TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Aisee we kijana umeshindwa kazi, yaani suala la eneo fulani kutokuwa na umeme hadi mtu akuambie PM Au number yake ya simu au mkuu umetumwa kwa kazi maalum ? Km kesi ya umeme hamna kwenye nyumba moja tu kweli mtu anaweza akataja jina na number yake
TUPATIE TAARIFA SAHIHI NA FASAHA KWA HUDUMA BORA.

NDUGU WAPENDWA WATEJA WETU MNAOTOA TAARIFA KUPITIA MITANDAO YETU YA KIJAMII TUNAWAOMBA MZINGATIE YAFUATAYO ILI KURAHISISHA UFAFANUZI NA UFUMBUZI WA TATIZO AU TAARIFA HUSIKA

1.ENEO HUSIKA

(Mnaweza kuwa eneo moja lakini mnahudumiwa na transfoma au njia ya kusambaza umeme (feeder) tofauti)

2.NAMBA YA SIMU

(Wakati mwingine umeme upo kote isipokuwa kwako hivyo na rahisi kuwasiliana na wewe)

3.KARIBU NA NINI

(Kuna alama vitu au watu mashuhuri karibu na eneo lako mfano ofisi ya Serikali ya Mtaa, Mahakama, Kituo cha Polisi nk)

4.JINSI YA KUFIKA MAKAZI YAKO

(Toa ufafanuzi wa jinsi ya kufika makazi yako,chukulia unamuelekeza mtu ambaya hajawahi kufika kabisa)

5.MKOA,WILAYA NA KITONGOJI/KIJIJI

(Taarifa hii ni muhimu sana kusaidia kubaini eneo husika lipo wapi kwani yapo maeneo yanayofanana kwa majina lakini yapo Mikoa tofauti mfano Magomeni ipo Dar es Salaam na Mkoa wa Mtwara pia.)

6.KAMA NI TATIZO LA MITA NINI KINATOKEA UKIWEKA UMEME

(Kila mita ina ujumbe wake unaoashiria kitu fulani hivyo kubainisha ujumbe kunamsaidia mpokea taarifa kukupatia maelezo sahihi mfano mita namba 24339173921 inaonyesha error 77)

7.KAMA NI KUSHINDWA KUNUNUNUA UMEME UNAPATA UJUMBE GANI NA UNANUNUA KWA NJIA GANI

(Ujumbe huu ni muhimu sana kuweza kubaini chanzo cha tatizo pamoja na njia iliyotumika kununulia umeme mfamo Mpesa, Tigopesa, Maxcom nk)


TUNAENDELEA KUWASIHII WATEJA WETU KUZINGATIA UTOAJI WA TAARIFA SAHIHI NA FASAHA KWA HUDUMA BORA ZAIDI KUTOKA TANESCO.

ENDELEA KUFURAHIA HUDUMA BORA KUTOKA TANESCO
 
MFUMO WA KUTUPATIA TAARIFA/LALAMIKO

1.JINA................................

2.SIMU...............................

3.MKOA.............................

4.WILAYA..........................

5.MTAA/KIJIJI/KATA.........

6.JINSI YA KUFIKA................

7.KITU/ALAMA/MTU MAARUFU.............................

8.NAMBA YA MITA................

9.TATIZO LAKO/UNACHOHITAJI....................

10.NAMBA YA TAARIFA ULIYOPEWA.................

*Zingatia*

-Kama ni manunuzi ya umeme onyesha mtandao na ujumbe unauopata ukinunuaumeme

-Kama ni kushindwa kuingiza umeme onyesha unachokiona kwenye mita yako unapoweka umeme

-Kama umeshatoa taarifa ofisi yeyote onyesha namba ya taarifa uliyopewa


"TANESCO TUNAYAANGAZA MAISHA YAKO"
Ivi umeelewa nilichoandika hapo,? Nimekuambia bagamoyo mkoa wa pwani maeneo ya mapinga hadi kerege, sasa namba yangu na jina langu la nn?
 
