Tangu Mungu amuulize Adamu, Adamu uko wapi? Wanaume hatupendi kabisa kuulizwa hilo swali

Tangu Mungu amuulize Adamu, Adamu uko wapi? Wanaume hatupendi kabisa kuulizwa hilo swali

Kama kweli shetani yupo, na uwezo na nguvu anazotajwa kuwa anazo, basi wewe Hauna uwezo wa kumshinda hata kwa sekunde.
Utagundua kwamba Shetani ni Side B ya Mungu ila ili ulielewe hili inakubidi uende deep sana kwenye kujiuliza maswali kwamba Mungu kweli muweza wa vyote alishindwa shindwa vipi kumzuia Shetani asimpe yule Mwanamke tunda au ni Mungu mwenyewe mpangaji wa kila kitu alienda kwa yule Mwanamke akiwa kwenye umbo la Shetani? Utajiuliza kabla ya Mwanamke mboni Adamu hakurubuniwa na Shetani ila baada ya Mungu kumleta Mwanamke Mwanamke akarubuniwa na Shetani? Hapo kupata majibu ya kina lazima uingie ndani zaidi kwenye maswali ya kujiuliza kwamba Mungu huyu alikua na mpango gani na Adamu na Hawa?
 
Mungu wala Shetani hawapo mkuu.
Mnajilisha upepo tu hakuna cha maana
Laiti kama Mungu na Shetani wangekuwepo, mimi ningekaa upande wa Shetani
Shetani ni Side B ya Mungu ukitaka kulijua hilo soma kitabu cha Ayubu utaelewa jambo, yaan Mungu alipiga story na Shetani akamwambia umemuona mtumishi wangu Ayubu nakutuma ukamjaribu? Kwa hio inamaana na pale bustanini Mungu alimtuma Shetani akamjaribu Mwanamke? Yaan lazima uingie ndani ya maswali kujiuliza maswali mengi na mengine ili upate majibu
 
ndio ni muweza wa yote, uko sahihi, twende kwenye hoja sasa
Okay nilitaka ujae humo sasa ngoja nikupeleke katikati ya kina kirefu cha bahari, Mungu ndio muweza wa vyote ilishindikanaje akashindwa kuweza kumzuia Shetani asimrubuni yule Mwanamke au ni Mungu ndie aliemtuma Shetani?

Na km ni Mungu ndie aliemtuma Shetani km ilivyoandikwa kwenye kitabu cha Ayubu ukiacha na story ya uasi wa Malaika ila ukija kwenye story ya Adamu na Hawa unaona Shetani alitupwa Duniani pamoja nao, sasa kwanini km ni Mungu alimtuma Shetani akamrubuni Mwanamke kwanini Mungu awatupe Adamu na Hawa pamoja na Shetani wakati ni yeye Mungu aliemtuma Shetani akamrubuni yule Mwanamke? Shetani alikua na kosa gani wakati yeye alitumwa na Mungu akamrubuni Mwanamke? Unakuja kugundua kwamba Shetani ni km Side B ya Mungu, zama ndani

Ukirudi kwenye simulizi ya kitabu cha Ayubu pia yanaibuka maswali mengine kwamba kumbe Mungu ametuweka sisi na Shetani huku duniani akiwa na lengo kwamba sisi turubuniwe na Shetani yaani hio ndio mipango ya Mungu tangu anaanza uumbaji? Emu tujaribu kutafakari hapo usije na majibu mepesi ya kwenye komunio ya kwanza nenda ndani njoo na majibu yenye mashiko
 
