TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
IMG-20171204-WA0001.jpg
 
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA

MABORESHO YA MIUNDOMBINU MKOA WA TEMEKE

Tunawataarifu Wateja wetu wa Mkoa wa Temeke kuwa, kutakuwa na maboresho ya miundombinu ya umeme kwa kufanya kazi za Kuhamisha njia ya umeme ya msongo mkubwa ili kupisha ujenzi wa barabara ya daraja la Mwalimu Nyerere, kubadilisha nguzo zilizooza, kuimalisha viunguo vya umeme na kukata miti iliyopita kwenye njia za msongo mkubwa wa umeme wa kilovolti 33, siku ya Alhamisi, Decemba 07, 2017 kuanzia saa 02.00 Asubuhi hadi saa 11.00 Jioni. Kutokana na maboresho hayo maeneo ya Vijibweni, Tungi, Kigamboni, Mjimwema, Kibada, Somangila, Kisarawe II, Kimbiji Pemba Mnazi, baadhi yamaeneo ya Toangoma na maeneo ya jirani yatakosa umeme

Tafadhali usishike waya uliokatika toa taarifa kupitia simu zifuatazo

Toa taarifa Dawati la dharura Mkoa waTemeke 0714485488, 0783360411, 0765654767 au Kituo cha miito ya simu namba 2194400 au 0768 985 100.

Tovuti:
www.tanesco.co.tz

Mitandao ya kijamii
www.facebook/twitter.com/tanescoyetu

Barua pepe:
customer.service@tanesco.co.tz

Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Imetolewa na: OFISI YA UHUSIANO,
TANESCO – MAKAO MAKUU.

Desemba 05, 2017
 
Kwani mnaona shida gani kutangaza kuna mgao rasmi? Kama ndio hali halisi tutangaziwe. TANESCO
 
Kinachoshangaza ni kwamba kila siku wanaboresha lakini matatizo hayaishi, huko viwandani tunaenda kwa kukatakata umeme hovyo hovyo.

Wekeni LUKU kwenye ofisi zote za serikali muweze kujiendesha. wakopaji wakiwa wengi tena wa mabilioni mtawezaje kuendesha shirika kwa pesa za walalahoi sisi.
 
Shirika la Umeme Tanzania - (Tanzania Electric Supply Company Limited - TANESCO), Tunaomba mtupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri kupitia huu uzi nasi tutawajibu.

Tunawaomba mzingatie yafuatayo ili kurahisisha ufafanuzi na ufumbuzi wa tatizo au taarifa husika;

1.ENEO HUSIKA

(Mnaweza kuwa eneo moja lakini mnahudumiwa na transfoma au njia ya kusambaza umeme (feeder) tofauti)

2.NAMBA YA SIMU

(Wakati mwingine umeme upo kote isipokuwa kwako hivyo na rahisi kuwasiliana na wewe)

3.KARIBU NA NINI

(Kuna alama vitu au watu mashuhuri karibu na eneo lako mfano ofisi ya Serikali ya Mtaa, Mahakama, Kituo cha Polisi nk)

4.JINSI YA KUFIKA MAKAZI YAKO

(Toa ufafanuzi wa jinsi ya kufika makazi yako,chukulia unamuelekeza mtu ambaya hajawahi kufika kabisa)

5.MKOA,WILAYA NA KITONGOJI/KIJIJI

(Taarifa hii ni muhimu sana kusaidia kubaini eneo husika lipo wapi kwani yapo maeneo yanayofanana kwa majina lakini yapo Mikoa tofauti mfano Magomeni ipo Dar es Salaam na Mkoa wa Mtwara pia.)

6.KAMA NI TATIZO LA MITA NINI KINATOKEA UKIWEKA UMEME

(Kila mita ina ujumbe wake unaoashiria kitu fulani hivyo kubainisha ujumbe kunamsaidia mpokea taarifa kukupatia maelezo sahihi mfano mita namba 24339173921 inaonyesha error 77)

7.KAMA NI KUSHINDWA KUNUNUNUA UMEME UNAPATA UJUMBE GANI NA UNANUNUA KWA NJIA GANI

(Ujumbe huu ni muhimu sana kuweza kubaini chanzo cha tatizo pamoja na njia iliyotumika kununulia umeme mfamo Mpesa, Tigopesa, Maxcom nk)

TUNAENDELEA KUWASIHII WATEJA WETU KUZINGATIA UTOAJI WA TAARIFA SAHIHI NA FASAHA KWA HUDUMA BORA ZAIDI KUTOKA TANESCO.

