TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
hivi ni kweli kahama hakuna nguzo tangu mwezi wa 2 au mnatuzungusha tutoe rushwa
na kuna matapeli wanajifanya waajiriwa wa tanesco wanapita kutaka kututapeli inaonekana wanashirikiana na watu wa ndani ya tanesco
kweli nguzo hakuna
nguzo moja shilingi laki 3 bado mnatuzungusha
mlaaniwe
why mlipokea hela yangu na nguzo hakuna
Nguzo Moja laki tatu?
Ulilipa kwa control namba au ulimpa mtu mkononi akurahisishie upatikanaji maana mie najua kihalali bei ya nguzo ni laki Tano +
 
Naomba mnijuze (yeyote mwenye kujua aseme siyo lazima TANESCO)

Hivi nikihitaji umeme kijijini na nguzo haijanifikia bado je ninaweza kutuma maombi? Na nasikia nguzo inahitajika kulipiwa je nitahitajika kulipia kiasi gani ili niwekewe nguzo (maana nimeambiwa mpaka niwe mita 30 kutoka ilipo nguzo sasa mimi nilipo ni mita wastani wa 60-70, hazizidi mita mia moja)
 
Naomba mnijuze (yeyote mwenye kujua aseme siyo lazima TANESCO)

Hivi nikihitaji umeme kijijini na nguzo haijanifikia bado je ninaweza kutuma maombi? Na nasikia nguzo inahitajika kulipiwa je nitahitajika kulipia kiasi gani ili niwekewe nguzo (maana nimeambiwa mpaka niwe mita 30 kutoka ilipo nguzo sasa mimi nilipo ni mita wastani wa 60-70, hazizidi mita mia moja)
Maombi kutuma ni Bure
Ukishatuma watakuja surveyor ata survey Bure
Ndani ya mita 30 kwa kijijini ni 27,000
(Ndani ya mita 80 ) inamaana nguzo Moja mita 50 + waya kutoka kwenye nguzo kuja kwako 30m inagharimu 519000 itategemea ila isikate kiwanja Cha mtu
 
Maombi kutuma ni Bure
Ukishatuma watakuja surveyor ata survey Bure
Ndani ya mita 30 kwa kijijini ni 27,000
(Ndani ya mita 80 ) inamaana nguzo Moja mita 50 + waya kutoka kwenye nguzo kuja kwako 30m inagharimu 519000 itategemea ila isikate kiwanja Cha mtu
Nashukuru sana, hivi hiyo nguzo nikishailipia itakuwa hakuna mtu mwingine kuchukulia umeme hapo kwenye nguzo yangu au watanirefund au ndo basi tena watapata mserereko?
 
Nashukuru sana, hivi hiyo nguzo nikishailipia itakuwa hakuna mtu mwingine kuchukulia umeme hapo kwenye nguzo yangu au watanirefund au ndo basi tena watapata mserereko?
Hakuna utaratibu wa kumchangisha jirani
Kwa mfano Kuna Mzee mmoja kikiji Fulani kanunua transfoma yake kwa ajili ya kuazisha mashine na ghala la nafaka lakini jirani yake akavuta kwa hiyo hiyo transfoma kwa 27000
Sembuse na wewe nguzo Moja
USHAURI
Mshirikishe jirani mpige hesabu mgawe kwa idadi yenu then mmoja mumpe hiyo Hela aesabike kama kailipia yeye ili mzani uwe sawa asionekane wa kulaliwa na wengine mnalipia gharama ya meter
 
Kuna swala la kubadilisha mita Dareslam,,,,,
Inaonekana mafundi wenu wanafanya ni mradi sasa wa kuwatishia watu kwa kuwaeleza mita zimechezewa na wanaomba wapewe pesa ili wafunge mpya la sivyo wawapeleke watu mahakamani!!
Na wanawatisha watu bila huruma!!
Pitieni maeneo ambayo mita zilitakiwa kuweka na hawajaweka siku ya leo kisa wanalazimisha wapewe pesa!!
Dau lao ni milioni moja na nusu Hadi laki nane!!
Tanesco fanyieni kazi hilo ,,, watendaji wenu wanamchafua mama
 
Hawa TAANESIKO walisema ikifika Julai wataweka mfumo wa ukilipa bill inaingia moja kwa moja
 
