Tanga: Mjamzito afariki dunia kituo cha afya kwa kukosa Tsh. 150,000

Tanga: Mjamzito afariki dunia kituo cha afya kwa kukosa Tsh. 150,000

Mama mjamzito, Mariam Zahoro (30) Mkazi wa Kijiji cha Mumbwi Wilayani Handeni, Tanga amefariki dunia akiwa kwenye Kituo cha Afya Kabuku kilichopo Wilayani humo ikidaiwa kuwa alikosa huduma ya upasuaji baada ya kushindwa kulipa Tsh. 150,000 alizotakiwa kutoa kwa ajili ya huduma hiyo.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia November 11 kwenye Kituo hicho ambapo Mama mzazi wa marehemu, Hadija Athumani amesema Wahudumu hawakumfanyia Mwanae operesheni kwa kudai hela ya matibabu.

“Nilinyanyasika nikatukanwa kama mbwa alitakiwa kufanyiwa operesheni hawakuweza kumfanyia kwasababu hatukuwa na hela na Mimi ni fukara, Mwanangu aliniita akasema Mama njoo hapa nakufa sasa Mimi sina uwezo nikaka pale akawa anasema Mama nishike mkono, amama nishike kichwa, nililala chini sikuwa na cha kufanya akanipa mkono akaniambia Mama nakufa ndipo alipofariki”

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Handeni Albert Msando amesema Serikali inalifanyia uchunguzi jambo hilo ili kubaini chanzo cha tukio.

Pia soma > Watumishi 3 wasimamishwa kazi kwa kusababisha Kifo cha Mjamzito kisa hajatoa Tsh. 150,000
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alisema wajawazito hawalipi kwenye hospitali za umma

Au aliongea ili kuongeza kura kwa CCM?
 
Haospitali Zingine wanaweka deni, siku ya kutoka unadaiwa, hapo inabidi wawajibishwe hao wahusika
Huu ndio utaratibu wa zahanati nyingi huku mjini hasa Kwa wamama wajawazito. Akishajifungua deni analipa analipa wakati wakuhudhuria kliniki ya mtoto
 
Nidhamu hospital mahospitalini imeshuka sana siku hizi. Hospital nyingi ukiwa na mgonjwa halafu huna ela ya matitabu unadharaurika sana.
 
Sawa Hebu nipe hiyo Sera inayosema hivyo Maana huku Katiak Hospitali tuna sera Tofauti ya Malipo kwa C/Section na kuna Muongozo mwingine wa malipo kwa Watoto uliotoka Since 2021 sasa ndo maana nataka kujua wewe huo muongozo Ni upi unautumia kusema C/Section ni bure
Upo Hosp ya Serikali wewe ?.
 
Nzuri, miaka zaidi ya 20 , na Bado unasema una muongozo unaodai C-section Kwa Wajawazito Hosp za Serikali ni malipo ?.
Kwanza natakiwa nikuulize kuhusu level ya kituo chako maana kwa hpa Hata watoto Paediatric under five wanalipia...
Na kingine kama unao muongozo unaosema ni bure Nitafurahi kuuona pia ukinipa
 
Kwanza natakiwa nikuulize kuhusu level ya kituo chako maana kwa hpa Hata watoto Paediatric under five wanalipia...
Na kingine kama unao muongozo unaosema ni bure Nitafurahi kuuona pia ukinipa
Niko Wilaya, labda unisaidie muongozo unaosema Wajawazito na U-5 wanalipia huduma
 
Niko Wilaya, labda unisaidie muongozo unaosema Wajawazito na U-5 wanalipia huduma
Anhaa bhasi kama uko Wilayani Ulizia Jinsi Wizara inavyofanya kazi katika mkoa na upate ithibaki kwa eneo mahalia..
Maana Hospitali zote za mikoa U-5 wote wanalipia ...

Na kingine nikusaidie Wajawazito Hawalipii only SVD kwa hospitali za wilaya ila kwa zingine hulipia na ndo maana nilikuomba Hiyo sera yako ya Bure umeshindwa unaniomba sera na Muongozo wa Kulipia?

Ikiwa umeshindwa kunipa muongozo wa Bure unatakaje mimi nikupe muongozo wa kulipia?
 
Back
Top Bottom