Unaona hilo swali la kimtego inamaana Mungu alikua anajua kila kitu maana yeye ndiye mpangaji wa kila kitu kila kilichopo na kilichotokea kilipangwa na yeye mwenyewe Adamu na Hawa wala hawakujua mipango ya Mungu kumbe Mungu alikua amepanga kuwatimua kwa kumtumia Shetani km Chambo ila kila kilichokua kinaendelea alikua anaona lab rat wanavyofanya anawachora tu kashajua huyu panya akipita hata atatokea pale ataenda pale nikimtoa hapa nitamuweka pale umeona hio kitu hapo au bado umefumbwa macho? Mungu mpango mzima alikua anaujua mpaka stage ya kuwatimua itakuaje alikua anajua kila kitu maana alishaandaa kila kitu ukizama deep utaelewa jambo kwamba kila lililotokea lilikua ni mpango wake yeye mwenyewe unakuja kugundua Shetani kasingiziwa yaan Mungu alishindwa kumzuia Shetani pale alikua anamuona au Mungu alienda kwa Mwanamke akiwa kwenye umbo la Shetani? Maswali magumu km hayo unabidi ujiulize kwanza
Ukweli ni kwamba shetani hakusema uongo wowote bali alimwambia ukweli halisi Eva.

Na nukuu halafu tuchambue verse by verse.

Mwanzo 3:1-7, 22-23 (KJV) Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?
Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula;
lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.
Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa,
kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.
Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala.
Wakafumbuliwa macho wote wawili wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini, wakajifanyia nguo.
Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele;
kwa hiyo Bwana Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa.


UCHAMBUZI KWA KINA.

4* Nyoka alimwambia Kwa kumhakikishia 100% kuwa hakika hamtakufa. Funguka la5 anampata ukweli 100% kuwa Mungu anajua siku mkila matunda hayo mtafumbuliwa macho Nanyi mtakuwa kama Mungu Kwa kujua mema na mabaya.Ni ukweli walifumbuliwa macho na wakajua mema na mabaya.


Funguka la7 linaweka ukweli huo kuwa walifumbuliwaacho "Mara macho Yao yakafumbuliwa" Hadi hapa tunaona shetani hakusema uongo kabisa Bali ukweli wote.


Ukumbuke fungu la 4 shetani alimwambia mwanamke hakika hamtakufa.... Sasa ukweli wa shetani anauthibitisha Mungu mwenyewe kwenye fungu la 22 na nukuu...

Mwanzo 3:22 (KJV) Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele;

Hapa Mungu mwenyewe anakiri wazi kabisa kuwa huyu mtu amekuwa kama yeye(Mungu) Kwa kujua mema na mabaya. Mungu anasema lazima kumzuia huyu mtu kula lile tunda la mti wa uhai(uzima) kwani akilila ataishi milele. Fungu la 23 Mungu anachukua maamzi ya kumtimua huyu mtu Busta Nini. Shetani hakuwa na kosa kabisa Bali aliwaeleza ukweli akiwa hakikisha hawatakufa kama tu wangekula lile tunda la uzima(uhai) maana hatujawahi ona kuwa kulikuwa na tunda la kifo ama mauti halikuwepo hivyo adamu angelikuwepo Hadi Leo kama asingefukuzwa na Mungu mwenyewe.
 
Ukweli ndo huu mara tu tukiulizwa swali hili upo wapi? maswali huwa ni mengi sana kichwani.

Ukiwa sehemu hatarishi hapo sasa ndo wasiwasi unakuwa mkubwa unajiuliza hivi kaniona au kaambiwa nilipo.

Inaweza chukua dk1-2 kujibu swali hili mazee.Mara nyingi huwa ni mtego usikurupuke kujibu kama uko
eneo tatanishi mazee.

Imagine Mungu mjuzi wa yote na mwenye uweza wote nikweli alikuwa hamuoni Adamu alipokuwa amejificha? jibu alikuwa anamuona ila ni mtego tu.

kuwa makini kujibu swali hili hasa akiuliza wife /mchepuko!
🤣🤣🤣Ni kweli kabisa aisee
 
Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?
Sasa umegundua kwanini nasema Shetani ni Side B ya Mungu? Soma hio verse kwa umakini utulivu kabisa bila kupepesa macho kisha soma hii verse hapa chini
(Mungu) Akasema: Ni nani aliyekuambia ya kuwa u uchi? Je! Umekula wewe matunda ya mti niliyokuagiza usiyale?
Utaona ile kule juu ni Side A na hii chini ni Side B

