Tanga, Korogwe: Ajali yaua 17 na kujeruhi 12

Tanga, Korogwe: Ajali yaua 17 na kujeruhi 12

Barabara zetu ni nyembamba

Barabara zetu ni giza

Barabara zetu zina viraka au mashimo

Magari mengi ya mizigo hayana Taa nzuri

Magari mengi ya mizigo huendeshwa na watu wasiojali gari au watumiaji wengine wa barabara

Madereva wengi wa magari (Binafsi, Mizigo, Umma) wanaendeshwa kwa mazoea.

Madereva wengi wa Coaster hutumia vilevi
Hizi ndo sababu za ajali nyingi Kwa Tanzania na Africa Kwa ujumla , magar yanaongezeka kila sku miundombinu Ile Ile ,
 
Kuna watakaokuja kubeza unachowaza....

Ila mara kadhaa tumeshashuhudia waafrika wanagombea maiti kwenda kuzika, ugomvi msibani na kutoelewana kati ya ndugu wa marehemu.

Moja ya maswali yako inaweza kuwa kweli, akipatikana mwana familia wa karibu na marehemu wa kwanza aliyekuwa anasindikizwa kama alikuwa na macho ya rohoni kuna siri mahala.

Kma ni ajali ya kawaida basi kuna liana mahala, ama wazee wa mji/ ardhi anakoenda kuzikwa marehemu hawamtaki....

Mungu awapatie ufumbuzi wapone majeraha ya mwilini na rohoni.
Kwa maana hyo misiba imekuwa 18 kwa wakt mmoja Mbna hi Ni hatari sana
 
View attachment 2505507View attachment 2505508View attachment 2505511
Picha za Ajali

Ndugu waandishi wa Habari na Ndugu wananchi wa Mkoa Wa Tanga na Tanzania kwa ujumla Nimepokea kwa masikitiko makubwa tukio la Ajali Mbaya iliyotokea usiku wa leo. Ajali hiyo imehusisha Magari mawili na kusababisha Vifo vya watu 17 na Majeruhi 12 Pamoja na Uharibifu mkubwa wa Magari hayo..

Ajali ilitokea Tarehe 03/02/2023 Majira ya Saa 4.30 Usiku Eneo la Magila Gereza Kata ya Magila Gereza Tarafa ya Mombo Wilayani Korogwe, Barabara Kuu ya Segera - Buiko.

Magari yaliyohusika na Ajali hiyo ni Gari Na T.673 CUC aina Mitsubish Fuso Ikiendeshwa na Dereva ambaye Jina Lake Halijafamika iligonga na Gari T.863 DXN aina ya Coaster Coaster Iliyokuwa imebeba Mwili wa Marehemu n Abiria 26 iliyokea Dar es Salaam Kuelekea Moshi Kilimanjaro kwa mazishi.

Ajali hii inasababisha Vifo 17 na Majeruhi 12. Ambao Majina yao wote Hayajafahamika. Miili ya Marehemu imehifadhiwa katika Hospitali yetu ya Wilaya Ya Korogwe na Majeruhi 10 Wamehamishiwa Hospitali ya Mkoa wa Tanga Bombo na Majeruhi 2 wamebaki Hospital ya Korogwe Kwa Matibabu.

Chanzo cha Ajali ni Mwendo Kasi na Uzembe wa Dereva wa Gari Na :T.673 CUC M/Fuso Kulipita gari la mbele Bila Ya kuchukua Tahadhari na kugongana Uso kwa uso Gari Na :T.863 DXN T/Coaster

Tukio la Ajali Baada ya kukaguliwa , Magali yote yameshaondolewa barabarani na Sasa Barabara inapitika.

Mgumba T. Omary
Mkuu wa Mkoa Wa Tanga.
Daaah yaani ni misiba juu ya msiba,poleni sana wafiwa wote, ndugu, jamaa na marafiki.
 
Tunaweza kusema mengi kwa kadri tuwezavyo na tudhaniavyo.
Lakini kuna watu wanapitia wakati mgumu lakini hii familia iliopata msiba natumaini wao kwa sasa wako kwenye wakati mgumu kuliko tunavyoweza weza kusema, pangine wanahitaji faraja ya taifa.

Changamoto za vyombo vya usafiri bado ni kubwa sana huku kwetu, madereva wamekua na haraka kuliko , na bahati mbaya hawafiki wanako harakisha kufika, hebu madereva mtafakari tena juu ya maisha, maisha ni furaha sio huzuni na maumivu, hebu tufanye maisha kuwa mazuri na ya furaha kwa kujali .

Pole nyingi sana kwa wote walio athirika, pole kwa walio jeruhiwa, pole kwa walio fiwa na kufiwa tena.

Wakati ufike watu wa kaskazini na wengineo tufikirie upya kama bado kunaulazima wa kufanya maziko nyumbani tu.
 
Watu 17, ambapo 14 ni wa familia moja, wamefariki dunia na wengine 12 wamejeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea eneo la Magira Gereza, Tarafa ya Mombo wilaya ya Korogwe mkoani Tanga.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoa wa Tanga, Omary Mgumba amesema Ajali hiyo imehusisha gari aina ya Mitsubishi Fuso iliyoligonga gari aina ya Coaster iliyokuwa imebeba mwili wa marehemu na abiria 26 ikitokea jijini Dar es Salaam kwenda Moshi kwa ajili ya mazishi.

Waliofariki kwenye ajali hiyo ni wanaume tisa, wanawake sita, watoto wawili mmoja wa kike na mmoja wa kiume.

Majeruhi 10 wamehamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga, Bombo kuendelea na matibabu na wawili wamebaki Hospitali ya Wilaya Magunga huku hali zao zikiendelea vizuri.

Mgumba amesema miili ya marehemu ipo katika Hospitali ya Wilaya Magunga, Korogwe.

Chanzo cha ajali ni kimeripotiwa kuwa ni uzembe wa dereva wa gari aina ya fuso kutaka kulipita gari lililokuwa mbele yake na ndipo lilipogongana uso kwa uso na Coaster hiyo.

TBCOnline
 
Midereva ya mafuso hata sijui wana matatizo gani? Yaani mwezi uliopita hapa kijijini kwetu bodaboda aligongwa na fuso yaani alichanguliwa changuliwa kulibak kiwiliwili tu.....hawa nahis watakuwa wanavuta bangi na gongo.....then nahis wanaona barabara zimetengenezwa kwa ajili yao tu kwan huwa wanatembea katikati ya barabra hawakai kwenye site zao.....
 
Back
Top Bottom