Tafadhalini TANESCO hapa Tandale Chama Transformer yenu linamwaga miali ya moto siku ya tano leo.Tumewapigia Magomeni lakini hakuna lolote walilofanya mpaka sasa
Muda si mrefu hii nguo yenu itaungua na kuchoma nyumba za jirani.

Magari yenu ya emergency yanapita hapa kila baada ya nusu saa lakini hawaoni tatizo lililo wazi kabisa
 
TANESCO Naomba kujua mtakuja kunifungia umeme kwangu Kimara Saranga lini maana nimelipia tokea December mwaka jana mwanzoni, mlinambia itachukua miez miwili ndo imeshaisha hivyo!mwenzenu nateseka sana vitu vyangu vya umeme vinaharibika tu najuta kuwafahamu maana hata kupasi nguo nishasahau, na pesa nimeshalipa 515618.

Alafu cha ajabu mliniambia nikishalipa nisirudi ofisin kuulizia ati mtakuja wenyewe!Mbona hamji jamani khaa..
 
nenda kwenye kituo chako cha karibu cha tanesco, mi mwenyewe niliwekwa tariff 1, nilibadilishiwa cery simple na sikuhonga hatta senti moja.
Naona Tanesco kigamboni bado kuna urasimu nimeandika barua ya maombi wameniambia nijaze fomu halafu baada ya wiki mbili ndio watanirekebishia na wanasema lazima waje nyumbani.

sasa sijui maana ya system wakati rekodi zote zinaonekana kwao.
naomba muliangalie hili
 
Naona Tanesco kigamboni bado kuna urasimu nimeandika barua ya maombi wameniambia nijaze fomu halafu baada ya wiki mbili ndio watanirekebishia na wanasema lazima waje nyumbani.
sasa sijui maana ya system wakati rekodi zote zinaonekana kwao.
naomba muliangalie hili
Hiyo ndio taratibu mkuu lazima tuje tukukagua maana wapo wanaoiba umeme halafu wanaomba kuwa tarif 4 ili kuhalalisha hilo
 
TANESCO Naomba kujua mtakuja kunifungia umeme kwangu Kimara Saranga lini maana nimelipia tokea December mwaka jana mwanzoni,mlinambia itachukua miez miwili ndo imeshaisha hivyo!mwenzenu nateseka sana vitu vyangu vya umeme vinaharibika tu najuta kuwafahamu maana hata kupasi nguo nishasahau, na pesa nimeshalipa 515618.Alafu cha ajabu mliniambia nikishalipa nisirudi ofisin kuulizia ati mtakuja wenyewe!Mbona hamji jamani khaa..
Ulilipa kwa jina gani na namba yako ya simu?kwa kiasi ulicholipa bado upo ndani ya muda wa mkataba wa huduma kwa wateja
 
Tafadhalini TANESCO hapa Tandale Chama Transformer yenu linamwaga miali ya moto siku ya tano leo.Tumewapigia Magomeni lakini hakuna lolote walilofanya mpaka sasa
Muda si mrefu hii nguo yenu itaungua na kuchoma nyumba za jirani
Magari yenu ya emergency yanapita hapa kila baada ya nusu saa lakini hawaoni tatizo lililo wazi kabisa
Tunaomba namba yako ya simu mkuu tufike eneo husika
 
Lalamiko la eneo husika linaweza kutumwa hata pm
Kwani ikiambiwa umeme magomeni mtaa fulani umekatika hamuwezi kushughulikia? Mnaweka urasimu hadi kwenye njia za kutoa taarifa?
 
Naona Tanesco kigamboni bado kuna urasimu nimeandika barua ya maombi wameniambia nijaze fomu halafu baada ya wiki mbili ndio watanirekebishia na wanasema lazima waje nyumbani.
sasa sijui maana ya system wakati rekodi zote zinaonekana kwao.
naomba muliangalie hili
Hata mimi nishawaandikia barua kimya, nilikwenda ofisini kwao jamaa mikwara mingi yaani unamuona jinsi inavyomuuma wewe kubadilishiwa tarrif
 
Hata mimi nishawaandikia barua kimya, nilikwenda ofisini kwao jamaa mikwara mingi yaani unamuona jinsi inavyomuuma wewe kubadilishiwa tarrif
ahhhh yaani inabidi tuwe wapole ,mimi wameniambia nisubiri labda baada ya mwezi.
 