Tanesco ni majizi
Ni baadhi ya watendaji wasio waadilifu,,,, kama siku ya tarehe 08/07/2024 maeneo ya Kimara walifanya vitu visivyo vya kiungwana na vya hovyo sana!! Wanawachekecha watu wasio na uelewa kwenye madude yao na kuomba wapewe 1.5mil, laki 8, laki 3 n.k so shame!!
Na baadhi ya nyumba hawajaweka mita wakisubiri pesa walizoomba!!
Watendaji wachache wasio waadilifu huchafua hizi taasisi!!
Watendaji mlioko maofisini fatilieni nyumba ambazo hawajawekewa mita, na waulizeni kwa nini hawajatolea taarifa ijapokuwa changamoto nyingine ni kubebana kwenye maofisi!! Ila wanachafua serikali kwa ujumla pamoja na taasisi yenu Tanesco-meneja Kimara na maeneo mengine tazameni hawa vijana wenu!!!
 
Kuunganishiwa umemw ni bei gani ? Kwa vijijini na mijini pia umeme unatarajiwa kupanda garama za kuunga au kupungua?
 
Halafu mbona kama mmeanzisha mgao wa kimya kimya? Au mabwawa mmeyatoa maji tena.

Hii nchi ngumu jamani, kila kitu hakiendi. Tuko kama jehanamu
 
swala la POWER-CUT kwenye metre za Wasion.LUKU haiingii.
Suluhisho lake ni nini?Kwanini msituelekeze tunarestet vipi--mpaka tuwapigie kila saa
 
Tanesco imekua kero sana kwa wateja wenu. kuanzia tarehe 1 mpaka 7 July 2024 kumekua na sintofahamu kubwa sana unaponunua umeme unapewa nusu ya ile pesa ulionunua, yaani mfano ukinunua umeme wa ths 5000/= ambapo ulitakiwa upate unit 14 utapata nusu yake yaani utapata unit 7. Ukiwasiliana na huduma kwa wateja wanakwambia kuna tatizo(error) katika mita yako ambayo inaonyesha kua mita yako imechezewa hivyo imesababisha deni lisilopungua chini ya tsh 1,000,000/= na kuendelea. Leo tarehe 15 July 2024 hata kama kweli mteja ulichezea mita katika matumizi ya kawaida ya yumbani kweli unaweza ukatumia umeme wa kiasi cha tsh milioni na ushee kwa muda wa siku 10 mpaka 15?.
Wanasema kuna wakaguzi wa mita/luku walipita na kuacha barua inayoeleza juu ya deni hilo ilihali wakaguzi hao hawajonekana wala barua hazijapokelewa kutoka Tanesco.
Operation kama hii kutoka Taasisi kubwa kama hii Tanesco inatekelezwa vipi bila kutoa taarifa wa wateja weke?

Note: Hili tatizo limekua kubwa hasa mkoa wa kinondoni( Kawe, Kijitonyama makumbusho N.K....) Tanesco pitieni Mifumo yenu vizuri, tunaamini mpo katika maboresho ya mifumo na lengo ni kweli 'KUANGAZA MAISHA YA WATANZANIA' ila kwa mabambiko haya ya madeni kwa wananchi ni kama mnaenda kinyume na kauli mbiu yenu.
NAWASILISHA...
 
swala la POWER-CUT kwenye metre za Wasion.LUKU haiingii.
Suluhisho lake ni nini?Kwanini msituelekeze tunarestet vipi--mpaka tuwapigie kila saa
Suluhisho la wassion jitahidi usiishiwe kabisa umeme hasa wassion toleo la kwanza linasumbua sana
Maana ukiishiwa umeme Kuna kuwa na changamoto ya kupoteza mawasiliano kati ya meter juu ya nguzo na remote Yako JITAHIDI USIISHIWE UNIT
 
Shirika la Umeme Tanzania - (Tanzania Electric Supply Company Limited - TANESCO), Tunaomba mtupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri kupitia huu uzi nasi tutawajibu.