Km una kichwa chepesi huwezi kunielewa
 
Sasa umegundua kwanini nasema Shetani ni Side B ya Mungu? Soma hio verse kwa umakini utulivu kabisa bila kupepesa macho kisha soma hii verse hapa chini

Utaona ile kule juu ni Side A na hii chini ni Side B

Km una kichwa chepesi huwezi kunielewa
Nimeshaeleza comment no67 mkuu
 
kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.
Sasa soma vizuri hapo nilipoweka bold maana yake Shetani alitaka Adamu na Hawa wawe Miungu? Au alitaka kuona nini kitajiri baada ya hicho kufanyika? Hivi una uhakika gani km Mungu hakua ndie Shetani aliemrubuni huyu Mwanamke? Inafikirisha eeh
 
Sasa soma vizuri hapo nilipoweka bold maana yake Shetani alitaka Adamu na Hawa wawe Miungu? Au alitaka kuona nini kitajiri baada ya hicho kufanyika? Hivi una uhakika gani km Mungu hakua ndie Shetani aliemrubuni huyu Mwanamke? Inafikirisha eeh
Sheani alikuwa anamwambia ukweli kuwa watakuwa kama mungu kama mungu mwenyewe alivyo sema kwenuye aya ile ya 22 na aya ya 23 akachukua uamzi wa kumtimua mwanadamu mle busatanini
 
Okay nilitaka ujae humo sasa ngoja nikupeleke katikati ya kina kirefu cha bahari, Mungu ndio muweza wa vyote ilishindikanaje akashindwa kuweza kumzuia Shetani asimrubuni yule Mwanamke au ni Mungu ndie aliemtuma Shetani?

Na km ni Mungu ndie aliemtuma Shetani km ilivyoandikwa kwenye kitabu cha Ayubu ukiacha na story ya uasi wa Malaika ila ukija kwenye story ya Adamu na Hawa unaona Shetani alitupwa Duniani pamoja nao, sasa kwanini km ni Mungu alimtuma Shetani akamrubuni Mwanamke kwanini Mungu awatupe Adamu na Hawa pamoja na Shetani wakati ni yeye Mungu aliemtuma Shetani akamrubuni yule Mwanamke? Shetani alikua na kosa gani wakati yeye alitumwa na Mungu akamrubuni Mwanamke? Unakuja kugundua kwamba Shetani ni km Side B ya Mungu, zama ndani

Ukirudi kwenye simulizi ya kitabu cha Ayubu pia yanaibuka maswali mengine kwamba kumbe Mungu ametuweka sisi na Shetani huku duniani akiwa na lengo kwamba sisi turubuniwe na Shetani yaani hio ndio mipango ya Mungu tangu anaanza uumbaji? Emu tujaribu kutafakari hapo usije na majibu mepesi ya kwenye komunio ya kwanza nenda ndani njoo na majibu yenye mashiko
Ufunuo wa Yohana 12:14-17

[14]Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.

[15]Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.

[16]Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.

[17]Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.

Nimekupa kisa hicho ili kujenga msingi wa hoja, mstari wa mkazo ni huo wa 17, shetani anadili na wanaoshika amri za Mungu, lengo lake ni kutaka kuona hakuna anayemtii Mungu.

Ayubu 1:6-7
[6]Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za BWANA, Shetani naye akaenda kati yao.

[7]BWANA akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu BWANA, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.

Kwenye Kisa cha Ayubu iangalie hiyo mistari miwili, wana wa Mungu walikuwa wanaenda kumuabudu naye shetani alikuwa miongoni mwao lakini sio kuabudu alikuwa na lake jambo, akitafuta wa kumdaka.

Nikija kwenye hoja:

1. Shetani yupo kwa ajili ya kupingana na Mungu

2. Shetani anazuia wanadamu wasimtii Mungu kinyume chake wamtii yeye,

3. Wakiwepo wa kumtii Mungu anafanya vita juu yao, kama tulivyoona kwenye ile mistari pale juu.

Sasa:
Mungu atamzuia shetani kwako endapo tu wewe unamtii Mungu, Mungu alimzuia Shetani asimuue Ayubu kwa sababu Ayubu alikuwa anamtii Mungu
 
Back
Top Bottom