TANESCO tutangazieni kama kuna mgao wa umeme nchini

TANESCO njooni mjibu huku
 
Mshaanza sifa za kijinga....Unataka kutuambia kipindi cha JIWe umeme ulikuwa haukatiki?
 
Hizi sasa ni Propaganda..., search humu humu ndani ni mwezi sasa watu wanalalamika umeme unakatika hovyo..., tofauti ni kwamba kipindi cha zamani ungesikia ila kipindi hiki cha kusifia na kuficha ukweli utajua wapi ? (Enzi hizi hata usiku ungelazimishwa uitwe mchana)
 
Ndio zao sana
 
#Kuna siku mtanikumbuka
 
Sisi wakazi wa kimara tumekumbwa na hali ya mlipuko na shoti mithili ya transformer kulipuka au shoti ya muingiliano wa phase.
Tuna mashaka na kuunguziwa vifaa vyetu kama TV, friji nk, kufuatia tatizo hill kujitokeza.

Tunaombeni taarifa rasmi na kujua ukubwa wa tatizo ili tuweze kujiandaa na hasara za biashara na vyakula vyetu kwenye friji.
 
nna wasiwasi na Tv na friji... nilikuwa nimelala nikasikia kama mlipuko.. ngoja kesho tutajua
 
Sijui kama Waziri na Naibu wake wana taarifa, siku hizi umeme unakatika tu bila taarifa na kwa week hata mara 5.
Wafanyabiashara wanaotegemea umeme wanapata tabu sana.

Kwakweli kama kuna mgao mtueleze ili tuwe tunajipanga kabisa maana mnatutia hasara.
Majibu yenu ya ajabu eti sijui kunguru kafanyaje, utadhani hao kunguru wameanza kuwepo siku hizi. TANESCO
 
 
Hii waione wale wanaosema kipindi cha Magufuli kulikuwa hakuna mgao wa umeme
Hizo zinaitwa sifa za kijinga Wakati ikifika Hadi kipindi makamu wa Rais enzi hizo Samia akiwa Tanga akasema anawapa Tanesco muda mchache mgao uishe Tanzania nzima sasa sijui yeye alikuwa makamu wa Rais kipindi cha Mwinyi au?

Kiufupi CCM imeoza yaani Haina unafuu

Mwingine atakuja anateka anaua ila madaraja anajenga
Mwingine hateki na kuua ila mambo vululuvululu sasa kazi ni kwetu
Wacha tuisome namba
 
Kosa tar 17.3 mungu hakumuona Hangaya
 
Naambiwa 65% ya umeme unaozalishwa Tanzania unatokana na gesi asilia kutoka Kusini, na unazalishwa na mitambo ya gesi ya Ubungo / Songas na Kinyerezi, gesi bado ipo na mitambo inapiga kazi kama kawaida, mabwawa nayo uzalishaji bado unaendelea, sasa tatizo liko wapi hadi mnakata umeme kila siku hovyo hovyo bila ratiba?

Wakati JPM akihutubia bunge kwa mara ya kwanza kama Rais wa Tz aligusia suala la Tanesco kuhongwa na makapuni binafsi ya ufuaji umeme ili kufungulia mabwawa ya maji na kutengeneza uhaba wa umeme, je, mchezo huu umerudi tena?
 
Kama haya yapo kweli basi vyombo vya usalama haswa zile idara nyeti hamna kitu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…