Shirika la Umeme Tanzania - (Tanzania Electric Supply Company Limited - TANESCO), Tunaomba mtupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri kupitia huu uzi nasi tutawajibu.

Tunawaomba mzingatie yafuatayo ili kurahisisha ufafanuzi na ufumbuzi wa tatizo au taarifa husika;

1.ENEO HUSIKA

(Mnaweza kuwa eneo moja lakini mnahudumiwa na transfoma au njia ya kusambaza umeme (feeder) tofauti)

2.NAMBA YA SIMU

(Wakati mwingine umeme upo kote isipokuwa kwako hivyo na rahisi kuwasiliana na wewe)

3.KARIBU NA NINI

(Kuna alama vitu au watu mashuhuri karibu na eneo lako mfano ofisi ya Serikali ya Mtaa, Mahakama, Kituo cha Polisi nk)

4.JINSI YA KUFIKA MAKAZI YAKO

(Toa ufafanuzi wa jinsi ya kufika makazi yako,chukulia unamuelekeza mtu ambaya hajawahi kufika kabisa)

5.MKOA,WILAYA NA KITONGOJI/KIJIJI

(Taarifa hii ni muhimu sana kusaidia kubaini eneo husika lipo wapi kwani yapo maeneo yanayofanana kwa majina lakini yapo Mikoa tofauti mfano Magomeni ipo Dar es Salaam na Mkoa wa Mtwara pia.)

6.KAMA NI TATIZO LA MITA NINI KINATOKEA UKIWEKA UMEME

(Kila mita ina ujumbe wake unaoashiria kitu fulani hivyo kubainisha ujumbe kunamsaidia mpokea taarifa kukupatia maelezo sahihi mfano mita namba 24339173921 inaonyesha error 77)

7.KAMA NI KUSHINDWA KUNUNUNUA UMEME UNAPATA UJUMBE GANI NA UNANUNUA KWA NJIA GANI

(Ujumbe huu ni muhimu sana kuweza kubaini chanzo cha tatizo pamoja na njia iliyotumika kununulia umeme mfamo Mpesa, Tigopesa, Maxcom nk)

TUNAENDELEA KUWASIHII WATEJA WETU KUZINGATIA UTOAJI WA TAARIFA SAHIHI NA FASAHA KWA HUDUMA BORA ZAIDI KUTOKA TANESCO.

ENDELEA KUFURAHIA HUDUMA BORA KUTOKA TANESCO

Vilevile pitia threads hizi kupata Maelezo ya ziada;

LUKU:Mfumo wenye Tija kwa Wateja na TANESCO

Fahamu mita za LUKU zinazofungwa majumbani

Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

Kw mawasiliano Kituo cha Miito ya Simu (+255) 22194400 or (+255) 768 985 100 Mitandao ya kijamii Tanescoyetu (@tanescoyetu) | Twitter Facebook: Tanesco Yetu

HAPA CHINI NI NAMBA ZA SIMU ZA MIKOA

Ofisi ya Mkoa wa Mbeya Simu ya Mkononi (+255) 757 529 380 ya Mezani (+255) 252 504 219

Ofisi ya Mkoa wa Ilala Simu ya Mkononi (+255) 784 768 586 ya Mezani (+255) 222 133 330

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kusini (Magomeni) Simu ya Mkononi (+255) 715 271 461/ (+255) 784 271 461

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kaskazini (Mikocheni) Simu ya Mkononi (+255) 784 768 584 / (+255) 716 768 584 ya Mezani (+255) 222 700 367/ (+255) 222 701 602 / (+255) 222 774 098

Ofisi ya Mkoa wa Temeke Simu ya Mkononi (+255) 712 052720 / (+255) 758 880155 / (+255) 732 997361

Ofisi ya Mkoa wa Pwani Simu ya Mkononi (+255) 78 5122020 / (+255) 65 7108782ya Mezani (+255) 23 2 402 386