ENDELEA KUFURAHIA HUDUMA BORA KUTOKA TANESCO

Kw mawasiliano Kituo cha Miito ya Simu (+255) 22194400 or (+255) 768 985 100 Mitandao ya kijamii Tanescoyetu (@tanescoyetu) | Twitter Facebook: Tanesco Yetu

HAPA CHINI NI NAMBA ZA SIMU ZA MIKOA

Ofisi ya Mkoa wa Mbeya Simu ya Mkononi (+255) 757 529 380 ya Mezani (+255) 252 504 219

Ofisi ya Mkoa wa Ilala Simu ya Mkononi (+255) 784 768 586 ya Mezani (+255) 222 133 330

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kusini (Magomeni) Simu ya Mkononi (+255) 715 271 461/ (+255) 784 271 461

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kaskazini (Mikocheni) Simu ya Mkononi (+255) 784 768 584 / (+255) 716 768 584 ya Mezani (+255) 222 700 367/ (+255) 222 701 602 / (+255) 222 774 098

Ofisi ya Mkoa wa Temeke Simu ya Mkononi (+255) 712 052720 / (+255) 758 880155 / (+255) 732 997361

Ofisi ya Mkoa wa Pwani Simu ya Mkononi (+255) 78 5122020 / (+255) 65 7108782ya Mezani (+255) 23 2 402 386

Ofisi ya Mkoa wa Arusha Simu ya Mkononi (+255) 75 8 174 343 Mezani (+255) 272 506 110

Ofisi ya Mkoa wa Tanga Simu ya Mkononi (+255) 658 122 412/ (+255) 687 677 667 Mezani (+255) 27 2 646 779

Ofisi ya Mkoa wa Kilimanjaro Simu ya Mkononi (+255) 765 397 925/ (+255) 682 771 310 Mezani (+255) 272 755 007/8

Ofisi ya Mkoa wa Manyara Simu ya Mkononi (+255) 689 795 599 / (+255) 75 9 534 130 Mezani (+255) 272 530 590

Ofisi ya Mkoa wa Mwanza Simu ya Mkononi (+255) 759 777 786 / (+255) 687 910 202 Mezani (+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

Ofisi ya Mkoa wa Geita Simu ya Mkononi (+255) 744 085 696 Mezani (+255) 28 2520330

Ofisi ya Mkoa wa Kagera Simu ya Mkononi (+255) 78 5 787 898 / (+255) 75 3 120 701 Mezani (+255) 282 220 061

Ofisi ya Mkoa wa Mara Simu ya Mkononi (+255) 762 165 087 / (+255) 732 985 672

Ofisi ya Mkoa wa Simiyu Simu ya Mezani (+255) 282 700 180

Ofisi ya Mkoa wa Dodoma Simu ya Mkononi (+255) 782 161 643 Mezani (+255) 262 321 728

Ofisi ya Mkoa wa Morogoro Simu ya Mkononi (+255) 68 4889272 / (+255) 65 4829046 Mezani (+255) 232 613 501/2

Ofisi ya Mkoa wa Singida Simu ya Mkononi (+255) 71 4 477 445 / (+255) 732 960 924 / (+255) 689 373 757 Mezani (+255) 262 502 133

Ofisi ya Mkoa wa Tabora Simu ya Mkononi (+255) 786 558 510 / (+255) 763 162 868

Ofisi ya Mkoa wa Shinyanga Simu ya Mkononi (+255) 754 521 070 Mezani (+255) 28 2762120

Ofisi ya Mkoa wa Kigoma Simu ya Mkononi (+255) 78 3720598 Mezani (+255) 28 2802668

Ofisi ya Mkoa wa Katavi Simu ya Mkononi (+255) 68 8345200

IMETOLEWA NA:- Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makauu.