Tunawaomba mzingatie yafuatayo ili kurahisisha ufafanuzi na ufumbuzi wa tatizo au taarifa husika;

1. ENEO HUSIKA

(Mnaweza kuwa eneo moja lakini mnahudumiwa na transfoma au njia ya kusambaza umeme (feeder) tofauti)

2. NAMBA YA SIMU

(Wakati mwingine umeme upo kote isipokuwa kwako hivyo na rahisi kuwasiliana na wewe)

3. KARIBU NA NINI

(Kuna alama vitu au watu mashuhuri karibu na eneo lako mfano ofisi ya Serikali ya Mtaa, Mahakama, Kituo cha Polisi nk)

4. JINSI YA KUFIKA MAKAZI YAKO

(Toa ufafanuzi wa jinsi ya kufika makazi yako,chukulia unamuelekeza mtu ambaya hajawahi kufika kabisa)

5. MKOA,WILAYA NA KITONGOJI/KIJIJI

(Taarifa hii ni muhimu sana kusaidia kubaini eneo husika lipo wapi kwani yapo maeneo yanayofanana kwa majina lakini yapo Mikoa tofauti mfano Magomeni ipo Dar es Salaam na Mkoa wa Mtwara pia.)

6. KAMA NI TATIZO LA MITA NINI KINATOKEA UKIWEKA UMEME

(Kila mita ina ujumbe wake unaoashiria kitu fulani hivyo kubainisha ujumbe kunamsaidia mpokea taarifa kukupatia maelezo sahihi mfano mita namba 24339173921 inaonyesha error 77)

7. KAMA NI KUSHINDWA KUNUNUNUA UMEME UNAPATA UJUMBE GANI NA UNANUNUA KWA NJIA GANI

(Ujumbe huu ni muhimu sana kuweza kubaini chanzo cha tatizo pamoja na njia iliyotumika kununulia umeme mfamo Mpesa, Tigopesa, Maxcom nk)

TUNAENDELEA KUWASIHII WATEJA WETU KUZINGATIA UTOAJI WA TAARIFA SAHIHI NA FASAHA KWA HUDUMA BORA ZAIDI KUTOKA TANESCO.

ENDELEA KUFURAHIA HUDUMA BORA KUTOKA TANESCO

Vilevile pitia threads hizi kupata Maelezo ya ziada;

LUKU:Mfumo wenye Tija kwa Wateja na TANESCO

Fahamu mita za LUKU zinazofungwa majumbani

Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

Kw mawasiliano Kituo cha Miito ya Simu (+255) 22194400 or (+255) 768 985 100 Mitandao ya kijamii Tanescoyetu (@tanescoyetu) | Twitter Facebook: Tanesco Yetu

HAPA CHINI NI NAMBA ZA SIMU ZA MIKOA

Ofisi ya Mkoa wa Mbeya Simu ya Mkononi (+255) 757 529 380 ya Mezani (+255) 252 504 219

Ofisi ya Mkoa wa Ilala Simu ya Mkononi (+255) 784 768 586 ya Mezani (+255) 222 133 330

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kusini (Magomeni) Simu ya Mkononi (+255) 715 271 461/ (+255) 784 271 461

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kaskazini (Mikocheni) Simu ya Mkononi (+255) 784 768 584 / (+255) 716 768 584 ya Mezani (+255) 222 700 367/ (+255) 222 701 602 / (+255) 222 774 098

Ofisi ya Mkoa wa Temeke Simu ya Mkononi (+255) 712 052720 / (+255) 758 880155 / (+255) 732 997361

Ofisi ya Mkoa wa Pwani Simu ya Mkononi (+255) 78 5122020 / (+255) 65 7108782ya Mezani (+255) 23 2 402 386

Ofisi ya Mkoa wa Arusha Simu ya Mkononi (+255) 75 8 174 343 Mezani (+255) 272 506 110

Ofisi ya Mkoa wa Tanga Simu ya Mkononi (+255) 658 122 412/ (+255) 687 677 667 Mezani (+255) 27 2 646 779

Ofisi ya Mkoa wa Kilimanjaro Simu ya Mkononi (+255) 765 397 925/ (+255) 682 771 310 Mezani (+255) 272 755 007/8

Ofisi ya Mkoa wa Manyara Simu ya Mkononi (+255) 689 795 599 / (+255) 75 9 534 130 Mezani (+255) 272 530 590

Ofisi ya Mkoa wa Mwanza Simu ya Mkononi (+255) 759 777 786 / (+255) 687 910 202 Mezani (+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

Ofisi ya Mkoa wa Geita Simu ya Mkononi (+255) 744 085 696 Mezani (+255) 28 2520330

Ofisi ya Mkoa wa Kagera Simu ya Mkononi (+255) 78 5 787 898 / (+255) 75 3 120 701 Mezani (+255) 282 220 061

Ofisi ya Mkoa wa Mara Simu ya Mkononi (+255) 762 165 087 / (+255) 732 985 672

Ofisi ya Mkoa wa Simiyu Simu ya Mezani (+255) 282 700 180

Ofisi ya Mkoa wa Dodoma Simu ya Mkononi (+255) 782 161 643 Mezani (+255) 262 321 728

