TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Siku hizi hata kutangaza kwamba kuna mgao wanaona aibu,

Ila wenye akili tunajua. Kagombana na wezi huku waaminifu hawajawaandaa!! Ila utasikia kuna watu wanahujumu!!
 
Huku Mwanza UMEME hakuna tangu asubuhi na hatujapata maelezo yoyote pia MAJI imekuwa ni kawaida kukatika kila siku wakati Ziwa tunaliona hapo na hakuna maelezo yoyote kwa nini hakuna maji, yaani hizi taasisi mbili ni pasua kichwa sijui hivyo viburi wanavitoa wapi..!!
Hadi kwa mlompa kura mkulu? Amakweli itafika muda tutashea maumivu tu.
 
Tumeshafeli ndo maana Muvi ni bandarini kusahaulisha ni jambo la muda tuu ila wenyewe itatusumbua 2018 up 2019 mara kumekucha 2020
 
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)

*TAARIFA YA KUANZA KUREJEA KWA UMEME *

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake kuwa umeme umerejea katika Mikoa yote Saa 07:11 Mchana isipokuwa Mkoa wa Mbeya kutokana na hitilafu iliyopo katika njia ya Mufindi.

Tutaendelea kutoa taarifa zaidi.

Shirika linaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza.

Tafadhali usishike wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka

Kwa mawasiliano zaidi

Tovuti: www.tanesco.co.tz

Mitandao ya Kijamii
www.facebook/tanescoyetultd
twitter.com/

Imetolewa na:-
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu

01/12/2017
Pia mtulipe kutokana na huo usumbufu.... Sio kuomba radhi kila siku.... Maana hamkutupa taarifa mapema.... Sisi mbeya ususani kyela umeme unarudi kama tulivyo uzoea yan kukatika sa mbili hasubuhi na kurudi kuanzia sa moja jioni na mda mwingine sa tano usiku ni mwezi sasa.

Je hili tatizo ni mwisho leo? Na kama likitokea tuwafanyeje? Na kwanini hamtupi taarifa mapema walau tuwe na subira ya muda flani..
 
Ni taarifa ipi ambayo hujaipata. Tanesco wametoa taarifa za hitilafu za umeme wewe unasema huna taarifa. Jitahidi kufuatilia taarifa sahihi katika ofisi za mkoa wako.
Tuna redio na TV niwajibu wao kututangazia kumbukua hii huduma sio bure tunatoa pesa zetu.... Na tumegharamia na bado pesa zetu wanachukua....

Ile dhana ya mteja ni mfalme kwa tanesco tuitoe? Alafu we ni nani huko tanesco mbona unapenda kujipachika kwenye nafasi za watu maana wao wanalipwa na wewe unalipwa kiasi gani? Je! Unakiwanda chochote kinachotumia umeme?
 
Mheshimiwa Mbunge wa Ilemela huu mgao wa jimboni kwako stuka, iweje buswelu nyamanoro nyakato pasiwe na umeme wiki ya tatu sasa, kila siku mchana hakuna umeme, sasa wachoma mageti waranda mbao wauza juice hawana kazi, zimebaki bar t

hebu dadisi chunguza kwanini ni ilemela tu ha
 
Mheshimiwa Mbunge wa Ilemela huu mgao wa jimboni kwako stuka, iweje buswelu nyamanoro nyakato pasiwe na umeme wiki ya tatu sasa, kila siku mchana hakuna umeme, sasa wachoma mageti waranda mbao wauza juice hawana kazi, zimebaki bar t

hebu dadisi chunguza kwanini ni ilemela tu ha

Na wewe Eddy acha ufala, hapa jukwaani kuna post zaidi ya tatu zote zinazungumzia tatizo la umeme nchi nzima, wewe unakuja kumuuliza mbunge kuhusu hizo sehemu tatu?
 