Vilevile pitia threads hizi kupata Maelezo ya ziada;


LUKU:Mfumo wenye Tija kwa Wateja na TANESCO

Fahamu mita za LUKU zinazofungwa majumbani

Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO
Mie naomba kujuzwa umeme single phase one km haufiki mana mie nmepimiwa ndo jibu nililopewa hilo, nmewaambia wanipe gharama nikaambiwa gharama ni kubwa zinaweza fika Mil 50 mara ninunue Transforma wafunge ndo umeme ufike. haikuniingia akilini kwa kwelii
 
Nimebadilishiwa tariff kwenda tariff 4 lkn namba nilizopewa kuongiza kabla ya token mita haikubali. Nifanyeje?

Vv
 
Mie naomba kujuzwa umeme single phase one km haufiki mana mie nmepimiwa ndo jibu nililopewa hilo, nmewaambia wanipe gharama nikaambiwa gharama ni kubwa zinaweza fika Mil 50 mara ninunue Transforma wafunge ndo umeme ufike. haikuniingia akilini kwa kwelii
Jina
Mkoa
Eneo
Namba ya simu
Tatizo
 
Habari zenu tanesco
Jamani mi toka jana naaingiza unit inasearch tu vile vimishale mwisho inaandika ERROR 17 sijui tatizo nini mnisaidie leo siku ya pili niko gizani.
 
Habari zenu tanesco
Jamani mi toka jana naaingiza unit inasearch tu vile vimishale mwisho inaandika ERROR 17 sijui tatizo nini mnisaidie leo siku ya pili niko gizani.
Tunaomba namba ya mita na namba ya simu
 
Namba ya mita na token ulizopewa tafadhali
Mita yake ni namba 24214169096
Namba alizopewa aingize ili ahamishwe tariff ni 4058 8557 7619 6863 2390 0157 2600 7881 3528 0953 .

Mita nyingine ni namba 24214169104. Namba zinazogoma ili aingizwe kwenye tariff nyingine ni 4041 4371 6933 6919 7977 6033 6564 4609 9654 9881.

Akiingiza hizo namba mita haisomi/hairespond, Akiingiza token baada ya kuwa ameingiza hizo namba bado mita haisomi
 
Naomba mawazo yenu kwa tatizo hili: natumia unit 8 kutwa.

Nina frigdge moja ndogo, taa energy saver kama 5 zinawaka saa 12 a day, tv mbili zinatumika kama saa 5 a day, . Nadhani unit 8 a day huu ni umeme mwingi ninao tumia.

Tatizo linaweza likawa wapi? Nimeleta fundi akacheki wiring akasema iko vizuri.

Ushauri tafadhali.

Asante
hanaga majibu kupitia ukurasa huu...........!!!
 
MFUMO WA KUTUPATIA TAARIFA/LALAMIKO

1.JINA.....................................

2.SIMU....................................

3.MKOA...................................

4.WILAYA................................

5.MTAA/KIJIJI/KATA.........

6.JINSI YA KUFIKA................

7.KITU/ALAMA/MTU MAARUFU.............................

8.NAMBA YA MITA................

9.TATIZO LAKO/UNACHOHITAJI....................

10.NAMBA YA TAARIFA ULIYOPEWA.................


"TANESCO TUNAYAANGAZA MAISHA YAKO"
 
Tunatizo la mita Tunaomb msada umeme wa elf 5 tunapata unit 14 wakat mwenye nyumba anapata unit 45 had hamsin
Mtakuwa mpo kundi la matumizi tofauti tunaomba namba yakomya mita tafadhali
 
MFUMO WA KUTUPATIA TAARIFA/LALAMIKO

1.JINA.....................................

2.SIMU....................................

3.MKOA...................................

4.WILAYA................................

5.MTAA/KIJIJI/KATA.........

6.JINSI YA KUFIKA................

7.KITU/ALAMA/MTU MAARUFU.............................

8.NAMBA YA MITA................

9.TATIZO LAKO/UNACHOHITAJI....................

10.NAMBA YA TAARIFA ULIYOPEWA.................


"TANESCO TUNAYAANGAZA MAISHA YAKO"
Hongera kwa kujitahidi
 
Back
Top Bottom