TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Jamani kweli na leo huku kimara baruti tusio na majenereta na hela ya kwenda baa kama sio vibanda umiza tusiangalie timu yetu ya taifa kweli?
 
Jamani kweli na leo huku kimara baruti tusio na majenereta na hela ya kwenda baa kama sio vibanda umiza tusiangalie timu yetu ya taifa kweli?
Sisi wamekata saa 12 asubuhi, watu hatujanyoosha na ni siku ya kazi. Hawa jamaa ni wapuuzi sana, failure kwenye kila kitu. Yaani nikimuona mfanyakazi wa TANESCO huwa najisemea jinga lileee 😀
 
Hivi namba za simu za TANESCO za muda wote ni zipi?. Nipo Dodoma natumia namba za simu za TANESCO zilizo kwenye contact zao nikigoggle hawapokei. Nina tatizo la umeme nyumbani kwangu. Naomba msaada.
 
Tanesco naomba msaada wenu mnielekeze kama submeter inaweza ikasababisha tatizo la umeme kama shot au umeme kua mdogo hauwaki nyumba nzima
 
Nimesoma malalamiko mbalimbali ya wateja wa UMEME! mm pia nikapata mstuko na kujaribu kufuatilia! Lkn pia nikasikia majibu yenu juu ya KILICHOITWA - unit za umeme kuisha kwa HARAKA -

Hii hali imetokea hivi karibuni, majibu yenu yalikuwa " hali hiyo inatokea kipindi hiki kwa kuwa wananchi wengi msimu huu wapo MAJUMBANI.

NILINUNUA umeme tarehe 19/12/2023 kwa tsh 20,000/= nikapata unit 51.9 KWH .matumizi ya hapa nyumbani ni
1 - rice cooker
2- pasi ( mara mojamoja jumapili)
3- feni vyumba 2 usiku kucha na mchana .
4- fridge
5- taa za kwenye ukuta ( fensi)
6- Tv
Umeme huu ulidumu siku 8.

Tarehe 27/12/2023 saa 20:32nilinunua tena umeme kwa tsh 20,000/= nikapata unit 42.1KWH

Matumizi yangu yamezidi kidogo kwani nimeongeza FENI jingine hivyo feni ziko 3 zinazokesha.

Fridge nilikuwa nalizima wakati wa mchana sababu ya joto kali lkn hivi sasa linafanya kazi muda WOTE.

Matumizi mengine yamebaki kama kawaida. Leo ni siku ya 10 umeme bado upo.

Tarehe hiyo hiyo 27/12/2023 saa 19:58 nilinunua umeme kwa tsh 20,000/= nikapata unit 56.1 KWH ( huu niliponunua sikuuona nilidhani umeshindikana nimeuona leo kwenye simu)

Kwanini 20 , 000/= unit 51.9 KWH
Kwanini 20 ,000/= unit 56.1 KWH

Iweje 51.9 unit Zitumike siku 8
Halafu 42.1 unit zitumike zaidi ya siku 10

NAWASILISHA
Secondly,
Sometimes unaweza wahisia Tanesco ni shirika la wezi lililorasimishwa kiserikali, i don't know why they're not consistent,

Mfano. Leo Tar. 1 utanunua umeme wa Elfu 5k unapata 14.0Kwh ukija kununua tena wa hiyo hiyo libuku 5k Tar 5/6 unapata 36.0 Kwh lakini ukija kununua tena umeme wa hiyo hiyo Elfu 5k kwa siku zinazofuata mfano Tar 10,15,20,25 unapata 11.0Kwh siku zote. Na Meter ni hiyo hiyo.

Ilhali kwa kawaida inafahamika yakuwa umeme wa Elfu Tano haupungui 14.0Kwh

Tanesco. Hii kubadilika badilika kwa unit za umeme ilihali price haibadiliki shida ni nini[emoji848]????
 
Sina uhakika kama uzi huu Tanesco wanajishughulisha nao,lakini kama wapo,tafadhali nawaomba mtoe ratiba ya mgao mkali wa umeme katika baadhi ya maeneo Shinyanga.
Umeme kila jioni unakata na unarudi usiku wa manane.
Asubuhi kabla ya saa 3 umeme mnakata tena hadi muda usiojulikana.

Je kuna tatizo gani?Au hii ni dharau tu kwa wananchi kwamba "watatufanya nini?"
 
Hivi mitaa walikojenga/wanakopanga watumishi wa TANESCO umeme haukatiki au ni vipi??
 
Wadau kutoka mikoa mbali mbali hembu ambapo hakuna umeme tutaje.

Niko Tanga,giza tupu,umekata saa moja kasoro.

Mvua wakati zinanyesha tuliambiwa hazifiki kwenye mitambo,wiki nzima kuna mafuriko kila sehemu,wahuni bado wanakata umeme kila siku.

Halafu Kuna washenzi wanasema Mama Kizimkazi anaupiga mwingi!!
 
Nilitaka nishamgae hawa mbwa waache umeme siku nzima bila kukataa.alaa kama kawaida yaki acha mchana usiku yana kata yaki kata usiku mchana yanaacha ndo maisha yetu saivi..trash
 
Back
Top Bottom