Na wewe Eddy acha ufala, hapa jukwaani kuna post zaidi ya tatu zote zinazungumzia tatizo la umeme nchi nzima, wewe unakuja kumuuliza mbunge kuhusu hizo sehemu tatu?
Ukabila mkuuu na ukwetu kwetu... Si wasukuma hao wanahisi kama umeme ni haki yao pekee maana nchi ni yao.. Wamejisahau sanaa.... Mwambie amfuate kwa office yake
 
Suala la umeme si kwamba lipo mwanza tuu ni kwamba kwa mikoa yote iliyounganishwa na grid ya taifa umeme unasumbua hakuna mgao ila ilitokea hitilafu katika msongo mkubwa wa umeme ndio maana umeme ulikuwa unasumbua..!!!
 
Sasa kama ni mgao iweje huku mgao mchana tu, wiki tatu sasa, situpeane kwa zamu, yapo maeneo hayaguswi kabisa na mgao mfano Isamilo mahina huko hamna mgao kwanini?
 
Suala la umeme si kwamba lipo mwanza tuu ni kwamba kwa mikoa yote iliyounganishwa na grid ya taifa umeme unasumbua hakuna mgao ila ilitokea hitilafu katika msongo mkubwa wa umeme ndio maana umeme ulikuwa unasumbua..!!!

Sio kwamba ULIKUWA ni bado USUMBUFU UNAENDELEA.
 
Suala la umeme si kwamba lipo mwanza tuu ni kwamba kwa mikoa yote iliyounganishwa na grid ya taifa umeme unasumbua hakuna mgao ila ilitokea hitilafu katika msongo mkubwa wa umeme ndio maana umeme ulikuwa unasumbua..!!!

Mkuu sio hitilafu ni zaidi ya hitilafu. Hili tatizo lina zaidi ya mwezi sasa na ukali wa mgao unazidi kushika kasi. Wewe umesikia tangazo jana kwamba ni hitilafu. Sio hitilafu kwani hili tatizo hata waziri alijitokeza kama wiki mbili zilizopita akihimiza Tanesco wamalize service ya mitambo yao mpaka mwisho wa mwezi huu.

Lakini kutokana na hali inayoondelea naona wanajichanganya maana mara wanasema ni hitilafu, huku waziri alisema ni service ya kawaida ya mitambo. Kutokana na lugha zao kutofautiana ni dhahiri kuna tatizo la msingi linalofichwa.
 
Yale magenereta ya SEMCO pale mwatex siwalisema yatawasha kanda ya ziwa sasa huu mgao unatoka wapi? Ni hujuma tu.
 
Mambo kama haya Chadema ndo yalipaswa kuyatolea matamko, lkn kwenye matatizo ya msingi ya watanzania Chadema hujificha, ila akikamatwa Heche polisi, hayo matamko utakayoyasikia sio ya Nchi hii
Eti matamko ndo yatamaliza matatizo tuliyonayo ikiwemo hili la Umeme? Unaota wewe. Mmebaki kuangalia kila kitu kwa jicho la ushabiki. Na bado, for you deserve all the shit.

Watu wengine sijui mnatumia nini kufikiri? Wewe endelea kukumbatia ccm, halafu ukisubiri chadema watoe matamko ili ccm irekebishe swala la umeme. There you go! Way to think! Mtanyoroshwa tu hadi mpate akili
 
Wakuu huu mgao wa umeme wa siri siri japo unaonekana kwa macho.. Nasema wa siri kwasababu huana maelezo ili watu tujipange kwa kununua ma generator.. Kwa mfano huku mbeya umeme ni kawaida kukatika sa mbili hasubuhi na kurudi sa tano usiku.. Ikumbukwe umeme kwa hii miaka ni muhimu sana kwa shughuli za viwanda vyetu vidogo vidogo kama saloon, welding n.k

Swali nnalo jiuliza ni nani wa kutumbuliwa kwa huu uzembe wa mgao wa umeme usio na kifani? Maana kama kutumbua kwenye sector ya umeme tumetumbua sanaaa hivi sahivi ni zamu ya nani!?

Na anayejua sababu ya umeme kukatika na huu mgao wa kutisha ni ipi?

nchi ya viwonder
Masasi laini ya mangaka haujawahi kuwaka masaa 24 hata kwa siku moja
 
Back
Top Bottom