Ofisi ya Mkoa wa Arusha Simu ya Mkononi (+255) 75 8 174 343 Mezani (+255) 272 506 110

Ofisi ya Mkoa wa Tanga Simu ya Mkononi (+255) 658 122 412/ (+255) 687 677 667 Mezani (+255) 27 2 646 779

Ofisi ya Mkoa wa Kilimanjaro Simu ya Mkononi (+255) 765 397 925/ (+255) 682 771 310 Mezani (+255) 272 755 007/8

Ofisi ya Mkoa wa Manyara Simu ya Mkononi (+255) 689 795 599 / (+255) 75 9 534 130 Mezani (+255) 272 530 590

Ofisi ya Mkoa wa Mwanza Simu ya Mkononi (+255) 759 777 786 / (+255) 687 910 202 Mezani (+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

Ofisi ya Mkoa wa Geita Simu ya Mkononi (+255) 744 085 696 Mezani (+255) 28 2520330

Ofisi ya Mkoa wa Kagera Simu ya Mkononi (+255) 78 5 787 898 / (+255) 75 3 120 701 Mezani (+255) 282 220 061

Ofisi ya Mkoa wa Mara Simu ya Mkononi (+255) 762 165 087 / (+255) 732 985 672

Ofisi ya Mkoa wa Simiyu Simu ya Mezani (+255) 282 700 180

Ofisi ya Mkoa wa Dodoma Simu ya Mkononi (+255) 782 161 643 Mezani (+255) 262 321 728

Ofisi ya Mkoa wa Morogoro Simu ya Mkononi (+255) 68 4889272 / (+255) 65 4829046 Mezani (+255) 232 613 501/2

Ofisi ya Mkoa wa Singida Simu ya Mkononi (+255) 71 4 477 445 / (+255) 732 960 924 / (+255) 689 373 757 Mezani (+255) 262 502 133

Ofisi ya Mkoa wa Tabora Simu ya Mkononi (+255) 786 558 510 / (+255) 763 162 868

Ofisi ya Mkoa wa Shinyanga Simu ya Mkononi (+255) 754 521 070 Mezani (+255) 28 2762120

Ofisi ya Mkoa wa Kigoma Simu ya Mkononi (+255) 78 3720598 Mezani (+255) 28 2802668

Ofisi ya Mkoa wa Katavi Simu ya Mkononi (+255) 68 8345200

IMETOLEWA NA:- Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makauu.
Naomba kujua taratibu za kuongeza mita kwenye Nyumba yenye mita mfano Mimi MPANGAJI nahitaji mita kwenye Chumba changu
 
Hiyo ndio taratibu mkuu lazima tuje tukukagua maana wapo wanaoiba umeme halafu wanaomba kuwa tarif 4 ili kuhalalisha hilo
sawa pamoja ndio utaratibu lakini ndio naambiwa labda baada ya mwezi ndio watakuja;kweli ndio Tanzania ya Viwanda hii
 
Mtu unalipoti tatizo kwa haraka zaidi kuepuka madhara unayoweza yapata kutokana na hitirafu ya umeme lakini cha kushangaza siku ya nne Leo tatizo bado lipo palepale,unaenda ofisini kwao wanakuambia mafundi watakuja lakini wapi ,unapiga emergence stori ni zilezile siku ya nne Leo sina umeme da aisee is so painful,Hivi hawa Tanesco wa maeneo mengine wapo kama hawa wa Songea au huko kungine kuna unafuu kidogo?
 
Hivi tanzania ya viwanda tutafika kweli kama umeme wa kuwasha taa tu ni mtihani viwanda sindiohatari
 
pole sana wanaleta za kujuana sana hawa jamaa Kaleman afik na huko..
Yaani ni shida sana mkuu unapiga simu anapokea mdada kwa bashasha utafikiri fasta tatizo litaisha lakini wapi ,Leo nimeshindwa kwenda hata kanisani maana siwezi nyosha nguo,inasikitisha sana
 
Back
Top Bottom