TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Tatizo la kutotuma Token limeanza tena.? Nimenunua umeme nusu saa imepita sijatumiwa token hadi muda huu.? Kulikoni.?
Wanajilipa billion 61, huduma mbovu, mimi nililipia kuwekewa umeme tangu december 2021, hakuna kitu, ukiwauliza wanakula takwimu za walioomba oooh kuna maombi zaidi ya 400!

Unajiuliza tatizo langu na takwimu zenu vinahuusianaje, mimi nataka umeme wewe unanipatakwimu nifanyejee.

TANESCO nawasiwasi na Elimu zao, kuanza waziri husika hadi mlinzi wa geti
 
tanesco kinondoni/kawe..mimi mkazi wa bunju A, Usalama mtaa wa mkoani shida ikifika saa moja usiku umeme unapungua taa mafriji hayawaki yanatetemeka, nadhani imefika kipindi mpitishe sheria ya fidia ya vifaa vya umeme na majanga kwa ujumla yatakayotokana na uzembe wa shirika lenu..kwann mnaongeza watu kwenye service line ikiwa mnajua line imeelemewa? TANESCO
 
Na hapo mkono ukiwa birika bas
Hata nusu mwaka utangoza
yaaani

niliomba umeme mwez wa saba nilitakiwa nguzo lakini nikapost hum nikaambiwa hivohivo nikajiongeza tayar umeme unawaka ukiwa huna mkono wa kutoa utasota na wanataka ujiongeze mwenyewe
 
Hopeless Tanesco, tangu asubuhi mpàka Sasa hivi karibu saa mbili usiku some parts of Tanga city hakuna Umeme. Na hakuna hata kutoa taarifa kwa wateja. Wamekata tu. Shida tupu mtaani.
 
Hatimaye TANESCO wameniletea umeme baada ya kuusubiria kwa muda wa miezi 6, nililipia ile 27 K last year Dec.. 25 Jun ndio wameingiza umeme

Najipongeza maana nilivumilia na nilikataa kupita short cut.
Asante
Screenshot_20220630_084448.jpg
 
Nimekuwa nikipiga simu toka tarehe 6 June 2022, nahitaji surveyor akanipimie nipate control number nilipie, cha ajabu mpaka leo 6-07-2022 bado sijapata, sikuweza kuwaza kama hii process inaweza chukua hata 2 days
 
Nimekuwa nikipiga simu toka tarehe 6 June 2022, nahitaji surveyor akanipimie nipate control number nilipie, cha ajabu mpaka leo 6-07-2022 bado sijapata, sikuweza kuwaza kama hii process inaweza chukua hata 2 days
Tafadhali onesha namba ya ombi kwa hatua zaidi
 
Hatimaye TANESCO wameniletea umeme baada ya kuusubiria kwa muda wa miezi 6, nililipia ile 27 K last year Dec.. 25 Jun ndio wameingiza umeme

Najipongeza maana nilivumilia na nilikataa kupita short cut.
Asante
Karibu sana
 
Hopeless Tanesco, tangu asubuhi mpàka Sasa hivi karibu saa mbili usiku some parts of Tanga city hakuna Umeme. Na hakuna hata kutoa taarifa kwa wateja. Wamekata tu. Shida tupu mtaani.
Huduma umerejea sasa tafadhali
 
yaaani

niliomba umeme mwez wa saba nilitakiwa nguzo lakini nikapost hum nikaambiwa hivohivo nikajiongeza tayar umeme unawaka ukiwa huna mkono wa kutoa utasota na wanataka ujiongeze mwenyewe
Tafadhali onesha namba ya ombi kwa hatua zaidi
 
Tafuteni ufumbuzi wa kuuza luku kwa mtindo wa vocha kuanzia shs 500, kuendelea hadi laki moja. Yaani unanunua tu vocha unajaza upo seminar Mwanza umeme unawaka nyumbani Dar.

Haya mambo ya kupanda juu ya stuli kudonoa donoa mita za luku ni ya kizamani. Tunataka umeme digital .yaani ukiingiza tu vocha kwenye simu au app umeme unawaka direct.
 
Maneja wa TANESCO kibaha.tunaomba utuanganzie wakazi zaidi ya 15 wa eneo la Mwanalugali,hisia kali. Karibu na eneo inapojengwa zahanati
-Wananchi wa eneo hili kila tunapofutilia umeme tunaambiwa zinatakiwa nguzo Kati ya tano na kumi kuwafikia Wananchi wote.(Kwa hiyo Ni mradi).
-Huu mradi umekuwa unazungumziwa tangu mwaka 2015 mpaka leo.
-Tanesco ni shirika la kuwaangazia wananchi maisha na siyo shirika la kuwaweka wananchi gizani.
-Mradi unakuwa na timeframe,ni mradi gani hauma timeframe (haukamiliki tangu 2015 mpaka 2022).
-Sisi wakazi wa Mwanalugali tunaamini TANESCO Kibaha wanazo nguzo za umeme za kutosha.
-Viwanja vya Mwanalugali Wakati vinapimwa 2006 Serikali ilisema kutakuwa na huduma ya maji, umeme, zahanati,soko nk.
-Tunashukuru Serikali imeleta mradi wa maji na zahanati inajengwa.
-wananchi wenye Viwanja wameanza kuendeleza baada ya kuona huduma ya maji na zahanati inajengwa.Wananchi wengi watakuja kujenga na kuishi Mwanalugali kama huduma ya umeme itafika.

Ushauri
1). TANESCO Kibaha ifikishe nguzo eneo hilo,ili sisi wananchi tulipie service line ya shs320,960
2). TANESCO Kibaha itume wapimaji wake kuja kuhakiki na kufanya makadirio ya hizo nguzo ili kuomba fund TANESCO makao makuu.Mkurugenzi Mikuu wa TANESCO ni kijana safi na result oriented,hawezi kushindwa nguzo 10 za umeme-kibaha Town Council.
3). Kama TANESCO haina fedha wakazi wa tunaweza kuchangia gharama kwa pamoja, badala ya kumwambia mteja mmoja kulipia nguzo tatu zaidi ya milioni Saba,ili kupata huduma.
4). TANESCO iwe inatembelea au inapeleka miundo mbinu ya umeme maeneo yote yaliyopimwa,ili kuleta chachu ya Maendeleo endelevu na kuongeza kanzidata ya wateja.
5). TANESCO Kibaha wanaweza kupeleka/kujenga nguzo za umeme Mwanalugali, wakati wanasubiri vifaa vingine vya umeme,wakishafikisha nguzo karibu na wateja ndiyo waanze kutoa control number kwa wateja ,kwa kufanya hivi shirika litaongeza idadi ya wateja na mapato kwa shirika

Mwisho tunaomba Mkurugenzi wa TANESCO Kanda ya Dar es Salaam na Pwani na Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, kutatua changamoto ya umeme Mwanalugali Kibaha Township.
Tumepokea ombi lako kwa hatua zaidi tafadhali
 
Inawachukua siku ngapi kumuunganisha mteja anayehitaji nguzo Moja, baada ya malipo, maaana Sasa ni mwez mmoja na Wiki Moja Sion dalili
Tafadhali onesha namba ya ombi kwa hatua zaidi
 
Naona mna nguzo za zege miaka 100 zitadumu japo wakulima wa miti ya nguzo imekula kwao ndo ilivyo technology. Sasa mtupunguzie bei ya nguzo maana hizi nadhani ni nafuu zaidi kuliko zile za miti.
 
Back
Top Bottom