Ofisi ya Mkoa wa Morogoro Simu ya Mkononi (+255) 68 4889272 / (+255) 65 4829046 Mezani (+255) 232 613 501/2

Ofisi ya Mkoa wa Singida Simu ya Mkononi (+255) 71 4 477 445 / (+255) 732 960 924 / (+255) 689 373 757 Mezani (+255) 262 502 133

Ofisi ya Mkoa wa Tabora Simu ya Mkononi (+255) 786 558 510 / (+255) 763 162 868

Ofisi ya Mkoa wa Shinyanga Simu ya Mkononi (+255) 754 521 070 Mezani (+255) 28 2762120

Ofisi ya Mkoa wa Kigoma Simu ya Mkononi (+255) 78 3720598 Mezani (+255) 28 2802668

Ofisi ya Mkoa wa Katavi Simu ya Mkononi (+255) 68 8345200

IMETOLEWA NA:- Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makauu.

NAMBA ZA SIMU ZA MADAWATI YA DHARURA YA TANESCO MIKOA YOTE

1. Ilala

0222133330/ 0784 768586/ 0715 768586.

2.Kinondoni Kusini (Magomeni)

0784271461/ 0715271461

3. Kinondoni Kasikazini(Mikocheni)

0784 768584/ 0716 768584

4. Temeke

0222138352/ 0732 997361/ 0758881055/ 0712 052720

5. Pwani
078 5122020/065 7108782/023 2402386

6. Mbeya
0759 777781/0787 023422


7.Arusha
0758174343/
0622612501/
+255 27 2506110

8.Tanga
0658 122 412/0687 677 667/ 027 2646 779

9. Kilimanjaro
0765 397 925/0682 771 310/ (+255) 272 755 007/8

10 Manyara
0689 795 599/ 0627938951

11. Mwanza
0759 777 786/0687 910 202/
(+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

12. Geita
0744 085 696/(+255) 28 2520330

13.Kagera
078 5 787 898 / 075 3 120 701/(+255) 282 220 061

14.Mara
0788 950 688/
028 262 2020/
0762 165 087

15.Simiyu
+255 282 700 180/0626383440/0745044072

16. Dodoma
0782 161 643/(+255) 262 321 728

17. Morogoro
068 4889272 /065 4829046/ (+255) 232 613 501/2

18 Singida
071 4 477 445 /0732 960 924 / 0689 373 757/(+255) 262 502 133

19. Tabora
0786 558 510 /0763 162 868

20. Shinyanga
0754 521 070/(+255) 28 2762120 /
0783 521 070

21. Kigoma
078 3720598/(+255) 2988226

22. Katavi
0688345200

23. Rukwa
0252161120/0768879813
24. Songwe
0684 611716/0763 430381.

25. Ruvuma
0252602281/0763 194 979/0787 758 986

26. Njombe
0744703988

27. Mtwara:
0789 999942/023 2333902

28. Iringa 0262702019/0739203015

29. Lindi
0752518247/0685692786


Kituo cha Miito ya simu/Call Centre Makao Makuu

0768 985 100/0222194400

Facebook
www.facebook.com/tanescoyetu

Twitter
www.twitter.com/tanescoyetu

Tovuti
www.tanesco.co.tz

Barua pepe
Customer.service@tanesco.co.tz

Imetolewa na:
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu
Je TANESCO huwa mnapokea pesa bila kutoa risiti? Kule Wilaya ya RUNGWE,mkoa wa mbeya,kata ya Kiwira ,kijiji kinaitwa ilundo,kuna eneo linaitwa ISOKO,wananchi wanachangishana shilingi laki 5 tano,wanapewa jamaa wa TANESCO wanapeleka nguzo na umeme unaunganishwa! Hizo pesa wanasema ni za nguzo,lakini hawatoi risiti! Hebu tupeni maelezo kamili! Kwani nasikia mtu wa kule kama hakuchanga hiyo laki 5 hawezi unganishiwa umeme hata kama nguzo ipo nyumba ya jirani,masharti kwanza apeleke laki 5 kwa balozi ndipo aunganishwe umeme
 
Hizi mashine za kuwekea umeme ukishanunua zinasumbua sana wakati unaweka nielekee wapi kupata msaada zaidi niko ilala
 
Back
Top Bottom