zenu official juu ya katizo la umeme kuliko kukataa kinyemela kama wezi.
 
Ndugu Mteja!
Tunafurahia kukuhudumia, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora
Jina
Namba ya simu
Mkoa
Wilaya
Eneo
Namba ya meter
Tatizo
makao makuu 0748550000
Nataka kuunganishiwa umeme mkoani Kilimanjaro maeneo ya vijijini Marangu
 
Nataka kuunganishiwa umeme mkoani Kilimanjaro maeneo ya vijijini Marangu
Ndugu Mteja!
Tunashukuru kwa kuwasiliana na TANESCO Huduma kwa Wateja, Tunakujulisha kuwa sasa TANESCO imekurahisishia maisha ya wewe kuweze kufanya maombi ya kuunganishiwa umeme kwa kutumia mfumo bora wa Nikonekt popote ulipo na wakati wowote, Unaweza kufanya maombi kwa njia zifuatazo:
- Nikonekt.tanesco.co.tz
-Nikoket App (Ipo Play store na Apple store)
- Kubofya *152*00#
-Kwenye ofisi za TANESCO

Kwa Maulizo au msaada wowote tafadhali wasiliana na kituo chetu cha huduma kwa wateja kwa namba 0748550000
TANESCO Huduma kwa Wateja
Makao Makuu
^SK
 
Nataka kuunganishiwa umeme mkoani Kilimanjaro maeneo ya vijijini Marangu
Zifuatazo ni gharama halisi za kuunganishiwa umeme kuanzia tarehe 5/01/2022
• Gharama za kuunganisha umeme mjini ndani ya mita 30 kwa mteja wa njia moja kutoka kwenye miundombinu ya umeme shilingi 320,960/=,
• Mteja wa njia moja ndani ya mita 70 kutoka kwenye miundombinu ya umeme shilingi 515,618/=,
• Umbali wa njia moja ndani ya mita 120 kutoka kwenye miundombinu ya umeme shilingi 696,670/=
• Aidha, gharama za kuunganisha umeme mjini ndani ya mita 30 kwa mteja wa njia tatu kutoka kwenye miundombinu ya umeme shilingi 912,014/=,
• Mteja wa njia tatu ndani ya mita 70 kutoka kwenye miundombinu ya umeme shilingi 1,249,385/=,
• Umbali wa njia tatu ndani ya mita 120 kutoka kwenye miundombinu ya umeme shilingi 1,639,156/=.

Zingatia
Gharama ya kuunganisha umeme vijijini kwa wateja wa njia moja ni shilingi 27,000/=

Gharama hizi ni kama ilivyoelekezwa na EWURA.

NB: Gharama zote zimejumuisha Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) 18%
TANESCO Huduma kwa Wateja
SIMU : 0748550000. ^ SK
 
Hivi inachukua mda gani kwa mtu kuunganishiwa umeme hasa wa nguzo moja ...akisha kamilisha malipo na pia ni hatua zip atafanya iwapo km kutoa ripoti katoa lakini hawajamfungia umeme mwezi na nusu sasa.tafadahari nijubu admin
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…